Unakaribishwa Kwenye “Ujitoaji Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1989!
1 Katika majuma machache tu, programu yenye kujenga kiroho itaanza, nawe waalikwa! Katika Afrika Mashariki, “Ujitoaji Kimungu” Mikusanyiko ya Wilaya itaanza Novemba 3 na imeratibiwa kuendelea mpaka Januari 1990. Kutakuwa na jumla ya mikusanyiko 11, hesabu kubwa zaidi kuliko wakati mwinginewo wote. Yehova mwenyewe anafanya uandalizi huu kupitia tengenezo lake, kwa hiyo tunaweza kuhudhuria tukiwa na matazamio ya hali ya juu ambayo hayatatamaushwa.—Zab. 61:4; Isa. 54:13.
2 Mwaka huu mikusanyiko itakazia uhitaji wa ujitoaji kimungu na itatuchochea tufanye maendeleo katika kutumia sifa hii. Hili ni jambo la maana sana kwa sababu ya ulimwengu usiomcha Mungu unaotuzunguka.
3 Kupitia mazoezi na nidhamu ya hatua kwa hatua, Yehova ametufanya tuwe watu wasio na kifani, wenye umoja katika tengenezo lenye kutokeza huku tukiwa katikati ya kizazi kisichojali. Ujitoaji kimungu wetu ni wa kweli na hauna unafiki ambao Paulo alieleza alipotaarifu kwamba katika siku za mwisho, watu wangekuwa na umbile la kujitolea Mungu lakini wakithibitika kuwa mabandia kwa nguvu zalo. (2 Tim. 3:1, 5, NW) Roho yetu ya kushirikiana na ionyeshe ujitoaji kimungu nyakati zote, na sikuzote tuthibitishe kuwa kweli kwa nguvu zao.—1 Kor. 14:40.
4 FIKA MAPEMA: Watu wa Yehova wanajulikana vizuri sana kwa sababu ya kutegemeka kwao na kufika kwa wakati. (Luka 16:10) Hili ni jambo la maana tunapohudhuria mkusanyiko. Tunapaswa kufika mapema kila siku na tuwe tumeketi kabla ya programu kuanza. Hii inataka kuruhusu wakati wa kutosha kutunza mambo yanayohitaji kuelekezewa fikira, kama vile kuegesha gari letu, kupata viti vinavyofaa kwa ajili ya jamaa yetu, na kupata tikiti za chakula za mkusanyiko.
5 Wakati wa mkusanyiko unatoa fursa nzuri ya kuonea shangwe ushirika mzuri. Lakini kutembelea marafiki mpaka usiku sana kunaweza kuzuia jitihada zetu za kufika kwa wakati siku inayofuata. Wasiwasi mwingi na mtamauko unaweza kutokea kwa sababu ya kuanza tukiwa tumechelewa na kwa sababu hiyo kufanya haraka haraka asubuhi. Ili kuzuia jambo hili, jamaa fulani zinaona kuwa jambo lenye mafaa kuweka wakati mzuri wa kwenda kulala. Kwa kushikamana na ratiba hiyo kwa uthabiti, yaelekea wanapata pumziko zuri usiku na wanakuwa tayari kuanza mapema kesho yake. Hili linawaepusha kufika programu ikiendelea, jambo ambalo linakengeusha fikira na linaweza kuudhi wale ambao tayari wameketi. Kuwafikiria wengine katika jambo hili kunaweza kuwa wonyesho wa kicho na staha yetu kwa Yehova, na kunatoa ushuhuda wa ujitoaji kimungu ulio wa kweli.
6 MKUSANYIKO WA SIKU TATU: “Ujitoaji Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya utakuwa wa siku tatu. Habari zilizochaguliwa kwa uangalifu ambazo ni za muhimu kwa afya yetu ya kiroho zitatolewa kwenye kila pindi. Habari mbalimbali zinazohusiana na ujitoaji kimungu zitazungumziwa katika hotuba, maonyesho, na drama ya ki-siku-hizi.
