Usichoke
1 Kitabu cha Mwaka 1991 kinasimulia mpanuko wenye kusisimua unaotukia duniani pote. Kuna vilele vipya vya wahubiri katika nchi moja baada ya nyingine.
2 Lakini ikoje katika eneo lenu? Je, wewe unakutana na kutojali au hata upinzani? Je, watu wana ubaridi kuelekea ujumbe wa Ufalme? Je, ni watu wachache wanaokuwa nyumbani? Je, ni wachache wanaoitikia kwa kupendezwa? Ikiwa ndivyo, waweza kutiwa moyo na shauri la Paulo kwenye Wagalatia 6:9: “Tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia [tusipochoka, NW].” Hakika kutenda mema kwatia ndani kuhubiri habari njema za Ufalme mlango kwa mlango inapowezekana. Hata hali ziweje, ni lazima sisi tuendelee kuhubiri kwa uharaka mpaka Yehova aseme kazi imekwisha. (Isa. 6:8) Hata katika maeneo magumu, wenye mfano wa kondoo wangali wanapatikana.
3 Sisi twaweza kufanya nini ili tusichoke katika huduma? Kubadili njia yetu au matangulizi yetu kwaweza kusaidia. Madokezo bora kabisa yanapatikana katika kitabu Kutoa Sababu. Je, wewe umeyajaribu? Njia fupi sana lakini ya moja kwa moja huenda ikanasa usikivu wa wenye nyumba wengi. Acha watu wajue kwamba wewe upo pale kwa sababu wewe unapendezwa kibinafsi nao na hali njema yao.
TOA KITABU KUOKOLEWA
4 Wakati wa Januari twaweza kuonyesha twahangaikia wengine kwa kuwatolea kitabu Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya. Kitabu Kuokolewa ni kifaa bora kabisa cha kusaidia wengine wajifunze jinsi wanavyoweza kuokoka vita ya Mungu inayokuja wakafurahie baraka za mfumo mpya wa mambo wenye uadilifu.
5 Kila sura ya kitabu hiki ina mambo bora kabisa ya kuzungumzia. Huenda ukaona sura ya 1 na picha kwenye kurasa 4 na 5 kuwa zenye kusaidia katika utoaji wako. Ni nani asingetaka kuishi katika hali za Paradiso zinazoonyeshwa humo? Sentensi tatu za kwanza za sura ya 1 huelekeza fikira kwenye wakati ujao ambao sisi sote tungependa kufurahia. Bila shaka, waweza kupata mambo mengine yenye kufaa utoaji wako, kama vile katika sura ya 4 na kielezi kwenye ukurasa wa 33 kinachoonyesha kusudi la Mungu la awali kwa ainabinadamu. Fungu la 6 hadi la 8 kwenye kurasa 32 na 34 hupatana vizuri na Kichwa cha Mazungumzo chetu cha sasa.
6 Hakika sisi twaweza kutiwa moyo na kutiwa nguvu kibinafsi kwa kushiriki katika kazi ya kuhubiri Ufalme juma kwa juma. Kwa kuongezea, hali yetu ya kiroho yaweza kuendelezwa ikiwa juu kwa kujifunza daima Neno la Mungu na kushiriki kwa ukawaida katika mikutano ya kundi.—Ebr. 10:23-25.
WATIE MOYO WENGINE WAENDELEE KUKAA WAKIWA WENYE NGUVU
7 Waweza kujisaidia na kutia wengine moyo kwa kufanya kazi pamoja nao katika huduma ya shambani. (Gal. 6:10) Kwa nini usiwaulize mapainia na wazee kama unaweza kufanya kazi nao? Pia, wale wasio wa kawaida au labda wasiotenda wangetiwa moyo kwa kupendezwa kwako na hali njema yao ya kiroho.
8 Sisi sote twahitaji kuvumilia katika utumishi wa Yehova na tusichoke katika hizi siku ngumu za mwisho. Uvumilivu kama huo utatuwezesha kudumisha bidii yetu ya Kikristo ujapokuwa ugumu au ubaridi upande wa wengine. (Ebr. 10:36-39) Mwombe Yehova akupe nguvu. (Isa. 40:29-31) Mwombe akusaidie uvumilie, na uendeleze mwelekeo chanya wa akilini. Kumbuka, sisi tunafanya kazi ya Mungu. Yeye huona tufanyayo katika utumishi wake, naye hasahau. (Ebr. 6:10) Kwa hiyo acheni sisi tusichoke! Badala ya hivyo, acheni sisi ‘tuzidi sana kutenda kazi ya Bwana,’ tukimtegemea Yehova atutie nguvu kwa ajili ya ‘kazi yake njema.’—1 Kor. 15:58; Gal. 6:9.