Wimbo 80
Kutembea Katika Jina la Mungu Wetu
(Mika 4:5)
1. E Mwenye Enzi, Yehova Mungu,
Kwa upendo wako twakusifu.
Wasamehe, watuonya njia.
Bwana, tutadumu hudumani.
2. Adui wengi. Wao ni jeshi.
Wajivunia miungu yao.
Ni ya uwongo; twasema kweli
Twaenda katika jina lake.
3. Bethlehemu katoka ’Tawala,
Kwa Muchunga anayeokoa.
Sasa “mabaki” wamerudishwa,
Wakweza ibada yako Bwana.
4. Mwabudu Yehova. ’Tumikie.
Na ujifunze, mapenzi yake.
Panga, mikuki ni ya amani.
Kwa furaha ’tamutumikia.