Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/90 uku. 2
  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • JUMA LINALOANZA NOVEMBA 5
  • JUMA LINALOANZA NOVEMBA 12
  • JUMA LINALOANZA NOVEMBA 19
  • JUMA LINALOANZA NOVEMBA 26
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 11/90 uku. 2

Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

JUMA LINALOANZA NOVEMBA 5

Wimbo 180

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Wakumbushe akina ndugu walete broshua Kufanya Mapenzi ya Mungu kwenye Mkutano wa Utumishi juma lijalo.

Dak. 20: “Kulipendekeza Neno la Mungu.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Wakati wa kuzungumzia mafungu 3 na 4, mhubiri mwenye kustahili atoe wonyesho wa Kichwa cha Mazungumzo kipya. Rejezea utoaji badala katika toleo la Novemba 1989 la Huduma ya Ufalme Yetu, ukurasa 2 juma linaloanza Novemba 6.

Dak. 15: Ile thamani ya New World Translation Reference Bible. Mazungumzo. Mzee azungumze pamoja na wahubiri wawili au watatu ambao wametumia vizuri kichapo hiki. Zungumzia taarifa ya Halmashauri ya New World Translation katika ukurasa wa 5. Kazia mambo makuu ya thamani ya vielezi-chini, marejezo, konkodansi mbili, na nyongeza. Kazia thamani ya kutumia kichapo hiki katika funzo la kibinafsi na katika kujitayarishia mikutano ya kundi. Ona pia Watchtower Novemba 1, 1985 kurasa 28-30.

Wimbo 46 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA NOVEMBA 12

Wimbo 6

Dak. 8: Matangazo ya kwenu na ripoti ya hesabu. Soma barua yoyote kutoka kwa Sosaiti yenye kuonyesha ukubali wa michango iliyofanywa kwa ajili ya kazi ya Sosaiti ya ulimwenguni pote. Pia, onyesha uthamini kwa ajili ya utegemezo wa kimwili katika kundi lenu. Tia moyo utendaji wa magazeti mwisho wa juma hili.

Dak. 17: “Kuelekeza Wanafunzi wa Biblia Kwenye Tengenezo la Yehova.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Wakati wa kuzungumzia fungu la 3, mhubiri anayestahili atoe wonyesho wa jinsi mwanafunzi anavyoweza kutiwa moyo ahudhurie mikutano ya kundi akitumia habari hususa kutoka broshua Kufanya Mapenzi ya Mungu, kurasa 14 na 15.

Dak. 20: “Je! Wewe Uko Tayari Kukabili Hali Ngumu ya Kitiba Yenye Kujaribu Imani?” Mazungumzo ya maswali na majibu yakiongozwa na mzee mwenye uwezo wa kunena, juu ya mafungu kuanzia mwanzo wa makala ya nyongeza kufika kichwa kidogo “Msaada Wenye Thamani Wakati wa Uhitaji.” Kazia kwamba haiwapasi kungoja mpaka jambo fulani linapotokea ndipo ujue la kufanya. Fanyeni mipango mapema kama jamaa sasa—iweni tayari!

Wimbo 36 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA NOVEMBA 19

Wimbo 101

Dak. 7: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Watie moyo wote waunge mkono utendaji wa utumishi wa shambani wakati wa mwisho-juma.

Dak. 20: “Saidia Wengine Wawe Stadi Katika Kutumia Neno la Mungu.” Mazungumzo kwa kutumia maswali na majibu. Kazia uhitaji wa kusaidia ili kuwa wenye mafanikio katika sehemu mbalimbali za huduma. Toa wonyesho wa jinsi wahubiri wanavyoweza kusaidia wanafunzi wa Biblia wanaostahili au jinsi mzazi anavyoweza kusaidia mtoto wake mdogo ajitayarishie huduma.

Dak. 18: “Je! Wewe Uko Tayari Kukabili Hali Ngumu ya Kitiba Yenye Kujaribu Imani?” Mnenaji mwenye ujuzi atoe hotuba iliyo wazi juu ya habari kuanzia kichwa kidogo “Msaada Wenye Thamani Wakati wa Uhitaji” hadi mwisho wa makala ya nyongeza, kazia manufaa za kufanya kazi pamoja na wazee wakati wa kushughulikia hali za kitiba za dharura.

Wimbo 183 na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA NOVEMBA 26

Wimbo 161

Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Kazia makala hususa kutoka magazeti ya sasa yanayoweza kutumiwa juma hili.

Dak. 10: “Kuoa Habari Njema—Kwa Mwelekeo wa Sala.” Hotuba yenye uchangamfu na yenye kuvutia. Kazia uhitaji wa kusali ili kupata mwelekezo na baraka za Mungu juu ya huduma yetu.

Dak. 15: “Twaa Fursa Utoe Ushahidi Wakati wa Desemba.” Mazungumzo ya makala kwa maswali na majibu.”

Dak. 15: Toa kitabu Kuishi Milele au Kitabu Changu katika Desemba. Hotuba na wonyesho. Wahubiri waweza kupata njia tofauti-tofauti za kuonyesha thamani ya vichapo hivi, ikitegemea aina ya eneo linalofanyiwa kazi na watu mmoja mmoja wanaowakuta. Sisi tunakabiliwa na magumu na matatizo yenye kutatanisha kila siku ya maisha, iwe ni kazini, shuleni, au nyumbani, na msaada wahitajiwa ili kutatua matatizo hayo. Twataka kusaidia watu kila mahali waelewe kwamba huu ndio wakati wa kumfafuta Mungu. Isaya 55:6, 7 laweza kutumiwa kuonyesha kwamba Mungu wa kweli aweza kupatikana. Lakini mtu lazima atafute Mungu sasa kwa kupata maarifa sahihi ya ukweli. (1 Tim. 2:3, 4) Halafu chagua sura kutoka kichapo unachotumia kusaidia mwenye nyumba athamini mambo yaliyo juu. (Katika kitabu Kuishi Milele huenda ukataka kuchagua mojapo ya sura zifuatazo: 4, 11, 19, au 29 au nyingine yoyote inayompendeza mwenye nyumba hususa unayezungumza naye.) Toa wonyesho wa jinsi wahubiri wanavyoweza kutumia maandiko hayo wanapofanya kazi nyumba kwa nyumba kwa toleo la kitabu wakati wa Desemba.

Wimbo 188 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki