Matangazo
◼ Toleo la fasihi kwa Septemba: Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? Mahali ambapo kichapo hicho hakipatikani katika lugha inayotumiwa katika eneo au kundi, tafadhali tumia kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Oktoba: Uandikishaji wa Amkeni! au Mnara wa Mlinzi au magazeti yote mawili. Novemba: Biblia New World Translation pamoja na kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. ANGALIA: Makundi ambayo bado hayajaagiza vifaa vya kampeni vilivyotajwa juu yapaswa yafanye hivyo kwenye Fomu ya Agizo la Vitabu (S-14-SW) ya mwezi utakaofuata.
◼ Mwangalizi msimamizi au mtu aliyewekwa naye apaswa akague hesabu ya kundi mnamo Septemba 1 au upesi iwezekanavyo baada ya hapo. Tangazia kundi, hilo linapokamilishwa.
◼ Wahubiri wanaopanga kufanya upainia msaidizi katika Oktoba wapaswa watoe maombi yao mapema. Hilo litaruhusu wazee kufanya mipango inayohitajiwa kwa ajili ya fasihi na eneo.
◼ Wazee wanakumbushwa kutekeleza shauri lililotolewa katika kurasa 21-3 za Mnara wa Mlinzi la Aprili 15, 1991, kuhusu mtu yeyote aliyetengwa au akajitenga na ushirika ambaye huenda ana mwelekeo wa kutaka kurudishwa.
◼ Katika kurasa 103-4 za kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu, mwelekezo umetolewa juu ya yale yanayoweza kutiwa ndani katika kuripoti saa za utumishi wa shambani. Wengine wamejiuliza kama mhubiri anayetafsiri hotuba ya watu wote inayotolewa na msemaji anaweza kuhesabu wakati huo. Ndiyo, wote wawili msemaji na mtafsiri wanaweza kutia wakati uliotumiwa katika ripoti yao ya utumishi wa shambani.
◼ Orodha ya Bei mpya imetayarishwa na nakala nne zinapelekwa kwa makundi katika sehemu ambazo bei zimebadilishwa. Nakala hizo zapaswa zigawanywe kwa mwandishi na ndugu wanaoshughulikia fasihi, magazeti, na hesabu.
◼ Sahihisho: Katika ukurasa 37 wa kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, kwenye utangulizi badilisha maneno ya mwisho yawe Agano la Kale badala ya Agano Jipya.