Umepangia Nini Machi na Aprili?
1 Mwezi wa Machi huanza kipindi cha utendaji wa kitheokrasi ulioongezeka kwetu sisi sote. Jumamosi, Machi 30, 1991, utatia alama mwaka wa 1,958 wa Ukumbusho wa kifo cha Kristo. Tunapokuwa tukifanya mipango yetu sisi wenyewe ya kuhudhuria, twahitaji kufikiria wengine ambao huenda wakahitaji mwaliko au usaidizi wetu wa kibinafsi kwa njia fulani. Sasa si mapema mno kuanza kufanya matayarisho kwa ajili ya Ukumbusho na kufikiria kuwaalika wengine.
2 Sisi twakuonaje kuhudhuria Ukumbusho? Twapaswa kukuona kuwa pendeleo na kuwa fursa ya kuonyesha uthamini wetu kwa ajili ya dhabihu ya Kristo. Kufikia wakati huu wazee bila shaka wameangalia mambo fulani ya msingi kama vile kumpa mgawo mnenaji, kufanya mipango kwa ajili ya mifano, kuamua wakati wa mkutano, kufanya mipango mahali ambapo zaidi ya kundi moja hutumia Jumba la Ufalme, na kadhalika.
3 Mwaweza kuanza kutumia vikaratasi vya pekee vya mwaliko kwenye Ukumbusho mapema katika Machi. Kumbukeni, havipasi kutumiwa kama vikaratasi vya kawaida vya mwaliko bali vinapasa kupewa kibinafsi kwa watu wenye kupendezwa. Kwa sababu mara nyingi watu husahau tarehe na nyakati, inadokezwa kwamba tuandike vizuri au kwa taipureta anwani na mahali pa Jumba la Ufalme na wakati wa kuadhimisha Ukumbusho chini au nyuma ya kikaratasi cha mwaliko. Ikiwezekana, tumia wakati kidogo pamoja na mtu unayealika kumsaidia aelewe wazi umaana wa Ukumbusho. Wasaidieni wapya wenye kupendezwa, ikiwezekana, kwa kuandamana nao kwenye Jumba la Ufalme. Fanyeni jitihada ya pekee kuwaalika na kuwasaidia wale ambao wamejua juu ya kweli kwa miaka kadhaa lakini ambao wamejizuia kuhudhuria mikutano kwa ukawaida.—Luka 11:23; Yn. 18:37b.
4 Mara tu baada ya mwadhimisho wa Ukumbusho twaingia katika ule mwezi wenye shughuli sana wa Aprili. Hotuba ya pekee imeratibiwa Jumapili, Aprili 7. Mfululizo wa makusanyiko ya mzunguko yenye kichwa “Kaeni Mkikesha na Kubaki Mkiwa na Akili Zenu” utakuwa ukiendelea. Na kwa sababu ya wakati wa likizo ya shule na sikukuu za kilimwengu, wengi watakuwa na fursa zaidi kushiriki utumishi wa shambani. Hivyo Aprili kwa kawaida huthibitika kuwa mwezi mzuri wa kujiwekea miradi ya kibinafsi ya utendaji uliongezeka katika huduma.
5 Kundi lenu litafanya mipango gani kwa ajili ya utumishi wa shambani kwa Aprili? Je, kutakuwako mikutano zaidi kwa ajili ya utumishi wa shambani? Hakika wazee watataka kuangalia jambo hilo sasa. Je, wewe utaweza kurekebisha ratiba yako ili utumie kwa faida mipango hiyo na kufanya kazi pamoja na wengine katika utumishi wa shambani? Je, waweza kuweka kando kwa muda utendaji mwingine usio wa maana sana?
6 Ndugu na dada wengi wanapanga kufanya painia msaidizi Aprili huu. Hao watia ndani wengine wenye madaraka ya familia na hata wengine wenye kazi ya kimwili ya wakati wote. Takwa la saa 60 humaanisha wastani wa saa 2 tu kila siku kwa mwezi huo. Wazee na watumishi wa huduma wengi wanapanga mambo yao wafanye painia msaidizi katika Aprili. Je, kundi lenu litakuwa na kilele kipya cha mapainia wasaidizi mwezi huo? Ikiwa ndivyo, kundi litavuna manufaa na baraka nyingi kutoka kwa Yehova.
7 Ikiwa hali hazikuruhusu kufanya painia msaidizi wakati wa Aprili, huenda ikawezekana kuongeza utendaji wako wa utumishi wa shambani kwa kutumia wakati fulani shambani pamoja na mapainia au pamoja na wengine ambao wanajaribu pia kuongeza utendaji wao kwa mwezi huo. Waweza kuwa na hakika kwamba Yehova atabariki jitihada zako. Kwa roho yake atakupa nguvu ufikie mradi wako.—Mit. 20:18; 21:5b.
8 Tutazamapo mbele kwenye majira ya Ukumbusho yanayokuja hakika sisi tutakuwa watu wenye shughuli. Kupanga kwa uangalifu na kufanya dhabihu ni mambo yanayohitajiwa ili kuwa na ushiriki kamili kadiri iwezekanavyo katika utendaji wa kitheokrasi uliopangiwa Machi na Aprili. Kama tokeo la utendaji wetu ulioongezeka wengi zaidi na wakubali ule mwaliko “Njoo!”—Ufu. 22:17.