Kuunganisha Utangulizi Wetu na Fasihi
1 Unapotayarisha utoaji wako mwezi huu, huenda kwanza ukafikiria matatizo makubwa yanayokabili watu katika eneo lenu halafu uteue vifungu vya maneno kutoka kwa magazeti ya karibuni au kutoka kwa broshua vinavyotaja utatuzi wa Kimaandiko, wenye kutumika.
2 Katika ujirani fulani, huenda watu wakahangaishwa na ukosefu mkubwa wa kazi na gharama ya juu ya maisha. Ikiwa kuna hali hiyo, unaweza kutaja tatizo hilo kihususa katika utangulizi wako.
Huenda ukasema:
◼ “Tumekuwa tukizungumza na majirani wetu kuhusu yale yanayoweza kufanywa ili kuhakikisha kwamba kuna kazi na makao kwa kila mtu. Je! unasadiki kwamba ni jambo la akili kutazamia kwamba binadamu watatimiza hilo? [Ruhusu itikio la mwenye nyumba.] Kuna mtu fulani anayejua jinsi ya kutatua matatizo hayo; ona ahadi yake hakika kwenye Isaya 65:21-23. [Soma.] Muumba wetu alifanya ahadi hiyo iandikwe ili tutiwe moyo, na sisi sote tunahitaji hiyo katika nyakati hizi ngumu, sivyo?”—rs-SW, kur. 11.
3 Kufikia hapo katika utoaji wako, unaweza kuunganisha habari iliyo katika magazeti ya karibuni au katika broshua. Ikiwa unatoa broshua “Tazama!” kwa nini usionyeshe jinsi wazo la makao na kazi kwa kila mtu limeonyeshwa katika upande wa mbele na nyuma ya jalada la broshua hiyo. Unaweza kuifungua ili mwenye nyumba aweze kuona picha nzima wakati uleule.
4 Katika maeneo ambamo wenye nyumba wana mambo mbalimbali yanayowahangaisha, utangulizi wenye kubadilikana utakuwa wenye msaada. Huenda ukataka kujaribu utangulizi wa pili ulioorodheshwa katika kitabu Kutoa Sababu chini ya “Ufalme.”
Ungeweza kusema:
◼ “Yesu alitufunza tusali Ufalme wa Mungu uje na mapenzi Yake yafanywe duniani kama mbinguni. Je! unafikiri kwamba ikiwa mapenzi ya Mungu yatafanywa hapa duniani, dunia kwa kweli itakuwa paradiso?” Baada ya itikio la mwenye nyumba, toa utangulizi wa Ufunuo 21:3-5 na usome.
Halafu, ikiwa unatoa broshua Serikali, soma sehemu ulizoteua za fungu la utangulizi katika ukurasa wa 3. Angalia maneno: “Kwa kutumia Ufalme huo, karibuni Mungu atamaliza vita, njaa, magonjwa na uhalifu.” Mwulize mwenye nyumba ni tatizo gani kati ya hayo analoona kuwa kubwa zaidi.
Ikiwa unatoa “Mnara wa Mlinzi” la Mei 15, huenda ukasema:
◼ “Watu wengi wangependa kusadiki kwamba ahadi hiyo itatimizwa, lakini hawana hakika kama Biblia ni mwongozo wenye kutegemeka. Nina hakika utapata makala hii, ‘Sababu kwa Nini Biblia Ni Zawadi Yenye Pumzi Kutoka kwa Mungu,’ kuwa yenye kuimarisha imani.”
5 Vijana pia wanaweza kutoa ujumbe wa Ufalme kwa mafanikio, hata kwa watu wakubwa.
Katika kutoa utangulizi wa Isaya 65:21-23, huenda wahubiri vijana wakasema:
◼ “Ninajua kwamba wewe ukiwa mtu mkubwa una maarifa mengi maishani kuliko mimi, lakini andiko hili linatufariji sisi sote.”
6 Hakikisha kuweka rekodi sahihi ya chochote ulichoangusha, kutia ndani broshua au magazeti hususa uliyoangusha. Utahitaji habari hiyo unaporudi kusitawisha kupendezwa.