Kuanzisha Mazungumzo Unaporudi
1 Ili kuwa na mafanikio katika kuanzisha mazungumzo na mtu ambaye ameonyesha kupendezwa katika ziara ya kwanza, jaribu kuendeleza yale mliyosema wakati uliopita. Kusudi ni kusaidia mtu huyo aelewe thamani ya mawazo na kichapo alichoachiwa mwanzoni.
2 Chukua wakati kutayarisha kufanya ziara hiyo ya kurudia. Chagua maelezo yatakayoamsha upendezi ambayo yamo katika kichapo unachoonyesha. Tumia utambuzi kuona ni kiasi gani cha habari mtakachopitia na muda utakaotumia. Mara nyingi mazungumzo mafupi ya jambo moja au mawili ndio bora zaidi isipokuwa kama upendezi usio wa kawaida unaonyeshwa. Fikiria vichwa vifuatavyo:
3 Ni hali gani za wakati ujao tunazoweza kutarajia zifanyizwe duniani ikiwa itakuwa makao ya mwanadamu ya kudumu? Msingi wa mazungumzo hayo ni Isaya 11:6-9 na 65:25, kama ilivyoelezwa na kuonyeshwa katika kitabu Usalama Ulimwenguni Pote katika kurasa 172-5.
Mazungumzo yaweza kuanzishwa kwa kusema:
◼ “Nilipozuru wakati uliopita, tulizungumza jinsi Mungu amekusudia kwamba dunia idumu milele. Lakini nilikuachia swali la kufikiria: “Ni hali gani zitakazokuwako wakati huo? Nimefurahi kurudi na kushiriki kifupi jibu la Biblia pamoja nawe.”
4 Yale tunayopaswa kufanya ili kufurahia maisha chini ya Ufalme wa Mungu. Kichwa hicho chaweza kukuzwa kwa kutumia Yohana 17:3 na Yeremia 31:34, kama inavyoelezwa katika kitabu Usalama Ulimwenguni Pote kurasa 119-20.
Ili kuanza, ungeweza kusema:
◼ “Nilifurahia mazungumzo pamoja nawe kuhusu ahadi ya Mungu ya kukomesha uovu. [Mwombe mtu huyo alete kitabu chake Usalama Ulimwenguni Pote.] Swali ambalo sisi sote twapaswa kulifikiria ni, Tunaweza kufanya nini tuwepo ili kufaidika na badiliko hilo? Ona yale Yesu alisema kwenye Yohana 17:3, kama inavyonukuliwa katika kitabu chako kwenye ukurasa 120.”
5 Ni mahitaji gani yatakayotoshelezwa katika dunia-paradiso? Unaweza kutumia ama Zaburi 65:9-13 na 72:16 ama Isaya 11:6-9 na 65:25. Maelezo yanayofaa yamo katika kitabu Usalama Ulimwenguni Pote kurasa 174-5.
Maneno yako ya kufungua yaweza kuwa:
◼ “Nilipokuwa hapa wakati uliopita [sema siku], tuliona ahadi ya Mungu kupitia Mwana wake ya kufufua wapendwa waliokufa kwenye Dunia-Paradiso. Ni nini baadhi ya mibaraka itakayofurahiwa wakati huo? Kitabu chako kinataja Kimaandiko baadhi yayo.” Ukitegemea marejezo yaliyo juu, soma andiko moja au mawili yaliyotajwa kutoka kwa Biblia na maelezo kutoka kwa kitabu, labda mafungu 7-10.
6 Watu wengi wameonyesha kupendezwa na ujumbe wa Ufalme tunaohubiri. Mara nyingi, sisi hutambua upendezi unaofaa wanapochukua vichapo vyetu. Nyakati nyingine, sisi huona uthamini wao katika mazungumzo yetu ya kwanza ya Kimaandiko. Kwa hiyo, fanya ziara za kurudia kwa wote wanaoonyesha kupendezwa, na ujaribu kuwafunza kweli.—Mt. 10:11; 28:19, 20; Yn. 21:17; Ufu. 22:17.