Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/88 uku. 2
  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Vichwa vidogo
  • JUMA LINALOANZA FEBRUARI 1
  • JUMA LINALOANZA FEBRUARI 8
  • JUMA LINALOANZA FEBRUARI 15
  • JUMA LINALOANZA FEBRUARI 22
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 2/88 uku. 2

Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

JUMA LINALOANZA FEBRUARI 1

Wimbo 68 (133)

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Watie moyo wote washiriki katika utumishi wa shambani Jumapili ya kwanza ya Februari.

Dak. 15: “Kutunza Mbegu ya Ufalme.” Mazungumzo ya maswali kwa majibu.

Dak. 15: Kujitayarisha kwa ajili ya Ziara za Kurudia. Mazungumzo: Mzee na wahubiri wawili au watatu wanaostahili wanakuwa na kipindi cha kufanya mazoezi kuzungumzia yale ambayo wao watasema wakati wanafanya ziara za kurudia kwa watu ambao wameonyesha kupendezwa.

Dak. 7: Toleo la Februari. Zungumzia habari ambazo zinaweza kutumiwa kwa matokeo mazuri na wachanga na wahubiri wapya pamoja na wale ambao wana ujuzi zaidi.

Wimbo 58 (130) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA FEBRUARI 8

Wimbo 100 (180)

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Tia shukrani za Sosaiti kwa michango. Watie moyo akina ndugu wategemeze utendaji wa siku ya magazeti Jumamosi ya pili ya mwezi.

Dak. 15: “Kutangaza Habari Njema—Kwa Kutumia Biblia.” Maliza habari kwa mazungumzo pamoja na wasikilizaji juu ya mambo yanayoifaa habari katika mafungu 1-5. Baada ya hapo, mhubiri aliyejitayarisha vizuri atoe wonyesho kuhusu jinsi tunavyoweza kutumia Biblia kwa matokeo mazuri hata kama mtu ana shughuli na, ikitegemea hali, atoe toleo la kitabu, aache trakti, au atayarishe njia kwa ajili ya kufanya ziara ya kurudia kama inavyoonyeshwa kwenye fungu 6. Malizia kwa shauri lenye uchangamfu na la kuonyesha hangaikio kwamba akina ndugu wafikirie kwa uzito kutumia Biblia sana katika huduma ya shambani.

Dak. 20: “Roho ya Ulimwengu.” Hotuba ikitolewa na mzee kutoka kitabu Reasoning, kurasa 389-93. Tumia habari kwa mahitaji ya kundi la kwenu, ukikazia umuhimu wa kuepuka roho ya ulimwengu huu yenye kudhuru.

Wimbo 90 (166) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA FEBRUARI 15

Wimbo 108 (200)

Dak. 10: Matangazo ya kwenu, Habari za Kitheokrasi, na matangazo yaliyochaguliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.

Dak. 15: “Wasaidie Wazee-Wazee na Wagonjwa.” Mazungumzo ya makala kwa maswali na majibu.

Dak. 10: Sisi Tunafanyaje Mahali Petu? Mazungumzo pamoja na wasikilizaji juu ya kuwasaidia wazee-wazee na wagonjwa katika kundi lenu. Toa madokezo yanayofaa kulingana na mahitaji ya kwenu.

Dak. 10: Ni Jinsi Gani Unavyoweza Kuwa na Marafiki wa Kweli? Hotuba ikitegemea Mnara wa Mlinzi wa Septemba 15, 1987, kurasa 5-7.

Wimbo 85 (158) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA FEBRUARI 22

Wimbo 5 (28)

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Tia ndani wonyesho mmoja au mawili ya sekunde 30-60 yakionyesha toleo la magazeti ya karibuni kwa ajili ya Jumamosi ya nne ya mwezi.

Dak. 18: “Fanya Mikutano Iwe Yenye Kufundisha Zaidi.” Mazungumzo ya makala kwa maswali na majibu ikiongozwa na mzee. Zungumzia maandiko ambayo yametajwa kwenye makala. Baada ya kuzungumzia fungu la 5, tia ndani mazungumzo ya dakika tano kati ya ndugu wawili yakikazia uhitaji wa kukaza fikira sana na kukuza ustadi wa kusikiliza vizuri. Angalia habari katika Kiongozi cha Shule, kurasa 25-7, mafungu 6-14.

Dak. 17: “Tumia Vitolewaji Vipya Ili Kufanya Mapenzi ya Mungu.” Mazungumzo machangamfu pamoja na wasikilizaji. Wavute watoe maoni ya kibinafsi juu ya walivyohisi vitolewaji vipya vilipotangazwa na wakati vichapo vilipopokewa. Mkazo wapasa utolewe kuhusu umuhimu wa kutumia maandalizi haya kutoka kwa Yehova ili kuhubiri na kufundisha habari njema.

Wimbo 9 (26) na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki