Kufundisha Kwenye Mafunzo ya Biblia ya Nyumbani
1 Hiki kilikuwa ndicho kichwa cha makala katika toleo la Huduma ya Ufalme Yetu ya Aprili 1985. Miongoni mwa mambo mengine makala hiyo ilichunguza njia za Yesu za kufundisha na ikatia moyo sisi tujifunze na kutumia njia hizi ili tuwe walimu wenye matokeo kwenye mafunzo ya Biblia yetu ya nyumbani. Kwa kuwa maisha zinahusika hakika sisi tunataka kufanyia maendeleo ustadi wetu wa kufundisha.—Mt. 28:19, 20; Yoh. 17:3.
2 Kwa sababu ya uhitaji wetu wa kufanyia maendeleo ustadi wetu wa kufundisha acheni sisi tufanye pitio la mambo machache kutoka makala hiyo. Kwanza, Yesu alifundisha kwa kuuliza maswali yenye ufahamu. (Mt. 17:24-26; Luka 10:25-36) Katika mistari kutoka simulizi la Luka angalia utumizi wa maswali yakiunganishwa na kielezi. Tumizi la maswali husaidia watu wasababu na kujichunguza wenyewe kwa msaada wa yale yanayofundishwa. Ni njia ya kufikia moyo wa mwanafunzi kwa busara.
3 Pia Yesu alitumia vielezi na masomo yenye vitendo katika njia zake za kufundisha. (Mt. 4:18, 19; Luka 15:3-10; Yoh. 13:2-16) Kwa kuongezea, yeye alitoa mambo kwa njia rahisi, fupi na iliyo wazi. Itakuwa msaada kama nini kwetu sisi, na kwa mwanafunzi, ikiwa sisi tutajifunza kutumia njia ya Yesu ya kufundisha.
MADOKEZO ZAIDI
4 Wakati wa kuongoza funzo la Biblia la nyumbani ni vizuri kuwa na pitio la kufungua la somo lililotangulia. Pitio hilo liwe fupi na likazie mambo makuu tu. Njia nzuri ni kukazia maandiko makuu kutoka somo la juma lililopita. Waweza kwa kweli kumwomba mwenye nyumba asome maandiko hususa na atoe maelezo au aonyeshe matumizi ya mistari hiyo. Pitio hilo la kufungua lapasa liongoze kwenye funzo la sasa.
5 Tunataka mwanafunzi afanye nini kuhusu mambo anayojifunza? Wakolosai 3:10 hujibu swali hilo. (Tafadhali soma.) Kwa hiyo tunataka kusaidia mwanafunzi aone uhitaji wa kufanya marekebisho katika maisha yake ili yapatane na viwango vya uadilifu vya Mungu. Kazia kwamba njia ambayo mtu huishi maisha yake ndiyo ambayo kwa kweli huthibitisha anataka kuishi katika mfumo mpya wa Mungu.—Mt. 7:21.
6 Tunataka mwanafunzi afanye nini na mambo anayojifunza zaidi ya kuishi kwayo? Sehemu ya mwisho ya Luka 6:45 huandaa jibu. (Tafadhali soma.) Ndiyo, twataka mwanafunzi aongee na wengine juu ya mambo anayojifunza. Mtie moyo ashiriki kweli hizi za ajabu pamoja na watu wa ukoo wake, marafiki, na wafanya kazi wenzake. Pengine mwanafunzi aweza kuandika juu ya ile karatasi iliyo tupu kwenye upande wa mbele wa Biblia orodha ya maandiko yanayojibu maswali ambayo kwa ukawaida huzushwa na watu katika eneo lenu. Ingawa kwenye hatua hii mwanafunzi hangestahili kushiriki rasmi katika huduma akiwa mwakilishi wa kundi, kumtia moyo atumie pamoja na wale anaojuana nao mambo aliyojifunza kutamtayarisha kwa ajili ya pendeleo hili la wakati ujao.
MWALIMU—‘WAKA KWA ROHO’
7 Kwa nini kuwa ‘unawaka kwa roho’ kuna tokeo chanya katika funzo letu? (Rom. 12:11, NW) Mara nyingi maneno haya yanashirikishwa na sifa za idili na uchangamfu na hisia. Idili huonyesha usadikisho wetu sisi wenyewe na ni yenye kupasishwa. Ikiwa sisi tuna idili katika funzo roho hii itafurika na kumwingia mwanafunzi na yaelekea itamsukuma kwenye tendo. Uchangamfu na hisia hutuzuia tusiwe wenye ubaridi, tusiwe mbali, na bila upendezi tukiwa walimu. Badala ya hivyo, tunataka kuonyesha upendezi halisi wa kibinafsi kwa mwanafunzi na masilahi yake. (1 The. 2:7, 8, 17-20) Na kwa kawaida watu huitikia waonyeshwapo upendo na upendezi halisi.
8 Kutumia madokezo haya yenye kusaidia katika pitio hili kutatusaidia kuwa walimu bora kwenye mafunzo yetu ya Biblia ya nyumbani.