7 Azimia kutokosa hata kipindi kimoja. Huenda hili likataka kujidhabihu kibinafsi na kufanya marekebisho katika ratiba yako. Wengine wanaliona kuwa jambo linalohitajiwa kufanya mipango ya pekee pamoja na mwajiri wao. Wengine hata wanaacha faida za kifedha ili waweze kuhudhuria vipindi vyote. Hakika Yehova atabariki wote ambao wanasali kwa moyo mweupe kuhusu jambo hili na kujitahidi kutoka moyoni ili wahudhurie.—Luka 13:24.
8 SIKILIZA KWA UMAKINI: Wakati wa programu ya mkusanyiko, usikengeushwe fikira na mambo ya kuona na sauti ambazo hazihusiani na habari inayozungumziwa kwenye jukwaa. Jinsi tulivyo wenye shukrani kwa Yehova aliyetupa zawadi ya uwezo wa kukaza fikira “kwa umakini” kuelekea mawazo ambayo tunachagua. Ujitoaji kimungu wetu unapaswa utuchochee kufanya uamuzi unaopatana na ombi la Yehova kwenye Isaya 55:2: “Nisikilize kwa bidii [umakini, NW].”
9 Ingawa ni kweli kwamba mhadhara wa Jumapili alasiri umetangazwa kwa ajili ya watu wote, habari zilizo nyingi zitakazotolewa kwenye mkusanyiko huu zimetayarishwa hasa kwa ajili ya wale ambao tayari wamejitoa kwa Yehova. Mkusanyiko utatujulisha mahitaji ya karibuni na kutusaidia twende kwa usambamba na tengenezo la Yehova linaloendelea. Kutosikiliza kwa umakini kutatufanya tubaki nyuma. Lazima tujishughulishe sana na programu ili tupate manufaa kamili kutokana na ulishaji mzuri wa kiroho.—1 Pet. 2:2.
10 Kwa muda wa miaka iliyopita, wajumbe wengi wa mkusanyiko wamekuza zoea lenye msaada la kuandika habari wakati wa programu. Vyombo vinavyofaa vya kutumia kuandika habari vinapasa kutiwa pamoja na Biblia na vitabu vya nyimbo kuwa vifaa vya kawaida wakati wa kuhudhuria mkusanyiko. Huenda watu fulani wakawa wanaona kuandika habari kuwa jambo lenye kutiliwa mashaka, wakihisi kwamba halina manufaa. Ikiwa umekuwa na mbetuko huo, mbona usijaribu kuandika habari fulani wakati wa “Ujitoaji Kimungu” Mkusanyiko? Kama ilivyo kweli kwa wengine wengi, huenda ukapata kwamba ni njia nzuri ya kukaza fikira kwa yale ambayo yanasemwa na kwamba linazuia akili zako zisiingiwe na mambo mengine au kutanga-tanga.
11 Mambo ya kuandikwa hayapasi kuwa mengi au yenye maelezo marefu. Kwa kawaida fungu la maneno machache linatosha kwa wazo kuu. Wazee wanaliona kuwa jambo lenye faida kuwa na mambo yaliyoandikwa kwa njia nadhifu kwa ajili ya kuongoza pitio lenye maana la programu ya mkusanyiko wakati wa Mkutano wa Utumishi. Baadaye wanaweza kuunganisha nyingi za habari zilizotolewa kwenye mkusanyiko katika kazi yao ya kufundisha na kufanya uchungaji.
12 Sisi sote tunapaswa tuelekezee fikira tunavyosikiliza, kwa kuwa hilo lamaanisha furaha na uhai wetu wenyewe. Tunapohudhuria “Ujitoaji Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya, tunapaswa kukumbuka mawaidha ya Yehova kwenye Mithali 8:33-35: “Sikieni mafundisho [nidhamu, NW], mpate hekima, wala msiikatae. Ana heri [furaha, NW] mtu yule anisikilizaye, akisubiri sikuzote malangoni pangu, akingoja penye vizingiti vya milango yangu. Maana yeye anionaye mimi aona uzima, naye atapa kibali kwa BWANA [Yehova, NW].”
