Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/89 uku. 2
  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Vichwa vidogo
  • JUMA LINALOANZA JUNI 5
  • JUMA LINALOANZA JUNI 12
  • JUMA LINALOANZA JUNI 19
  • JUMA LINALOANZA JUNI 26
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 6/89 uku. 2

Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

JUMA LINALOANZA JUNI 5

Wimbo 37

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyochaguliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Dokeza mambo ya kutumia katika utumishi wa shambani kutoka magazeti ya karibuni. Eleza jinsi magazeti haya yanaweza kutumiwa katika utumishi wa shambani au wakati wa kutoa ushuhuda kivivi hivi. Watie moyo wote washiriki utumishi wa shambani katika mwisho-juma huu.

Dak. 15: “Chukua Kila Fursa Kutoa Ushuhuda—Sehemu 1.” Mazungumzo ya maswali kwa majibu. Tia moyo akina ndugu watumie madokezo ambayo yametolewa na kutumia trakti vizuri.

Dak. 20: Pitia Kichwa cha Mazungumzo Kipya. Zungumzia maandiko na jinsi yanavyounga mkono habari zilizotokezwa. Pitia utangulizi na viunzi kama inavyoonyeshwa kwenye Huduma ya Ufalme Yetu ya Mei 1989 chini ya “Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi,” juma linaloanza Mei 29. Kisha wonyesho uliofanyiwa mazoezi vizuri utolewe ukizungumzia habari inayotajwa katika fungu 5 la makala “Piga Mbiu Kuhusu Amani na Usalama wa Kweli.”

Wimbo 139 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA JUNI 12

Wimbo 158

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Sifu akina ndugu kwa msaada wa kimwili kwa kundi na utie ndani shukrani za uthamini kwa michango iliyopokewa na Sosaiti. Eleza mipango ya utumishi wa shambani kwa mwisho-juma huu. Zungumzia mambo makuu katika magazeti ya karibuni yatakayotolewa.

Dak. 15: “Kuonea Shangwe Ushirika wa Kitheokrasi.” Mazungumzo ya maswali kwa majibu. Tia ndani maelezo yanayofaa kuhusu manufaa zinazopatikana kutokana na washirika wazuri.

Dak. 20: “Piga Mbiu ya Amani na Usalama wa Kweli.” Mazungumzo ya maswali kwa majibu. Tia ndani maelezo kuhusu mambo yaliyotokezwa katika ukurasa 8 wa kitabu Amani ya Kweli na mambo mengine yanayotumika katika eneo la kundi.

Wimbo 31 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA JUNI 19

Wimbo 78

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Mazungumzo ya andiko la siku na maelezo yalo.

Dak. 20: “Kutangaza Habari Njema—Kwa Kuvuta kwa Maneno ya Usadikisho.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Baada ya kuzungumzia makala, mhubiri aliyejitayarisha vizuri atoe wonyesho kuhusu jinsi jambo hili linavyoweza kufanywa, akitumia kielelezo kilicho kwenye fungu 4 au habari nyingine inayofaa.

Dak. 15: “Vuka Uje Makedonia.” Hotuba itolewe na mwangalizi wa utumishi ikitegemea makala yenye kichwa hiki iliyoonekana katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Juni 1988. Tokeza idili ya kufanyia kazi sehemu zilizo mbali na zisizofanyiwa kazi kwa ukawaida katika eneo la kundi lenyewe.

Wimbo 197 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA JUNI 26

Wimbo 210

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Dokeza habari za mazungumzo katika magazeti ya karibuni, na kutoa maonyesho mawili mafupi yaliyotayarishwa vizuri. Kazia Mnara wa Mlinzi katika wonyesho mmoja na Amkeni! katika mwingine. Tia moyo wote washiriki kazi ya magazeti Jumamosi.

Dak. 15: “Unga Mkono Ziara ya Mwangalizi wa Mzunguko.” Maswali na majibu. Wakati wa kuzungumzia fungu 2, hoji mwangalizi msimamizi kuhusiana na matayarisho yanayohitajiwa kwa ziara ya mwangalizi wa mzunguko. Kazia jinsi kundi linavyoweza kusaidia kufanya ziara iwe yenye mafanikio. Panga mapainia au wahubiri watoe maelezo mawili au matatu ya kibinafsi kuhusu jinsi wamenufaika na ziara zilizopita. Jenga idili kwa ziara itakayofuata ya mwangalizi wa mzunguko.

Dak. 20: Mambo makuu katika Kitabu cha Mwaka 1988. Hotuba iliyotayarishwa vizuri kuhusu habari ya utangulizi katika Kitabu cha Mwaka 1988. Elekezea fikira maongezeko yenye kutokeza yanayoonyeshwa katika ripoti ya ulimwenguni pote. Kadiri wakati unavyoruhusu, rejezea maono fulani yanayotolewa na kuonyesha jinsi yanavyotia moyo na kunufaisha akina ndugu wa mahali penu.

Wimbo 16 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki