Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
JUMA LINALOANZA JUNI 4
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yanayofaa katika Huduma ya Ufalme Yetu. Tia ndani mipango ya utumishi wa shambani kwa ajili ya mwisho-juma.
Dak. 20: “Uwe Stadi Katika Huduma Yako.” Mazungumzo ya makala kwa maswali na majibu. Wakati wa kufikiria mafungu 5 na 6, toa wonyesho wa matumizi ya madokezo yanayopatikana katika Mnara wa Mlinzi wa Julai 15, 1988 na Januari 15, 1985 na kitabu Kutoa Sababu. Pia, uliza wahubiri wasimulie matokeo mazuri yaliyopatikana mahali penu kwa kutumia madokezo yaliyopokewa kupitia tengenezo la Yehova.
Dak. 15: Jinsi ya Kuokoka Vita ya Mungu. Mazungumzo na wonyesho wa Kichwa cha Mazungumzo kipya kwa kutumia mahubiri yaliyodokezwa yafuatayo: “Hujambo, u mzima? Tunajitahidi kushiriki na majirani wetu maoni mazuri juu ya wakati ujao. Wengi leo wanahangaika juu ya kuokoka, na wana sababu nzuri. Upungufu wa chakula, uchafuzi, jeuri na hali nyingine nyingi zenye kutishia uhai zimesababisha wengi wahofu yaliyoko mbele. Je! mambo hayo yanakuhangaisha wewe pia? Na bado kuna tisho au hatari kubwa zaidi mbele yetu. Ni nini hiyo? Kuokoka vita ya Mungu inayokaribia. Hata Biblia inatutia moyo kwenye Sefania 3:8 tuendelee kutazamia vita hiyo. Angalia maneno haya: (Soma.) Ni lazima wewe na mimi tufanye nini ili tuokoke kutekelezwa hukumu kwa Mungu juu ya waovu? Sefania 2:2, 3 yasema ni lazima sisi tujizoeze maamuzi ya kihukumu ya Mungu na kujizoeza uadilifu. Tafadhali soma pamoja nami maneno haya mazuri. (Soma.) Kwa wale wanaoishi kwa kulingana na ushauri huo wakati ujao waweza kuwa mwangavu na wenye tumaini kama katika tamasha inayoonyeshwa kwenye kurasa 4 na 5 za kitabu hiki chenye kichwa: Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya.” Waweza kutumia habari katika mafungu haya ya ufunguzi au labda mambo fulani katika sura 2 au 4 au sura nyingine ya uchaguzi wako. Kisha kitabu chaweza kutolewa kwa mchango wa kawaida.
Wimbo 178 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA JUNI 11
Dak. 5: Matangazo ya kwenu, ripoti ya hesabu, na shukrani kwa upaji.
Dak. 10: Sanduku la Swali. Hotuba ikitolewa na mzee.
Dak. 15: “Kusaidia Vijana Wakinze Msiba.” Mfikirio wa maswali na majibu. Wasifu vijana kwa ajili ya kusoma na kutumia habari za Young People.
Dak. 15: Jinsi ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia. Hoji wahubiri wawili au watatu ambao wamefaulu kuanzisha mafunzo. Wameona ni nini chenye matokeo? Ni jinsi gani wanaendeleza kupendezwa kukiwa hai? Toa maonyesho mafupi juu ya jinsi ya kuanzisha funzo la Biblia kwenye ziara ya kwanza na wakati wa kufanya ziara ya kurudia.
Wimbo 143 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA JUNI 18
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Tia ndani mipango ya utumishi wa shambani kwa ajili ya juma lililosalia. Pia, eleza waziwazi mipango ya kueneza sehemu zisizofanyiwa kazi mara nyingi za eneo la kundi na mipango kwa ajili ya kampeni ya eneo lililo peke yake. Hakikisheni kutumia siku za soko na kuwa na fasihi za kutosha. Baadhi ya makundi yatapokea migawo hususa ya “Makedonia.” Hata hivyo, yaelekea kila kundi litaona uwezekano wa kufika ndani zaidi viungani kuliko ilivyo kawaida kwa kuwa na matayarisho mazuri ya kimbele.
Dak. 20: “Kutosheleza Uhitaji Wako wa Kiroho.” Mfikirio wa maswali na majibu wa makala. Hoji kichwa mmoja wa familia na mhubiri mseja juu ya jinsi wanavyokabiliana na wito wa kufanyiza wakati ili kutosheleza uhitaji wao wa kiroho. Watie moyo akina ndugu wachunguze mipango yao wenyewe na kufanya kazi kwa bidii kuelekea kufanya maendeleo yanayotakwa.
Dak. 15: Tafadhali pitieni madokezo yaliyotolewa kwenye ripoti ya mwisho ya mwangalizi wa mzunguko.
Wimbo 177 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA JUNI 25
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Utoaji mfupi wa magazeti ukionyesha matoleo ya karibuni yaliyopo kwa ajili ya matumizi mwisho-juma huu. Tangaza vichwa vya broshua zinazopatikana katika kundi kwa ajili ya matumizi katika utumishi wa shambani wakati wa Julai. Toa wonyesho juu ya jinsi broshua yaweza kutumiwa katika eneo lenu. Watie moyo wahubiri washiriki katika utumishi wa shambani mwisho-juma huu kwenye siku ya magazeti na wakiwa na broshua mnamo Jumapili.
Dak. 15: “Kutangaza Habari Njema—Tukiwa Familia.” Mwenezo wa maswali na majibu wa habari. Uliza swali moja au mawili tu kwenye kila fungu ili mafungu yasomwe.
Dak. 20: “Msaada Wakati Unaofaa.” Mwangalizi wa utumishi azungumza habari pamoja na wasikilizaji. Kazia manufaa za mpango wa mwangalizi wa utumishi kuzuru vikundi vya Funzo la Kitabu la Kundi. Watie moyo wote wafanye jitihada maalumu ili kushiriki katika utendaji wa juma wakati wa ziara ya mwangalizi wa utumishi.
Wimbo 214 na sala ya kumalizia.