Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/88 kur. 1-2
  • Kutunza Mbegu ya Ufalme

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutunza Mbegu ya Ufalme
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ZIARA ZA KURUDIA ZINAWEZA KUWA MAFUNZO
  • Wanatakwa—Mapainia-Wasaidizi 2,500
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Tangazeni Kotekote Sifa Bora za Yehova
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Mradi Mzuri kwa Ajili ya Mwaka Mpya wa Utumishi
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Je! Wewe Unaweza Kufanya Upainia Msaidizi?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 2/88 kur. 1-2

Kutunza Mbegu ya Ufalme

1 Mkulima anatayarisha ardhi na kupanda mbegu, halafu ni shangwe na uradhi ulioje anaohisi mbegu inapochipuka! Ingawa jitihada inahitajiwa kwa upande wake, yeye atafanya kazi ngumu kwa shangwe akiwa na tumaini la kuwa na mavuno mazuri. Yesu alifananisha “neno la Mungu” kwa mbegu iliyopandwa. (Luka 8:11) Basi, tutataka kuwa na shirika kamili katika kupanda mbegu ya Ufalme, yaani, “neno la ufalme” tukiwa na tumaini la kwamba itawafikia watu ambao mioyo yao inathibitika kuwa kama “udongo mzuri,” ulioelezwa katika mfano wa Yesu.—Mt. 13:19, 23, Luka 8:15.

2 Je! wewe ulikuwa na pendeleo la kuangusha vingine vya vitabu vya zamani mwezi uliopita, au je! wewe ulikuwa na mazungumzo mazuri ya Kimaandiko pamoja na watu walio katika eneo lako? Je! wewe unaweza kufanya zaidi ili kukuza kupendezwa kwao katika ujumbe wa Ufalme? Ziara za kurudia ni njia yenye matokeo ya kutunza kupendezwa kunakoonyeshwa. Ziara hizi zinaweza kufanywa kwa muda wa siku moja au mbili baada ya ziara ya kwanza.

3 Wakati wa mwezi wa Februari, tuna nafasi zaidi kutoa vitabu vya zamani. Jambo fulani linalopatikana katika kimojapo huenda likawa ndilo jambo ambalo mtu mwenye kupendezwa anahitaji ili kuamsha tamaa ya kufanya maendeleo kiroho. Pia, uwe tayari kushiriki mambo fulani kuhusu baraka ambazo Ufalme utawaletea wale wenye mioyo yenye kutaka kupokea.

4 Upainia msaidizi utawaandalia wengine nafasi ya kupanua utumishi wao, kufanya ziara za kurudia, na labda kuanzisha mafunzo mapya. Kila mwaka akina ndugu na dada wengi wanatumia nafasi ya kufanya upainia msaidizi katika Machi na Aprili. Mwaka huu Aprili ina Jumamosi tano, faida inayoonekana waziwazi kwa wale ambao wana kazi za kimwili za wakati wote. Huenda wahubiri wadogo wakatumia kipindi cha sikukuu ya ulimwengu ya Ista kushiriki katika huduma ya shambani.

5 Katika makundi kadhaa, baraza zima la wazee, watumishi wa huduma, na wake zao wameweka kielelezo kizuri kwa kufanya upainia msaidizi. Aprili uliopita kundi moja lilikuwa na mapainia wasaidizi 83 na wa kawaida 12. Hicho ni chanzo kilichoje cha kitia-moyo kwa makundi yote! Yehova na abariki mpango wenu wa uangalifu!

ZIARA ZA KURUDIA ZINAWEZA KUWA MAFUNZO

6 Ili uwe mwenye matokeo unapofanya ziara za kurudia, unahitaji kuwa umeandika maandishi yanayofaa kwenye kikaratasi chako cha nyumba kwa nyumba. Jambo hili litakusaidia wewe uamue habari utakayozungumzia unapofanya ziara ya kurudia. Wahubiri wengine wanapenda kumwacha mwenye nyumba aongeee sana wakati wa ziara ya kwanza na kwa njia hiyo wanapata kujua anachofikiri na habari ambazo zinampendeza yeye. Ikiwa mtu huyo anaelezo maoni yenye makosa, huenda likawa jambo la hekima kuepuka kukazia fikiria maelezo hayo mwanzoni, na badala yake, kukazia ahadi za Ufalme.

7 Kazi ya funzo la Biblia ndiyo njia kuu ambayo kupitia kwayo watu wanasaidiwa kujifunza makusudi ya Yehova. Huenda ukatumia jambo fulani katika vitabu ambalo unahisi kwamba linaweza kumpendeza sana mtu huyo. Uliza swali, kisha onyesha jinsi kichapo kinavyoandaa mara moja jibu la Biblia. Zungumzia mafungu kadhaa ikiwa wakati unaruhusu. Mwelekeo unaofaa unaonyesha kwamba sisi tumesadikishwa kikweli kwamba kile ambacho tunacho ni kizuri. Kwa kulifikiria kusudi lako, wewe pia wapaswa kuwa na uwezo wa kuanzisha mafunzo mazuri ya Biblia karibuni. Unaweza kutumia kitabu ambacho ulimwangushia mwenye nyumba au kile ambacho tayari yeye anacho. Badiliko la kuingia kwenye kitabu Kuishi Milele linaweza kufanywa mara moja unapohisi kwamba linafaa.

8 Je! si jambo lenye kuvutia sana kupanda mbegu halisi na kisha kuitazama mimea ikikua tunapoitunza? Tutakuwa na uradhi mkubwa zaidi wakati tunapoona “neno la ufalme” likipata mizizi na kukua ndani ya mioyo ya watu mmoja mmoja tunaojifunza nao. Wanapoingia katika ukweli, wao wanakuwa chanzo cha sifa na heshima kwa Yehova. Na abariki sana jitihada zetu tunapopanda mbegu ya Ufalme kisha kutunza kile ambacho inatokeza, kwa sifa yake!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki