Kusaidia Wengine Wathamini Mambo ya Kiroho
1 Ukumbusho unathibitika kuwa pindi yenye kuchangamsha moyo jinsi gani! Kila mwaka tunakumbushwa thamani ya dhabihu ya Kristo Yesu kwa ajili ya aina ya binadamu yote. Sherehe hii ya kipekee sana inatupa nafasi ya kuwasaidia wapya wathamini mambo ya kiroho ambayo Mungu ametutolea kupitia kwa Mwana wake mpendwa kwa ukamili zaidi. (Marko 9:7) Tunaweza kuwasaidiaje wale wanaohudhuria Ukumbusho washirikiane na kundi kwa ukawaida?
2 Bila shaka, wengi wa wale wanaohudhuria Ukumbusho, hata kwa mara ya kwanza, wanatambua njaa ya kiroho ndani yao wenyewe ambayo inahitaji kutoshelezwa. (Mt. 5:3) Tunaweza kufanya nini ili tuwachochee watafute njia za kutosheleza uhitaji huu?
3 Jambo moja lingekuwa kuwatembelea mara moja iwezekanavyo. Waonyeshe kupendezwa kwa kibinafsi na ujitolee kuwasaidia wafanye maendeleo ya kiroho. Wengi wanaohudhuria Ukumbusho hawana funzo la Biblia la kibinafsi. Wasaidie wafahamu kwamba ili wanufaike kikamili kutokana na dhabihu ya Kristo Yesu na wapate upendeleo wa Yehova, funzo la kawaida linahitajiwa. Jitahidi kufanya mipango ya programu ya ulishaji huo wa kiroho kulingana na nafasi yao.
4 Ukiwatembelea juma linalofuata lile la Ukumbusho na ujitahidi kupangia funzo la Biblia, wakati ule ule unaweza kuwapa mwaliko mchangamfu wa kuhudhuria hotuba ya pekee itakayokuwa Aprili 10, “Kwa Nini Kuishi Kulingana na Viwango vya Biblia?” Jitolee uambatane nao kwenye Jumba la Ufalme, ikiwa inahitajiwa wape nauli ya kusafiria.
WAALIKE WATOE USHUHUDA
5 Namna gani wale ambao tayari wanajifunza na labda wanahudhuria mikutano kwa ukawaida? Ni maendeleo gani zaidi wanayohitaji kufanya? Umewadokezea wajaribu kuwatolea ushuhuda marafiki zao, watu wa ukoo, wafanya kazi wenzi, na watu wengine wanaokutana nao ki-vivi-hivi? Hilo litawasaidia wafanye maendeleo kiroho. Watakuwa wakionyesha uthamini wao kwa dhabihu ya Yesu na kweli ambazo wanajifunza.
6 Huenda mwanafunzi wa Biblia akasita-sita kuongea na wengine, akiwaza kwamba huenda wasisikilize ukweli. Huenda akahitaji kujifunza kwamba kila mtu mmoja mmoja ni wa maana sana kwa Mungu, anayeona moyo na anayejua wakati mtu anapokuwa tayari kukubali habari njema. Msaidie mwanafunzi wako ang’amue kwamba ni mapenzi ya Mungu “namna zote za watu waokolewe na kuja kwenye maarifa sahihi ya ukweli.” (1 Tim. 2:4, NW; Mdo. 17:26, 27) Mwonyeshe kwamba Yesu Kristo alitumwa na Mungu ‘atoe nafsi yake iwe fidia [dhabihu, NW] ya wengi.’ (Mt. 20:28) Ikiwa mwanafunzi wako anaweza kusaidiwa athamini jambo hilo, ataona ni kwa sababu gani apaswa kujaribu kuzungumza juu ya ukweli kwa kila mtu wakati wo wote anapokuwa na fursa. Usadikisho wake wa kibinafsi utatiwa nguvu, naye atapata shangwe ya kutoa hazina yenye thamani zaidi ambayo yeye anayo.—Gal. 6:6; Mdo. 20:35.
7 Wale wanaostahili wapaswa waalikwe ili washiriki katika huduma ya shambani wakati wa mwezi wa Aprili. (Mt. 9:37, 38; omSW kur. 97-9) Yehova anawapendelea wale ambao wana mbetuko wa kumtumikia hata ikiwa uwezo wao ni wenye hadi. Kweli kweli, sisi sote tumependelewa sana kushirika kazi ya kuokoa uhai kwa kuiga Mwokozi wetu, Yesu Kristo. (Mt. 28:19, 20) Kwa kutimiza utume wa kuhubiri, sisi sote tutakuwa tukitii shauri lililotolewa na mtume Paulo: “Kufanya kazi pamoja na yeye, sisi pia twasihi ninyi msikubali fadhili isiyostahiliwa ya Mungu na kukosa kusudi layo.”—2 Kor. 6:1, NW.
8 Hatujui ni wangapi ambao bado watakuja kuthamini pendeleo la kumtumikia Yehova. Lakini tunahakikishiwa kwamba kwa kuendelea kuwasaidia wengine wathamini mambo ya kiroho tutapokea baraka za ajabu, na ndivyo na wao.—2 Kor. 6:2.