Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
JUMA LINALOANZA OKTOBA 3
Wimbo 103 (193)
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yanayofaa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Tia moyo utendaji wa magazeti kwa ajili ya Jumamosi. Dokeza habari za kuzungumzia zinazofaa kadiri wakati unavyoruhusu.
Dak. 18: “Je! Wewe Unahubiri Ukiwa na Kusudi?” Mazungumzo ya makala kwa maswali na majibu. Kazia umaana wa kufanya ziara za kurudia tukiwa na kusudi la kuanza mafunzo ya Biblia. Unapozungumzia fungu la 5, toa wonyesho kuhusu jinsi toleo la uandikishaji linavyoweza kufanywa katika ziara ya kurudia.
Dak. 17: Vijana—Msidanganywe. Hotuba na mahojiano. Vijana ni lengo la pekee la Shetani. Yeye anachagua wale wasio na ujuzi mwingi, akiwatongoza kama alivyotongoza Hawa. (Mwa. 3:1) Anadanganya vijana kwa vivutio, vitamanisho, vishawishi. Anaendeleza wazo la kwamba vijana walio katika ukweli wanakosa bure tu kujipatia jambo fulani lenye raha. (Mwa. 3:4, 5) Anakuza tamaa ya kibinafsi ya kufanya lako mwenyewe, ujiamulie mwenyewe lililo jema na baya. Shetani anafanya njia za ulimwengu, kama vile ukosefu wa adili katika ngono, kuvuta sigareti, matumizi mabaya ya dawa za kulevya, ushirika pamoja na wasioitikadi, na vitumbuizo vya ulimwengu, vionekane kuwa vyenye kuvutia. Anafanya vionekane kuwa visivyo na madhara, kama vile tunda mtini lilivyoonekana kwa Hawa. (Mwa. 3:6) Vijana Wakristo wanapaswa kuwa na mwelekeo gani kuhusu vitu hivi, na kwa nini? (1 Yn. 2:15-17) Kwa kuwa ulimwengu unapita, vijana wanapaswa kufuatia miradi gani? (Mt. 6:33; 24:14; 28:19, 20) Yehova hufanya uandalizi wa kuwahami vijana wasidanganywe: Kitabu Ujana, broshua Shule, Amkeni! inayozungumzia “Vijana Wanauliza,” mikutano, makusanyiko, wazazi, na wazee. Kwa nini kutumia maisha katika utumishi wa Yehova ni njia bora zaidi ya maisha? (Mit. 27:11; Mhu. 12:1) Kadiri wakati unavyoruhusu, hoji kijana mmoja au wawili walio vielelezo vizuri ambao wamekuza tamaa zinazofaa. Pata kujua ni nini kimewasaidia wapinge mikazo shuleni. Kazia uhitaji wa wengine kuwasaidia vijana ili wabaki wakiwa washikamanifu na wasidanganywe na ulimwengu.
Wimbo 73 (157) na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA OKTOBA 10
Wimbo 66 (129)
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na ripoti ya hesabu.
Dak. 20: “Ongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo.” Maswali na majibu. Wakati wa kuzungumzia fungu 4, toa wonyesho wa painia au mhubiri mwenye ujuzi akionyesha jinsi funzo linavyoweza kukomeshwa. Toa hesabu ya mafunzo ya Biblia yanayoongozwa na kundi. Yamefanya maendeleo gani? Watie moyo kwa uchangamfu wote wanaoongoza mafunzo wachunguze matokeo ya kila mmoja kulingana na habari hii. Wowote wanaohitaji msaada wanaweza kuzungumza na mwangalizi wa utumishi au kiongozi wa funzo la kitabu.
Dak. 15: Kutia Nguvu Jamaa Zenye Mzazi Mmoja. Mzee anayestahili ahoji wazazi watatu au wanne walio peke yao. Fikiria mambo kihalisi. Wanakabili matatizo gani yasiyo na kifani? Wamejifunza kukabiliana na hali yao jinsi gani? Ni katika njia zipi kundi limekuwa lenye kuunga mkono? Wameweka miradi gani ya kibinafsi au ya jamaa nayo imesaidia jamaa jinsi gani? Uwe mwenye mwelekeo chanya na uwasifu sana kwa kuchangia kwao hali ya kiroho ya kundi. Wakumbushe wote uhitaji wa kuwakumbuka hawa katika sala zetu.—2 The. 1:11, 12.
Wimbo 107 (190) na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA OKTOBA 17
Wimbo 51 (92)
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Zungumzia matangulizi katika kitabu Reasoning ambayo yanaweza kutumiwa pamoja na Kichwa cha Mazungumzo na yangefaana na eneo la kwenu. Onyesha kwa nini matangulizi hayo yatakuwa yenye matokeo.
Dak. 17: “Kutangaza Habari Njema—Kwa Ujasiri, Lakini kwa Busara.” Mazungumzo ya maswali kwa majibu. Toa wonyesho mmoja wa vielelezo vinavyotajwa katika fungu 3, ukitumia kitabu Reasoning.
Dak. 8: “Maandikisho.” Ndugu anayestahili apaswa kusoma mafungu yote na kutia ndani maelezo yanayofaa.
Dak. 10: Mahitaji ya kwenu. Rudieni madokezo ya kufanya maendeleo kama ilivyo katika ripoti ya mwisho ya mwangalizi wa mzunguko.
Wimbo 113 (2) na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA OKTOBA 24
Wimbo 55 (106)
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Tia moyo wote washiriki katika kazi ya magazeti Jumamosi au siku ya soko.
Dak. 20: “Kusaidia Wengine Watumikie Yehova kwa Nafsi Nzima.” Mazungumzo yakitolewa na mwangalizi msimamizi. Painia wa kawaida mwenye ujuzi atoe wonyesho juu ya jinsi ya kuwa na mazungumzo yanayogusa moyo pamoja na mwanafunzi wa Biblia ambaye anahudhuria mikutano kwa ukawaida lakini anajizuia kubatizwa. Tumia makala ya Mnara wa Mlinzi wa Februari 15, 1982 “Ni Nini Kinachonizuia Nisibatizwe?” Hoji mmoja au wawili walio katika utumishi wa wakati wote, ukiwauliza ni nani aliyewatia moyo na kuwasaidia wafanye marekebisho ili wawe katika utumishi wa wakati wote. Waulize wanafanya kazi kuelekea miradi gani zaidi.
Dak. 15: “Kunufaika Kutokana na Utii kwa Agizo la Kimungu.” Mazungumzo ya jamaa yakikazia mijibizo chanya kuhusu programu ya siku ya kusanyiko la pekee la kwanza na hamu ya programu mpya.
Wimbo 58 (130) na sala ya kumalizia.