Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
JUMA LINALOANZA DESEMBA 4
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Tia ndani maelezo juu ya magazeti ya karibuni. Taja mambo fulani hususa yanayoweza kutumiwa katika huduma ya shambani. Tia moyo utegemezaji wa utendaji wa magazeti Jumamosi.
Dak. 20: “Je! Wewe Unathamini Thamani Yavyo?” Maswali na majibu. Toa wonyesho wa utoaji katika mafungu 5 na 6. Tia moyo wote washiriki katika kutoa toleo mwisho-juma huu.
Dak. 15: “Vijana Wanauliza . . . Naweza Kufanyaje Maendeleo Katika Kufanya Mazungumzo?” Mazungumzo pamoja na vijana wawili au watatu walio kielelezo kizuri yakitegemea Amkeni! (Kiingereza) ya Mei 22, 1989, kurasa 23-5. Mkazo unapaswa kuwekwa juu ya njia ambazo katika hizo mazungumzo yanaweza kuanzishwa na wenye umri mkubwa zaidi na watu katika huduma ya shambani. Wonyesho mfupi waweza kutolewa ukieleleza madokezo yaliyotolewa katika mambo hayo. Chaguo lingine unaloweza kutumia ni Amkeni! ya Juni 8, 1989, kurasa 19-21 kuwa msingi wa mazungumzo hayo.
Wimbo 40 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA DESEMBA 11
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyochaguliwa katika Huduma ya Ufalme Yetu. Tia ndani ripoti ya hesabu ya kundi pamoja na shukrani za Sosaiti za michango ya kundi lenu. Tangaza mipango ya utumishi wa shambani ya kundi.
Dak. 20: “Kutangaza Habari Njema—Wakati wa Sikukuu.” Maswali na majibu. Toa wonyesho wa utoaji uliodokezwa.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu au mwangalizi msimamizi azungumza mambo makuu ya “Maswali Kutoka kwa Wasomaji,” ya Julai 1, 1989, akitia moyo vijana wanaume walio vielelezo vizuri wafikilie mapendeleo makubwa zaidi ya utumishi.
Wimbo 183 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA DESEMBA 18
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Eleza mipango ya kwenu ya kutoa ushahidi.
Dak. 17: “Toa Magazeti Kwenye Kila Fursa.” Fikirio la maswali na majibu. Unapofikiria fungu la 4, toa wonyesho juu ya jinsi ya kumfikia mtu anayengojea usafiri wa umma au katika hali kama hizo. Kazia uhitaji wa kuwa chonjo kutoa magazeti kwenye kila fursa.
Dak. 18: “Kwenda Sambamba na Ongezeko la Kitheokrasi.” Mazungumzo ya maswali na majibu ya nyongeza. Wasifu kwa uchangamfu wahubiri kwa ajili ya kutegemeza kazi ya Ufalme.
Wimbo 53 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA DESEMBA 25
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Taja toleo la fasihi la Januari, na ujulishe kundi ni vitabu gani vinavyopatikana kwenu. Elekeza fikira kwenye mipango ya utumishi wa shambani ya mwisho-juma.
Dak. 15: Kuonyesha Adabu Nzuri Tunapokuwa Kwenye Jumba la Ufalme. Hotuba ikitegemea Mnara wa Mlinzi wa Juni 15, 1989, kurasa 16-17. Kazia uhitaji wa (1) kuwasili kwa wakati, (2) kukazia fikira programu, (3) kupendezwa kwa shauku ya kibinafsi na wengine.
Dak. 10: Kazi za Wakaribishaji Kwenye Mikutano ya Kundi. Mfikirio wa Sanduku la Swali na mzee na mkaribishaji mmoja au wawili. Onyesha uhitaji wa wote katika kundi kushirikiana na wakaribishaji.
Dak. 10: “Endelea Kulinda Jinsi Utembeavyo.” Tia moyo wote kundini wafanye mipango ya kuhudhuria kusanyiko la mzunguko. Zungumza juu ya kuwasaidia wazee-wazee na walio dhaifu wanaohitaji msaada katika kundi lenu. Toa madokezo yanayohusu.
Wimbo 18 na sala ya kumalizia.