Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/90 uku. 2
  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • JUMA LINALOANZA AGOSTI 6
  • JUMA LINALOANZA AGOSTI 13
  • JUMA LINALOANZA AGOSTI 20
  • JUMA LINALOANZA AGOSTI 27
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 8/90 uku. 2

Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

JUMA LINALOANZA AGOSTI 6

Wimbo 30

Dak. 12: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Soma Sanduku la Swali na kutoa maelezo mafupi juu ya umaana wa mavazi, mapambo, na sura inayofaa wakati wa kuwakilisha tengenezo la Yehova. Tia moyo utoaji ushahidi wa magazeti Jumamosi hii.

Dak. 18: “Uwe Mwenye Bidii Katika Kueneza Ujumbe wa Ufalme.” Mfikirio wa maswali na majibu. Baada ya kuzungumza fungu 6, toa wonyesho wa jinsi ya kutoa broshua kama ilivyodokezwa katika fungu. Tumia Kichwa cha Mazungumzo. Kazia uhitaji wa kuwa mwenye bidii katika utumishi wa shambani.

Dak. 15: “Kutumia Shule Ili Kufanyia Maendeleo Huduma ya Shambani.” Mwangalizi wa Shule azungumza na wasikilizaji Somo 19 katika Kiongozi cha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Kazia njia ambazo kwazo shule huchangia maendeleo yetu katika huduma ya shambani. Watie moyo wale waliojiandikisha katika shule wafanye vikao na hotuba kuwa zenye kutumika kwa ajili ya matumizi ya eneo lenu.

Wimbo 31 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA AGOSTI 13

Wimbo 211

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na ripoti ya hesabu. Soma shukrani zozote kutoka kwa Sosaiti kwa ajili ya michango iliyotolewa kwa kazi ya ulimwenguni pote ya Sosaiti na Hazina ya Jumba la Ufalme ya Sosaiti. Wasifu akina ndugu kwa ajili ya michango hiyo na kwa ajili ya kutegemeza kundi la kwenu. Watie moyo wote washiriki katika utendaji wa utumishi wa shambani katika mwisho-juma.

Dak. 18: “Fuliza Kuzaa Matunda Kwa Uvumilivu.” Hotuba yenye kutegemea nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Agosti. Onyesha matumizi ya kwenu ya habari, ukitia moyo wote waone hali zao za kibinafsi kwa maoni ya Yehova.

Dak. 17: “Sababu Wapaswa Kutaka Kuongoza Funzo la Biblia.” Mfikirio wa maswali na majibu. Kwa ufupi hoji mhubiri au painia ambaye amesaidia mtu fulani akafikia wakfu na ubatizo. Uliza ni uhusiano wa aina gani uliositawi baina yake na mwanafunzi (wanafunzi) na ni manufaa gani zilizopokewa kwa kuongoza mafunzo.

Wimbo 133 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA AGOSTI 20

Wimbo 29

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Pia, tia moyo ushiriki katika utendaji wa shambani wa mwisho-juma.

Dak. 20: “Je! Watoto Wako Ni Tayari Kurudi Shuleni”? Mfikirio wa maswali na majibu pamoja na wasikilizaji. Mafungu na maandiko yasomwe. Endapo kuna mambo yaliyoonwa kwenu yanayotoa kielezi mawazo yaliyotolewa, yaweza kutolewa kwa kadiri wakati unavyoruhusu.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu au hotuba juu ya “‘Simameni Imara’—Msijikwae” katika Mnara wa Mlinzi wa Aprili 15, 1990, kurasa 26-8.

Wimbo 191 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA AGOSTI 27

Wimbo 92

Dak. 7: Matangazo ya kwenu. Zungumza ripoti ya utumishi ya Mei ya Afrika Mashariki na mambo yoyote chanya ya ripoti ya kundi kwa mwezi huo. Taja umaana wa kupeleka ripoti za utumishi wa shambani mara moja. Tangaza mipango ya utumishi wa shambani.

Dak. 23: “Kutangaza Habari Njema—Kwa Kufanyiza Fursa za Kutoa Ushahidi wa Vivi Hivi.” Mwenezo wa maswali na majibu. Baada ya kufikiria fungu 3, omba wasikilizaji madokezo juu ya pindi nyingine zinazoweza kuwa wazi ili kutoa ushahidi wa vivi hivi. Taja jinsi muhula mpya wa shule unavyowapa vijana fursa ya kunena juu ya ukweli. Kufuatia fungu 6, hoji kifupi mhubiri mmoja au wawili ambao wamefanikiwa katika kutoa ushahidi wa vivi hivi. Uliza: ‘Wao wanahubiri pindi zipi? Ni kwa nini wanaona njia hii ya kuhubiri kuwa yenye mafanikio? Wao binafsi wamenufaikaje?’ Watie moyo wote waufanye mradi wao kushiriki habari njema kila siku. Malizia kwa kukazia uhitaji wa kuonyesha watu hangaiko lenye kina.

Dak. 15: Tumia kitabu Creation katika Septemba. Hotuba yenye wonyesho. Zungumza mambo ya kuongewa kutoka kitabu yanayoweza kutumiwa wakati wa kutoa kitabu Creation katika Septemba. Labda habari katika sura 16 na 17 juu ya “Ni Kwa Nini Mungu Aruhusu Mteseko?” na “Je! Unaweza Kuitumaini Biblia?” zingeweza kuvutia mwenye nyumba. Mhubiri aliyestahili sana atoe wonyesho wa toleo, akitumia maandiko kama vile Waebrania 3:4 na Ufunuo 4:11 kukanusha nadharia ya mageuzi na kujenga imani katika Mungu kuwa Mfanyizaji binadamu. Habari katika kitabu Kutoa Sababu chini ya kichwa “Uumbaji” Yaweza kutumiwa kwa kadiri wakati unavyoruhusu. Tangaza mipango ya utumishi wa shambani ya kundi, na ualike wengine washiriki.

Wimbo 129 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki