Mikutano Inayotusiadia Kufanya Wanafunzi
JUMA LINALOANZA DESEMBA 31
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Taja kifupi mambo ya kuzungumziwa kutoka magazeti ambayo yaweza kutumiwa kutoa ushuhuda juma hili.
Dak. 18: Pitia Kichwa cha Mazungumzo na kupanga wonyesho ukitumia mhubiri stadi akitumia utoaji uliodokezwa katika toleo la Juni 1990, la Huduma ya Ufalme Yetu, chini ya Juma Linaloanza Juni 4. Angalia mambo zaidi juu ya baraka watakazofurahia waokokaji wa vita ya Mungu kama inavyoonyeshwa kwenye Ufunuo 21:3, 4. Patanisha na toleo la vitabu vya zamani vikiwamo akibani. Vitabu vya zamani visipokuwamo akibani basi toa kitabu Kuokolewa.
Dak. 17: Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko. Mazungumzo kati ya mzee na ndugu kijana ambaye ajipata akivutiwa na ulimwengu. Mzee atumia habari katika kitabu Kutoa Sababu, kurasa 265-68, “Roho ya Ulimwengu.” Mzee afafanua roho ya ulimwengu na kueleza kwa nini kutiwa doa nayo ni jambo la kuhangaikiwa. (1 Yoh. 5:19; Ufu. 12:9) Mzee avuta ndugu huyo kwenye mazungumzo na kutoa sababu juu ya mambo haya: Kuharibiwa kwa hali yetu ya kiroho ikiwa roho ya ulimwengu inaongoza kufikiri kwetu na tamaa zetu. Roho ya ulimwengu yategemea kiburi na uasi dhidi ya Yehova. Jambo ambalo lazima lifanywe ili kujiondoa kwenye roho ya ulimwengu. Uhitaji wa kuepuka mwendo wa Hawa wa ukaidi na kukinza mwelekeo wa kuasi mamlaka. Njia ambazo katika hizo roho ya ulimwengu hujidhihirisha katika mwenendo wa watu leo. Mitego ya kupenda vitu vya kimwili; uhusiano wavyo na roho ya ulimwengu. Jinsi usemi na vitendo visivyofaa huchangia roho yenye kosa. Utofautisho unaofanywa na Biblia kati ya mtu wa kiroho na wa kimwili. Usiabudu binadamu. Mzee amalizia kwa jambo lililoonwa kuonyesha kwamba kwa kweli sisi hatukosi chochote tusipojihusisha na utendaji wa kilimwengu. Msichana mmoja mchanga mwenye umri wa miaka tisa, alilazimika kuondoka pamoja na familia yake katika nchi ya Kiafrika ambako kazi ilikuwa imepigwa marufuku wakaenda nchi nyingine ambako alitumia miaka 14 katika kambi ya wakimbizi. Miaka yake yote ya utineja ilitumiwa katika maisha yenye amani iliyohusu kujifunza Biblia na mikutano. Sasa yumo katika utumishi wa wakati wote. Ijapokuwa hakuwa na njia ya kuwa katika ulimwengu na vitumbuizo vyao, hakukosa chochote! Ndugu kijana aonyesha uthamini kwa ajili ya mazungumzo.
Wimbo 80 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA JANUARI 7
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.
Dak. 15: “Usichoke.” Mazungumzo ya mambo makuu ya makala hiyo. Omba madokezo kutoka kwa wasikilizaji wakati wa kuzungumzia fungu la 3. Mhubiri anayestahili afanye wonyesho wa toleo, akitumia dokezo katika fungu la 5. Tia kundi moyo waendelee kuwa na shughuli nyingi shambani na wasichoke au kuvunjwa moyo na ubaridi au upinzani wanaokutana nao.
Dak. 20: Twaweza Kuendeleaje Kuwa Wenye Nguvu? Mfululizo wa mahoji kukazia uhitaji wa kuendelea kuwa wenye nguvu na kutochoka. (1) Hoji wawili au watatu ambao wamekuwa wakitumikia kwa miaka kadhaa na ni vielelezo vizuri. Ni mikazo gani ya kuacha kuhubiri wamepata na wakaishinda? Wamesaidiwa na nini wazidi kuendelea na wasichoke? (Waweza kutaja sala, kuhudhuria mikutano kwa ukawaida, funzo la kibinafsi, kitia-moyo kutoka kwa wengine, na kadhalika.) Walifanya nini wajilinde wasipunguze mwendo au kuacha kabisa? (Waweza kutaja umaana wa ushirika wa ukawaida mikutanoni, kuendeleza funzo la kibinafsi, uthamini wa uhusiano pamoja na Yehova, na kadhalika.) Wamedumishaje usawa wa kiroho? (Waweza kutaja msaada wa wazee au wengine, kutanguliza masilahi ya kiroho maishani, sala kwa Yehova, na kadhalika.) (2) Hoji baadhi ya watoto ambao ni wahubiri wa kawaida na ni vielelezo vizuri. Wamesaidiwa na nini wawe wa kawaida katika utumishi? Wazazi wamewasaidiaje? Je, wahubiri wengine huwatia moyo na kuwasaidia katika utumishi wa shambani? Miradi yao ni nini katika utumishi wa Yehova? Malizia kwa pitio fupi la mambo ambayo yamekaziwa katika mahoji.
