Je! Kupendezwa Kwaweza Kuamshwa Tena?
1 “Wenye furaha ni wale wanaoona uhitaji wao wa kiroho.” (Mt. 5:3, NW) Maneno hayo ya Yesu katika Mahubiri ya Mlimani yamejaa maana. Wengi wa ainabinadamu hawajui kwamba wanahitaji mambo ya kiroho ili kufanya maisha zao ziwe zenye furaha na kusudi. Kuna wale walioona hivyo mahitaji ya kiroho hapo mbeleni lakini wakapoteza hali hiyo. Jambo fulani liliwafanya wawe baridi kuhusiana na mambo ya kiroho. Waliyaacha yale yaliyo ya manufaa kwao kikweli. Swali ni, Je! kupendezwa kwa watu hao kwaweza kuamshwa tena? Kwa furaha, inawezekana kwa wengine.
2 Huenda ukajua mtu aliyejifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova miaka iliyopita, labda hata alipokuwa mtoto, lakini hakuendelea kushirikiana na watu wa Mungu. Hata hivyo, huenda baadhi ya mafundisho ya Biblia na kanuni za uadilifu zikawa zilikazwa sana akilini mwa mtu huyo na bado anayakumbuka. Hali za ulimwengu zinapozidi kuwa mbaya na hali za maisha zinapobadilika, huenda mtu huyo akakumbuka mambo aliyojifunza hapo mbeleni na akaweza kumgeukia Mungu akiwa na utayari wa kujifunza maarifa zaidi ya Biblia. Kuwazuru watu kama hao kwa kusudi la kuanzisha upya funzo la Biblia kwaweza kuthibitika kuwa kwenye kuthawabisha sana.
3 Kwa kweli jitihada zapaswa kufanywa mara kwa mara kuwazuru wale waliohudhuria mwadhimisho wa Ukumbusho. Acha wajue kwamba unapendezwa nao kikweli na hali njema yao ya kiroho, na uwaulize ikiwa unaweza kujifunza Biblia pamoja nao. Jitihada za pekee zapaswa kufanywa kuwasaidia wale watakaohudhuria “Wachukuaji Nuru” Mkusanyiko wa Wilaya unaokuja. Katika visa fulani, huenda kukawa na manufaa kwa mhubiri mwingine kumzuru mtu ambaye funzo lake lilikatizwa kwa sababu ya kukosa kufanya maendeleo.
4 Bila shaka, watu tunaojifunza nao wanatazamiwa kuchukua ibada ya Yehova kwa uzito na waonyeshe kiasi fulani cha bidii-nyendelevu katika funzo lao la Biblia. Lakini kwa upande wetu, tunataka kuhakikisha kwamba tumetia jitihada za kutosha ili kuwasaidia na kwamba tunaweza kuhisi kuelekea wengine kama vile mtume Paulo alivyohisi aliposema, “Mimi sina hatia kwa damu ya mtu awaye yote.”—Mdo. 20:26.