Matangazo
● Toleo la fasihi kwa Novemba: New World Translation pamoja na kitabu “Ufalme Wako Uje.” Desemba: Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia au Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Januari na Februari: Chochote cha vitabu vyenye kurasa 192 ambacho kilitangazwa kabla ya 1980 na hakikuchapishwa kwenye karatasi nzuri sana kwa nusu ya mchango wa kawaida.
● Makundi yanapaswa yaanze kuagiza Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova cha 1989 katika maagizo yao ya fasihi ya Novemba. Kitabu cha mwaka kitapatikana katika Kiingereza, Kifaransa, na Kiswahili. Vitabu vya Mwaka ni bidhaa za kuagizwa kwa kiasi. Mapainia wa kawaida na wa pekee ambao wamekuwa kwenye orodha kabla ya Julai 1, 1988, wanaweza kupokea nakala moja ya bure, na kundi linaweza kuomba kupunguziwa bei.
● Wakati wa 1989 Amkeni! itakuwa na sehemu katika matoleo kadha wa kadha yenye kichwa “Wakati Ujao wa Dini kwa Kutegemea Wakati Uliopita.” Makala hizi zinachunguza wakati ujao wa dini kwa kutazama nyuma historia ya kidini na kutumia kanuni ya kisababishi na athari. Wahubiri wanaombwa watayarishe utoaji mzuri na kuonyesha habari hizo wakati wowote inapofaa. Katika njia hiyo, watu ambao wanahangaishwa na kupungua kwa dini leo wanaweza kusaidiwa wajifunze juu ya tumaini la Ufalme.
● Mojapo drama zitakazoonyeshwa kwenye “Haki ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya inategemea Ezekieli 9:1-11 na Hesabu 35:1-34. Nyingine inategemea Mwanzo 6:1–7:24; 18:20–19:26. Kila mmoja apaswa kusoma habari hiyo ili anufaike na drama zitakazotolewa.
● Ikiwa Funzo la Kitabu la Kundi halitaongozwa wakati wa juma la mkusanyiko, nusu ya habari iliyogawiwa juma hilo inaweza kusomwa juma linalotangulia mkusanyiko na nusu ile nyingine juma linalofuata baada ya mkusanyiko. Katika njia hiyo habari hii yenye maana haitakosa kusomwa.
● Bei mpya za uandikishaji wa ndege kwa nakala moja moja: KShs. 350/= mhu.; 318/= pai; Tshs. 1,856/= mhu.; 1,766/= pai; FRw 1,660 mhu.; 1,470 pai; SRps. 67.50 mhu.; 53.50 pai; S£ 88.00 mhu.; 82.00 pai; Ushs. 3,910 mhu.; 3,510 pai.
● Tafadhali kumbukeni kwamba trakti ni za kugawanywa bure. Watu hawaombwi kuzilipia ingawa wahubiri na mapainia wanazichangia wanapozipokea kutoka kwenye kaunta ya fasihi.
● Vinavyopatikana: Kiingereza
Creation, chapa ya kawaida, ndogo
Maisha ya Jamaa; Kalenda ya 1989
Ibada; Uzima uu Huu; Kweli
Biblia chapa ya kawaida; Ufalme Wako Uje; Word of God
Kitabu cha Nyimbo, chapa ndogo;
Biblia yenye marejezo; Konkodansi
Deluxe Bible–Chapa ya kawaida na ya mfukoni
● Kaseti—Ezekiel, Isaiah, Romans, Proverbs, Luke, Samuel, 1 Kings, Joshua, Judges, Deuteronomy
Kiswahili:
Huduma Yetu; Ujana Wako
Vichwa vya Mazungumzo