Wimbo 10 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA JANUARI 14
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu na shukrani kwa upaji. Pongeza kundi kwa kutegemeza kazi ya ulimwenguni pote. Vuta fikira kwenye habari katika “Uwe Tayari Kwa Kampeni ya Uandikishaji wa Mnara wa Mlinzi,” na uwatie moyo wahubiri waagize magazeti ya ziada wanayohitaji. Wahubiri watataka kuja na Watch Tower Publications Index yao ya karibuni zaidi kwenye Mkutano wa Utumishi juma lijalo.
Dak. 23: Hati ya Kitiba na Kadi ya utambulisho. Mwandishi aone kwamba kadi zimegawanywa na azungumzie mafungu 1, 2, 4-7, 9, na 10 ya barua ya Sosaiti ya Januari 1, 1991, kuhusu jambo hili. Sababu pamoja na wasikilizaji kwa nini maagizo hayo yapasa kufuatwa kwa uangalifu ili kadi zituhami kwa mafanikio zaidi iwezekanavyo. Wazee waweza kufanya kama walivyofanya mwaka jana. Msikawie kujaza kadi na kuhakikisha kwamba zimetiwa sahihi ifaavyo.
Dak. 12: Kazi za Mtumishi wa Vitabu. Mwangalizi wa utumishi ahoji mtumishi wa vitabu, akipitia madaraka yanayohusika. Ingekuwa vizuri kukazia mahitaji ya kwenu ambayo yangesaidia kufanyia maendeleo ugawanyaji wa vitabu baada ya mikutano.
Wimbo 108 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA JANUARI 21
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Tia ndani mipango ya utumishi ya mwisho wa juma. Kila mtu apaswa kuja na nakala ya trakti Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani kwa ajili ya Mkutano wa Utumishi juma lijalo.
Dak. 15: “Kutimiza Huduma Yetu ya Ufalme kwa Msaada wa Index.” Hotuba ikitolewa na mzee pamoja na ushirika wa wasikilizaji. Toa wonyesho wa jinsi mzee na mtumishi wa huduma wanavyoweza kutumia Index kujitayarishia ziara ya uchungaji. Zungumzia jinsi ya kufundisha wahubiri watumie Index watajirishe usomaji Biblia wa kila juma.
Dak. 20: “Kutangaza Habari Njema—Kwa Trakti na Vikaratasi vya Mwaliko.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Panga maandiko yasomwe. Baada ya kuzungumzia fungu la 7, painia au mhubiri stadi atoe wonyesho akianza funzo katika ziara ya kurudia akitumia trakti Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani. Watie moyo wahubiri watumie njia hii katika ziara za kurudia, hasa wakati imekuwa vigumu kuwapata wenye nyumba nyumbani katika ziara ya kwanza. Waalike wahubiri waliojitayarisha watoe maelezo juu ya mafanikio waliyopata wakitumia njia hii.
Wimbo 203 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA JANUARI 28
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Dokeza mambo ya kuzungumzia kutoka magazeti yanayoweza kutumiwa mwisho wa juma hili.
Dak. 15: “Umepangia Nini Machi na Aprili?” Mazungumzo ya maswali na majibu. Andaa mambo zaidi yoyote yanayopatikana tayari kuhusu mwadhimisho wa Ukumbusho.
Dak. 20: Je, Wewe Waweza Kufanya Utumishi wa Painia Msaidizi katika Machi, Aprili na/au Mei? Mazungumzo yenye uchangamfu yakiongozwa na ndugu mwenye ujuzi akiwa painia wa kawaida au painia msaidizi. Hoji wahubiri kadhaa waliofanya painia msaidizi wakati uliopita. Ni marekebisho gani waliyofanya ili wafikie mradi wao? Kazia mipango yenye mafaa waliyofanya. Majira ya Ukumbusho yakiwa yanakaribia, watie moyo wahubiri wanaopendezwa kupainia wazungumzie mipango yao pamoja na mzee. Kwa kuwa na mwelekeo chanya sasa, wengi wataonea shangwe utumishi huo. Kwa wengine hilo laweza kuwa mwanzo wa utumishi wa painia wa kawaida. (kmSW 2/90 uku. 3) Fomu za maombi zaweza kupatikana kutoka kwa mwangalizi msimamizi au mwandishi.
Wimbo 151 na sala ya kumalizia.