13 WIMBO NA SALA: Mojapo mapambo yaliyo mazuri sana ya ujitoaji kimungu wetu ni kumwimbia Yehova Mungu sifa. Kuimba kunaonekana kulikuwa sehemu ya kawaida ya Ukristo wa kweli katika karne ya kwanza. (1 Kor. 14:15) Yehova anapendezwa pia watu wake wanapomfikia kwa sala ya moyo. Mikusanyiko ya wilaya inatupa fursa isiyo na kifani ili tuunganike pamoja na maelfu ya ndugu na dada zetu katika kusifu Yehova katika wimbo na sala. Hata hivyo, wengine wameonyesha ukosefu wa staha kwa sehemu hizi za maana sana za ibada yetu. Jinsi gani? Kwa kufika isivyohitajiwa kwenye mkusanyiko wakati au baada ya wimbo na sala ya kufungua. Kwa nini? Katika pindi chache huenda kukawa na sababu nzuri za kufanya hivyo. Hata hivyo, watu fulani wanaweza kuacha pendeleo la kuimba na kujiunga katika sala ili tu wafike kwenye magari yao mapema. Wengine wameondoka kwenye viti vyao ili wawe miongoni mwa wale wa kwanza kwenye mstari ili wapate vitolewaji vya fasihi au chakula. Lazima uangalifu utolewe ili kwa kufuatia manufaa ya kibinafsi, tusiruhusu mtazamo wa kilimwengu wa mimi kwanza au vitabia visivyo vya kimungu kama vile choyo na ubinafsi vizuie maendeleo yetu ya kiroho. Tukiwa watu wa ujitoaji kimungu, tunajitahidi kudhihirisha staha inayofaa kwa sehemu hizi za ibada yetu zilizo bora sana, yaani, kusali kwetu na kumwimbia Yehova.
14 ADABU ZETU ZA KIKRISTO: Kwa muda wa miaka iliyopita, adabu zetu za Kikristo na sura yetu kwenye mikusanyiko vimetuletea sifa njema tukiwa Mashahidi wa Yehova. Hii ni kwa sababu kwa kufaa tunaiona mikusanyiko yetu kuwa sikukuu za kiroho, si vikusanyiko vya kijamaa. Kwa kufaa, tunajitahidi kuonyesha akili timamu ya kiroho na kujiendesha tukiwa wahudumu.
15 Angalia jambo hili lililoonwa na jamaa moja ya Shahidi walipokuwa wakila chakula kwenye mkahawa kwenye jiji moja la mkusanyiko mwaka uliopita. Ndugu aliandika hivi: “Mwanamume mmoja na mke wake walikuwa penye ile meza nyingine karibu na yetu. Walipomaliza mlo wao, mwanamume huyo akasogea karibu na meza yetu, akaomba radhi, na akasema kwamba angependa kutusifu kwa sababu ya sura nadhifu na safi. Mke wangu akamwambia mwanamume huyo kwamba tulikuwa tunahudhuria Mkusanyiko wa Watchtower mwisho-juma huo. Akasema kwamba alikuwa na hakika kwamba tulikuwa tunahudhuria. Alikuwa ameona wengi wa ndugu na dada zetu kuzunguka hoteli wakati yeye na mke wake walipokuwa wakiishi humo; na wote walionyesha mwenendo ulio kielelezo kizuri na mavazi mazuri. Alisema kwamba vijana walio katika kanisa analohudhuria, hawavalii wala kutenda kama vijana wetu. Jambo hili linanifanya nithamini kwa nini ni jambo la maana kuwalea watoto wetu tangu umri mdogo wawe kielelezo kizuri cha Mkristo nyakati zote. Lazima sifa itolewe kwa tengenezo la Yehova kwa shauri lenye nguvu na mwelekezo ili kuweka kielelezo kizuri.”
16 Jambo lenye kuhuzunisha, watu fulani wanaohudhuria mikusanyiko wamekuwa wazembe mno katika mtazamo, mavazi, msemo, na mwenendo wao. Jambo hilo linapoonekana wazi katika kundi la mahali penu au wakati wa mkusanyiko, wale walio na sifa za kiroho wanapaswa watoe shauri lenye upendo wakiwa na maoni ya kufanya mrekebisho-upya. (Gal. 6:1; Efe. 4:11, 12) Ujitoaji kimungu wetu unapaswa utusukume tuwe wenye bidii yenye uendelevu katika kutegemeza sifa yetu njema na kudumisha viwango vya juu vya mwenendo nyakati zote.
17 Bila shaka, programu ya mkusanyiko inapomalizika wengi wanaona shangwe kuwa pamoja kwa ajili ya chakula na ushirika. Hilo linaweza kupendeza na wakati unaweza kutumiwa vizuri katika mazungumzo mazuri tunaposhiriki mambo yaliyoonwa na kufanya pitio la mambo makuu ya mkusanyiko. Inaleta furaha kwetu sisi na utukufu kwa Mungu tunapojiendesha ‘kwa namna inayostahili zile habari njema.”—Flp. 1:27, NW.
18 Kikumbusha kimoja cha mwisho chenye fadhili kinahusiana na kutembeleana na kuzungumziana wakati vipindi vinapoendelea. Ni wazi kwamba tunaterema kuona marafiki kwenye mkusanyiko, lakini staha kwa Yehova na kuwafikiria ndugu zetu kwapasa kuwe jambo kuu akilini mwetu. Kwa sababu hiyo, hatungetaka kuwa tukisumbua-sumbua au kukengeusha fikira za wengine wakati wa programu. Ikiwa inakubidi kuacha kiti chako kwenda kwenye shughuli fulani ya maana, fanya hivyo upesi na kwa utulivu iwezekanavyo. Pia, programu inapoendelea, hakuna mtu anayepaswa kuwa akitembelea wengine kwenye ukumbi. Tuko huko ili tusikilize na kujifunza.—Luka 8:18.
19 KWA WAZAZI: Watoto wachanga na matineja wanaalikwa hasa kuhudhuria “Ujitoaji Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya. Habari nyingi zitakazotolewa zitawatia moyo hasa. Ni jambo zuri kama nini kuona ujitoaji kimungu wa wachanga ambao wamejifunza kuelekeza fikira kwa umakini kwenye mikutano yote ya Kikristo na ambao wanapendezwa sana na programu ya mkusanyiko! (Zab. 148:12) Lakini mengi yanategemea kielelezo na usimamizi wa wazazi. Wachanga wengi wamezoezwa vizuri sana kuandika habari. Ikiwa wewe ukiwa mzazi bado hujawafunza watoto wako kuandika habari, mbona usitumie wakati unaobaki kabla ya mkusanyiko wenu ili ufanye hivyo? Hata walio wachanga sana wanaweza kutiwa moyo kuandika mitajo ya Maandiko na maneno ya msingi yanayohusiana wanayosikia yakisemwa na wasemaji. Wazazi fulani wanapanga kupitia habari kuu kutoka programu ya siku baada ya kurudi mahali pao pa kulala au wanaposafiri kwenda nyumbani.
20 Bila shaka, wazazi walio wengi wanathamini kwamba mbetuko wa asili wa watoto ni kucheza. Hawana maarifa maishani, nao hawajakomaa. Basi, wanapaswa kufundishwa wakati wa kuelekeza fikira na jinsi ya kujiendesha wenyewe kwenye mikutano. Hili linataka usimamizi mzuri wa wazazi wao. Wazazi fulani wamelegea katika sehemu hii. Nyakati nyingine, ingawa huenda wazazi wakawa wanamwonyesha Yehova kicho kinachofaa wakati wa sala, watoto wao wanacheza na kukengeusha fikira za wengine. Wazazi wanapaswa kujua watoto wao wanafanya nini wakati wa sala. Wanafanya nini wanapoondoka kwenye viti vyao wakati wa programu? Je! watoto wanaachwa bila usimamizi wakati na baada ya programu ya mkusanyiko?
