Matangazo
◼ Toleo la fasihi kwa Aprili na Mei: Uandikishaji wa Mnara wa Mlinzi. Maandikisho yanaweza kupatikana kwa mwaka mmoja au miezi sita. Hakuna mipango yoyote kwa maandikisho ya miezi mitatu ya magazeti hayo.
Juni: Mankind’s Search for God. Katika Kiswahili tumia kitabu chochote cha kurasa 192 kwa mchango wa kawaida. Julai: Yoyote ya broshua zifuatazo: Furahia Milele Maisha Duniani!, “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya,” Je! Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, au Serikali Itakayoleta Paradiso. ANGALIA: Makundi ambayo hayajaagiza vifaa vya kampeni vilivyotajwa juu yapaswa yafanye hivyo kwenye Fomu ya Agizo la Vitabu (S-14-SW) ya mwezi utakaofuata.
◼ Mwangalizi msimamizi anapaswa ahakikishe kwamba mipango yote kwa ajili ya mwadhimisho wa Ukumbusho inaenda vizuri. Hiyo inatia ndani migawo ya wakaribishaji na wenye kupeana mifano pamoja na uandalizi wa mkate usiotiwa chachu, divai nyekundu, glasi, na kadhalika.—Ona orodha ya mambo makuu katika toleo la Machi la Huduma ya Ufalme Yetu.
◼ Wakaribishaji kwenye Ukumbusho wapaswa wawe macho kuwasalimu wapya na wahudhuriaji wasio wa kawaida. Kwa wale ambao labda wangependa mtu fulani aongoze funzo la Biblia nyumbani pamoja nao, jitahidini kupata majina yao na sehemu wanayoishi. Habari hiyo yapaswa ipewe mwangalizi wa utumishi.
◼ Katika nakala yako ya kitabu cha nyimbo, rekebisha nyimbo zifuatazo:
Wimbo 143, ubeti wa tatu mstari wa mwisho, badala ya mstari kusema; Mu-ngu ndi-ye ngu-vu ye-tu (ye-tu); badilisha uwe; Mu-ngu ni ngu-vu ye-tu (ni ye-tu);
Wimbo 180, ubeti wa mwisho kwenye mstari wa mwisho, badala ya mstari kusema; Hu-pa tu-ma-i-i-ni ku-bwa sa-na; badilisha uwe; Hu-pa tu-ma-i-ni ku-bwa za-i-di;