Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/88 uku. 2
  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Vichwa vidogo
  • JUMA LINALOANZA APRILI 4
  • JUMA LINALOANZA APRILI 11
  • JUMA LINALOANZA APRILI 18
  • JUMA LINALOANZA APRILI 25
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 4/88 uku. 2

Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

JUMA LINALOANZA APRILI 4

Wimbo 7 (27)

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Toa muhtasari wa habari zilizo chini ya “Mipango Yako Ni Ipi kwa Ajili ya Aprili?” Kungali kuna wakati wa kupeleka ombi la utumishi wa painia msaidizi wakati wa Aprili. Tia moyo kutoa ushuhuda jioni. Pendekeza kwamba jitihada ya pekee ifanywe Jumamosi, Aprili 9, kuwaalika watu kwenye hotuba ya pekee “Kwa Nini Kuishi Kulingana na Viwango vya Biblia?” Wakati ukiruhusu, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu yale ambayo wao wanapanga kusema wakati wa kualika marafiki, majirani, na watu wa ukoo kwenye hotuba. Dokeza kutumia T-13, Sababu Kwa Nini Wewe Unaweza Kuitumaini Biblia.

Dak. 18: “Kutokosa Kusudi la Huduma Yetu ya Shambani.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Toa maonyesho mafupi mawili au matatu kwa kutumia habari kwenye kurasa 13-15 za kitabu Reasoning chini ya “Siku za Mwisho,” “Wakati Watu Wengi Wanaposema: ‘Mimi nina dini yangu mwenyewe,’” na “Wakati Watu Wengi Wanaposema: ‘Mimi Nina Shughuli.’” Tia moyo ushirika wenye idili kwa kutoa uandikishaji.

Dak. 15: “Kusaidia Wengine Wathamini Mambo ya Kiroho.” Maswali na majibu. Baada ya fungu la 7, mhubiri mwenye ujuzi atoe wonyesho kuhusu jinsi ya kualika mwanafunzi wa Biblia ashiriki katika huduma ya shambani.

Wimbo 51 (92) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA APRILI 11

Wimbo 72 (35)

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yanayofaa katika Huduma ya Ufalme Yetu. Ripoti ya hesabu. Tia shukrani za Sosaiti kwa kupokea michango iliyopelekwa na sifu akina ndugu kwa kuunga mkono kundi kimwili. Toa maonyesho mawili ya sekunde 30 mpaka 60 kuhusu utoaji wa magazeti ya karibuni.

Dak: 15: “Sababu kwa Nini Wakristo Wapaswa Kuwa Wafuataji Haki. Hotuba ikitegemea makala katika Mnara wa Mlinzi wa Februari 15, 1988.

Dak. 20: “Kuweka Kando Wakati kwa Ajili ya Maandalizi ya Kitheokrasi.” Maswali na majibu. Pata maelezo kutoka kwa wasikilizaji juu ya jinsi watu wapya wenye kupendezwa wanaweza kusaidiwa wajitayarishe kikamili kwa ajili ya funzo lao la Biblia kila juma. Tia ndani maelezo kutoka kwa maandiko yaliyotajwa.

Wimbo 38 (67) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA APRILI 18

Wimbo 41 (77)

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Rudia habari zilizomo katika “Kijitabu Blood Kitakachodarisiwa.” Ni jambo la maana sana wote waweke nyongeza ili waitumie wakati wa Funzo la Kitabu la Kundi. Mhubiri ambaye amejitayarisha vizuri aonyeshe jinsi ya kutoa uandikishaji, akiunganisha na elezo la kumalizia juu ya Isaya 48:17, 18 kulingana na Kichwa cha Mazungumzo.

Dak. 18: Tunaweza Kuwasaidiaje Mapainia Wetu? Hotuba inayotegemea mambo ya msingi kutoka nyongeza katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Agosti 1986, mafungu 12-20, na makala katika Mnara wa Mlinzi wa Agosti 1, 1982 juu ya “Yehova Ategemeza Jeshi Lake la Watumishi wa Wakati Wote.” Mapainia wanahitaji msaada wetu nao wanauthamini. Kazia kile ambacho kundi la kwenu linaweza kufanya kuwapa kitia-moyo na msaada.

Dak. 15: Mwangalizi wa Utumishi awahoji akina ndugu ambao wamepewa mgawo wa kutunza idara za vitabu na magazeti. (omSW uku. 124) Waombe wapitie kifupi kazi za idara zao. Eleza jinsi ushirikiano wa wote kundini ni jambo la maana sana. Tia moyo kwamba vifaa vya pekee viagizwe kupitia kundi badala ya kuagiza moja kwa moja kutoka kwa Sosaiti, kuchukua agizo la magazeti kwa ukawaida, kutoa taarifa mapema kuhusu badiliko lo lote la agizo la magazeti, na kadhalika. Tia ndani maneno yenye uthamini kwa kazi ambayo watumishi wa huduma wanafanya kwa ajili ya kundi na kwa ushirikiano wa wahubiri katika mambo haya yanayohitajiwa sana.

Wimbo 28 (48) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA APRILI 25

Wimbo 58 (130)

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Toa wonyesho mfupi kuhusu utoaji wa magazeti ya karibuni ambayo yatatolewa juma hili. Onyesho makala moja katika kila toleo ambayo inaweza kuvutia sana watu walio katika eneo lenu. Tia moyo kushiriki katika utumishi Jumapili ya kwanza ya Mei.

Dak. 18: Kutangaza Habari Njema—Kwa Kutumia Trakti Katika Kila Fursa. Mazungumzo ya maswali na majibu. Tia ndani maonyesho mafupi ya kutumia trakti kwa kutoa ushuhuda wa vivi hivi shuleni na kazini.

Dak. 15: Mahitaji ya kundi lenu. Au hotuba kuhusu “Kupuuza Maonyo na Kutahini Mungu” katika Mnara wa Mlinzi wa Desemba 15, 1987, kurasa 21-5.

Wimbo 18 (55) na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki