Kutokosa Kusudi la Huduma Yetu ya Shambani
1 Katika sehemu nyingi leo mhubiri anaweza kutumia saa moja au mbili katika huduma ya shambani bila kupata nafasi ya kumtolea mtu ushuhuda au kuangusha kitabu cho chote. Labda watu wachache wamo nyumbani, au mtu fulani anapopatikana nyumbani huenda akatuambia kwamba ana dini yake mwenyewe na hapendezwi kubadili. Huenda mwingine akasema: “Unafanya kazi nzuri, lakini dini yangu inanipa vitabu vyote ninavyohitaji.” Jambo hili linapotokea je! sisi tunasema tu “Asante” na kuendelea na mlango unaofuata, au angalau tunajaribu kueleza kusudi la ziara yetu?
2 Yesu alipata matatizo yanayofanana na haya katika huduma yake. Wakati wanafunzi fulani wa Wafarisayo waliposema: “Mwalimu, twajua ya kuwa wewe u mtu wa kweli, na njia ya Mungu waifundisha katika kweli,” yeye bila kusita-sita alitoa ushuhuda wenye matokeo sana hivi kwamba wao wakastaajabia yale aliyoyasema. Yeye hakuruhusu kusifu-sifu kwao kusikostahili kumkatize asitoe ushuhuda kwa ujasiri.—Mt. 22:15-22.
YENYE HARAKA ZAIDI SASA
3 Siku moja tutafanya ziara yetu ya mwisho kwa watu walio katika eneo letu. Kila wakati tunaposhiriki huduma ya shambani, tunapaswa kufanya hivyo tukilifikiria jambo hilo. (2 Kor. 6:2; Isa. 55:6) Watu wapaswa waonywe kwamba “siku ya kisasi” ya Yehova iko karibu, nao lazima wasaidiwe ili wapate njia ya pekee ya kuokolewa.—Isa. 61:1, 2; Ezek. 33:8, 9.
4 Tunapotoa toleo la kitabu la sasa, tunapofanya kazi ya magazeti, au kufanya ziara ya kurudia, usiache kusema kweli kwa adhama, busara, na adabu njema. Sikuzote mwonyeshe mwenye nyumba staha inayostahili, na wakati ule ule, fanya yote ambayo unaweza kufanya ili umsaidie mwenye nyumba aelewe kusudi la ziara yako.
KUTIMIZA KUSUDI LETU KATIKA APRILI
5 Maneno yako ya kwanza ni ya maana sana. Yale ambayo unasema katika utangulizi wako mara nyingi yanaamua kama utavuta uangalifu wa mtu na kuweza kuendeleza mazungumzo. Ni nini vingine vya vipingamizi vinavyopatikana katika sehemu yako? Afadhali uzushe kimojapo cha hivyo katika utangulizi wako.
6 Mathalani, ikiwa watu walio katika eneo lako wana mbetuko wa kidini na eneo hilo linaenezwa mara kwa mara, huenda ukauliza hivi: “Yamkinika unatambua kwamba sisi ni Mashahidi wa Yehova. Ikiwa wewe binafsi unashirikiana na mojapo ya makanisa yaliyo katika sehemu hii, huenda wataka kujua kwa nini tunazuru mara nyingi. [Ruhusu maelezo.] Tatizo moja kubwa linalotuhangaisha ni mvunjiko wa jamaa ambao umeenea ulimwenguni pote. World Book Encyclopedia kilisema kwamba: ‘Mierevuko mizima-mizima imeokoka au imetoweka, ikitegemea kama maisha ya jamaa yalikuwa imara au dhaifu.’” Kutoka jambo hilo, elekea kwenye Mwanzo 1:27, 28.
7 Matatizo yanayohusiana na jamaa yatazungumziwa katika matoleo ya Mnara wa Mlinzi ya Aprili na Mei. Kwa hiyo, baada ya kusoma Isaya 48:17, 18, eleza kwa usadikisho kwamba Mnara wa Mlinzi limesaidia mamilioni ya jamaa waishi maisha yenye furaha, yenye matokeo zaidi. Huenda ukataka kutaja jinsi limekusaidia wewe binafsi. Toa maelezo mafupi kuhusu mojapo ya makala kuu na umjulishe mtu huyo kwamba anaweza kupata Mnara wa Mlinzi kupitia posta kwa mwaka mzima.
8 “Muda ubakio si mwingi.” (1 Kor. 7:29) Hatujui ni fursa ngapi ambazo zimebaki kuwatafuta watu wa aina ya kondoo. Watu ambao hawaonyeshi upendo kwa ukweli wanahitaji kuonywa. Ulimwengu ukiwa umepatwa sana na pigo la ubaridi-baridi, lazima tuhubiri ukweli kwa ujasiri na usadikisho kukiwa kungali kuna wakati. (Mdo. 4:29, 31; 14:3) Ikiwa tunafanya sehemu yetu kutimiza kusudi la huduma yetu, tunaweza kuhakikishiwa kwamba “kondoo” wataitikia sauti ya Mchungaji Mwema.—Yoh. 10:4, 27.