21 UTUMISHI WA CHAKULA: Mpango wa utumishi wa chakula uliorahisishwa unaolingana na ule wa mwaka jana unapangwa kwa ajili ya 1989. Jambo hili linarahisisha mzigo wa kazi na kuruhusu kuelekeza fikira zaidi kwenye sehemu ya kiroho ya mkusanyiko, wafanya kazi wakiwa wanaweza kuonea shangwe sehemu kubwa ya programu. (Kut. 12:16b; Kum. 31:12, it Buku 1 kur. 503-4, 821; linganisha Luka 10:38-42.) Orodha ya vyakula inaandaa chakula cha kutosha kwa ajili ya vipindi vya asubuhi na mchana. (Linganisha Mathayo 14:14-20.) Kwa ajili ya chakula cha jioni, kila mtu ana uhuru wa kufanya mipango yake mwenyewe. Huenda chakula cha jioni chenye moto kikaandaliwa saa moja hivi baada ya kipindi kumalizika kwa ajili ya wale ambao wanalala mahali pa mkusanyiko.
22 Sosaiti inathamini sana sana utegemezo mzuri ambao nyinyi akina ndugu na dada mmekuwa mkitoa kwa mipango ya utumishi wa chakula kwenye mikusanyiko ya wilaya kwa muda wa miaka iliyopita. Jambo hili limefanya iwezekane kukodi vifaa vizuri na kushughulikia gharama za mkusanyiko. Limewawezesha pia kubaki mahali pa mkusanyiko wakati wa pumziko fupi la mchana na kuwapo kwa wakati mkiwa mmeburudishwa kwa ajili ya programu ya kiroho iliyo ya maana sana.
23 Ushirikiano wenu kamili unaombwa kwa habari ya kuhifadhi viti. Tafadhali kumbukeni kwamba VITI VINAWEZA KUHIFADHIWA KWA WASHIRIKI WA KARIBU WA JAMAA YAKO PEKE YAO NA WOWOTE AMBAO HUENDA WAKAWA WANASAFIRI PAMOJA NAWE KATIKA GARI LAKO. Tafadhali msiwawekee wengine viti. Nyakati fulani, viti vya ziada haviwekewi mtu fulani hasa. Hili ni jambo la kutoonyesha upendo na linawapotosha wakaribishaji na wengine wanaotafuta viti vilivyo wazi. Kupatana na shauri la Biblia, tunapaswa kukamilisha ujitoaji kimungu wetu kwa kuonyesha shauku ya kidugu na kushirikiana kikamili na mpango unaokubaliwa kwa ajili ya kuhifadhi viti.—2 Pet. 1:5-8.
24 Inadokezwa kwamba uchaguzi mzuri ufanywe kwa habari ya kuleta vitu vya kibinafsi kwenye mahali pa mkusanyiko. Wakati uliopita, watu fulani wameleta mizigo mikubwa ambayo haiwezi kuwekwa chini ya viti. Hii iliwekwa kwenye vijia au juu ya viti. Jambo hili linafanya wengine wanyimwe viti, na hata linaweza kuvunja sheria za kuzima moto na za usalama. Tunahitaji kuonyesha ufikirio katika mambo haya.
25 Matumizi ya kamera za vidio na vifaa vya kunasia sauti yanaruhusiwa kwenye mkusanyiko. Hata hivyo, wale wanaotumia vifaa hivyo wanapaswa kuwa waangalifu ili waepuke kusumbua-sumbua au kukengeusha wengine. Vifaa kama hivyo havipaswi kuwekwa kwenye vijia au kwenye miingilio. Vifaa hivyo havipaswi kuunganishwa kwenye mfumo wa kuhutubia watu wote au matundu ya umeme. Taa zenye mwangaza mwingi hazitaruhusiwa. Wale ambao wanakengeusha fikira au kupuuza yoyote ya miongozo iliyo juu wanapaswa warekebishe jambo hilo bila kukawia wanapoambiwa. Wakaribishaji na wengine wanaosimamia mambo watakuwa macho kurekebisha uvunjaji wowote wa miongozo hiyo, nao wanapaswa kupata ushirikiano kamili wa wale wanaotumia vyombo hivyo.
26 UJITOAJI KIMUNGU WETU utakabili mitihani mikali wakati ujao ulio karibu. “Kwa kweli, wale wanaotamani kuishi kwa ujitoaji kimungu katika ushirika na Kristo Yesu watanyanyaswa pia.” (2 Tim. 3:12, NW) Jinsi tulivyo wenye shukrani kwa Yehova kwa maandalizi ya kiroho kama vile “Ujitoaji Kimungu” Mikusanyiko ya Wilaya, ambako atatuzoeza na “kutuagiza sisi tukatae katakata kutomcha Mungu na tamaa ya ulimwengu na tuishi kwa utimamu wa akili na uadilifu na ujitoaji kimungu katikati ya mfumo huu wa mambo uliopo.”—Tito 2:12, NW.
[Sanduku katika ukurasa wa 10]
Vikumbusho vya Mkusanyiko wa Wilaya
MAHALI PA KULALA: Mipango kwa mwaka huu, kwa sehemu iliyo kubwa, itafuata kiolezo cha miaka iliyotangulia. Mikusanyiko iliyo mingi inatumia vyumba vya kulala au vifaa vilivyo mahali pa mkusanyiko ili wote wanaohudhuria wapate mahali pa kulala. Huenda kukawa na mahali pa kulala katika nyumba za watu binafsi. Hata hivyo, tafadhali kumbukeni kwamba, si jambo linalofaa wajumbe wachukue kivivi hivi tu ukaribishaji wageni wa ndugu zao na kutazamia wawakaribishe kwa siku za ziada ili waweze kuzuru sehemu fulani wakati wa likizo au kufanya mambo mengine kabla au baada ya mkusanyiko. Vyumba hivi ni kwa wakati wa mkusanyiko tu. Wale wanaopata mahali hapo pa kulala wanapaswa wahakikishe kwamba wao na watoto wao wanatenda kwa njia yenye staha kuelekea nyumba ya mkaribishaji wao na wasiharibu kitu chochote au kuchunguza-chunguza miliki au sehemu za kibinafsi za nyumba hiyo. Wenye nyumba wakiwa na matatizo yoyote kuhusiana na jambo hili wanapaswa kujulisha Idara ya Mahali pa Kulala mara moja, na ndugu waliopo watafurahi kusaidia. Mnaweza kupeleka fomu ya maombi ya mahali pa kulala iliyojazwa kupitia msawazishaji wa mkusanyiko katika kundi lenu.
SAA ZA PROGRAMU: Ni mwendo wa hekima na unaoonyesha uthamini wenye staha ikiwa tumeketi programu inapoanza. Katika majiji yote ya mikusanyiko, programu ya Ijumaa itaanza saa 4:20 asubuhi na muziki, kisha wimbo na sala, na vipindi vitamalizika saa 11:10 jioni. Programu ya Jumamosi na Jumapili itaanza saa 3:30 asubuhi. Jumamosi programu itamalizika saa 10:55 alasiri na Jumapili programu itamalizika karibu saa 10:00 alasiri. Hotuba ya watu wote Jumapili itaanza na wimbo na sala saa 8:00 alasiri.
UBATIZO: Wale wanaotaka kubatizwa wanapaswa wajitahidi kuwa kwenye viti vyao katika sehemu iliyoonyeshwa kabla ya programu kuanza Jumamosi asubuhi. Mavazi yenye kiasi na taulo yanapaswa kuletwa na kila mmoja anayepanga kubatizwa. Akina dada hasa watataka kuchunguza kimbele waone kama mavazi wanayopanga kuvaa yanaonyesha uchi yanapolowa maji. (Ona Huduma ya Ufalme Yetu, Novemba 1987, ukurasa 3, fungu 6) Baada ya hotuba ya ubatizo na sala itakayotolewa na msemaji, mwenyekiti wa kipindi hicho atawatolea wanaobatizwa maagizo mafupi kisha ataomba wimbo uimbwe. Kuanzia mstari wa mwisho, wakaribishaji watawaelekeza wenye kubatizwa kwanye mahali pa uzamisho au kwenye magari yatakayowapeleka hapo, huku wahudhuriaji wengine wakimaliza kuimba wimbo. Kwa kuwa ubatizo kwa kufananisha kujiweka wakfu kwa mtu ni jambo la usiri na la kibinafsi kati ya mtu na Yehova, hakuna uandalizi kwa unaoitwa ubatizo wa mshiriki ambao watu wawili au zaidi wanaotaka kubatizwa wanakumbatiana au kushikana mikono wanapobatizwa.
KITAMBULISHO CHA MAPAINIA: Mapainia wote wa kawaida na wa pekee, na waangalizi wasafirio pia watahitaji kuleta Kitambulisho na kadi yao ya Mgawo [S-202] kwenye mkusanyiko. Wale ambao watakuwa wamefikisha miezi sita tangu waanze upainia wakati wa mkusanyiko wa wilaya watakaouhudhuria wanaweza kupokea tikiti za chakula za mikusanyiko wakionyesha kitambulisho chao kwenye mkusanyiko huu mmoja tu. Tunza kadi hiyo kama pesa. Huwezi kupata nyingine kwenye mkusanyiko. Vichapo vyovyote vitakavyotolewa kama zawadi au vingine kwa bei ya painia vitapatikana kwa mapainia katika chumba cha vitabu tu, kwa kuonyesha kitambulisho chao. Wale walio katika utumishi wa Betheli wanaweza kupokea maandalizi yayo hayo kwa kuonyesha kitambulisho chao cha Betheli.
UTUMISHI WA KUJITOLEA: Msaada wa kujitolea unahitajiwa ili mkusanyiko wa wilaya uendeshwe vizuri. Hata kama unaweza kufanya kazi kwa sehemu fulani tu ya mkusanyiko, utumishi wako utathaminiwa. Ikiwa unaweza kusaidia, tafadhali piga ripoti kwenye Idara ya Utumishi wa Kujitolea. Watoto wa umri ulio chini ya miaka 16 wanatakwa wafanye kazi pamoja na mzazi au mtu mwingine mzima mwenye daraka.
KADI YA SHAVU LA KOTI: Tafadhali vaa kadi ya shavu la koti iliyotayarishwa kipekee kwenye mkusanyiko na pia unaposafiri kwenda na kutoka mahali pa mkusanyiko. Mara nyingi hii inatuwezesha tutoe ushahidi mzuri tunaposafiri. Unapaswa upokee kadi ya shavu la koti kupitia kundi lako kwa sababu hazitapatikana kwenye mkusanyiko.
TAHADHARI: Bila kujali mahali unapoegesha gari lako, unapaswa ufunge gari lako wakati wote na usiache ndani kitu chochote kinachoonekana. Fungia mizigo yako yote nyuma ya gari, ikiwezekana. Pia, ujilinde dhidi ya wevi wanaovutiwa na mikusanyiko mikubwa. Hii inatia ndani kutoacha kitu chochote chenye thamani bila mtu wa kukitunza katika viti kwenye mikusanyiko. Kuongezea, imeripotiwa kwamba kuna hatari kubwa zaidi ya kuanguka juu ya ngazi wakati akina dada wanapovalia viatu vyenye visigino virefu. Tafadhali iweni waangalifu.