Maswali ya Funzo la Kijitabu Mashahidi wa Yehova na Suala la Damu
Juma la Kwanza
3 1 Ni uhakika gani juu ya damu unaoendelea kueleweka vizuri zaidi?
3 2 Ni njia gani ya utibabu inayokubaliwa, lakini ni nani wasiokubali?
3 3, 4 Ni maoni gani ya Biblia ambayo Mashahidi wa Yehova hushikilia juu ya uhai, na ni maswali gani yanayozushwa na hili?
3 5 Kusudi la kichapo hiki ni nini, na jambo hili litashughulikiwa jinsi gani?
4 1 Habari hii ni yenye kupendeza kwa nani?
4 2 Ni baadhi ya maoni gani mengine kuhusu damu, na ni juu ya msingi gani Mashahidi wa Yehova wanachukua msimamo kuhusu damu?
5 1 Kwa sababu ya msimamo unaochukuliwa na Mashahidi wa Yehova, ni swali gani linalotokea kimantiki?
5 2, 3 Ni nini linaloonyesha kwamba Biblia ina mengi ya kusema juu ya damu, na Mungu alitoa amri gani kuhusu damu mapema mwa historia ya aina ya binadamu?
6 1 Ni nini linaloonyesha kwamba katika kuua wanyama mengi zaidi ya ulaji yanahusika?
6 2, 3 Muumba aliambatanisha nini kwenye utumizi wa damu, na sisi tunajuaje kwamba si damu ya wanyama tu inayohusika?
7 1, 2 Ilikuwa aina gani ya amri aliyopewa Noa kuhusu damu, na ni maelezo gani ya rabi mmoja yanayohusu hapa?
8 1, 2 Ni sheria gani kwa Waisraeli iliyoonyesha kwamba marufuku ya Mungu juu ya damu yalikuwa yangali yakitumika, na ilikuwa njia gani pekee Waisraeli wangeweza kutumia damu?
8 3, 4 (a) Ni hadhari gani ambayo wawindaji Waisraeli walitakwa kuchukua walipoua wanyama kwa ajili ya chakula, na kwa nini? (b) Kwa kutii amri hii, walionyesha utambuzi wa uhakika gani?
9 1 (a) Ni adhabu gani zilizoonyesha kwamba kuvunja sheria ya Mungu juu ya damu kulikuwa kosa zito? (b) Ni maandiko gani yanayoonyesha kwamba kula mnofu pamoja na damu ndani yao kulitokeza hatia?
9 2 Ni kielelezo kipi cha Kimaandiko kinachoonyesha kwamba sheria ya Mungu juu ya damu haingeweza kuwekwa kando wakati wa dharura?
Juma la Pili
10 1 Kwa nini ni jambo lenye akili kukata maneno kwamba sheria ya Mungu kuhusu damu ya mnyama inatumika pia kwa damu ya kibinadamu?
10 2 Ni matokeo gani ambayo kifo cha kidhabihi cha Mesiya kilikuwa nayo kwenye vizuizi vya ulaji vya ile sheria ya Musa?
10 3 Wakati wa kushughulikia suala la tohara kwa ajili ya Wakristo wasio Wayahudi, ni nini lililoamuliwa kuhusu damu?
11 1 Uamuzi huu wa baraza la kimitume ulikuja kuwa sehemu ya nini?
11 2, 3 Uamuzi huo ulitaarifu nini waziwazi, na tunajuaje kwamba haukuwa kauli tu ya mitume?
12 1 Kulingana na Profesa Walther Zimmerli, amri hiyo ilifanyiza tofauti gani?
12 2 Ni nini linaloonyesha kwamba amri ya kushika mwiko wa damu haikuwa kizuizi cha ulaji tu bali ilikuwa takwa la kimaadili?
12 3, 4 Ni nini linaloonyesha aina yenye kudumu ya katazo la damu na kwamba halikuwa takwa la muda tu?
13 1, 2 Eusebio anasema nini kuhusu kutambuliwa kwa katazo la damu katika siku yake?
13 3 hadi 14 2 Ni nini walilosema Tertulliano na Minusio Feliki kwa habari ya Wakristo kutokula damu katika siku yao?
14 3, 4 Ni taarifa gani alizotoa Askofu na mwanachuo wa Biblia Mkatoliki juu ya kisa cha damu?
15 1 Baraza la Kwiniseksiti lilitaarifu nini kuhusu damu, na Otto wa Bamberg alisema nini kwa waongofu wapya kuhusu damu?
15 2 Martin Lutheri aliandika nini kuhusu Matendo 15:28, 29
15 3 Ni elezo gani alilofanya mwanatheolojia Mbaptisti juu ya Mwanzo 9:3, 4?
16 1 Ni jibu gani ambalo William Jones kiongozi wa kidini aliwapa wale ambao wangepuuza katazo la Biblia juu ya damu?
16 2 Ni azimio gani la Mashahidi wa Yehova kuhusu damu, likitegemezwa juu ya mambo ya uhakika na maandiko gani?
Juma la Tatu
17 1 Ni mambo gani matatu ambayo yamethibitishwa, na ni upi ulio msingi wa Kimaandiko kwa kila moja?
17 2, 3 Ni swali gani linalojitokeza lenyewe sasa, na ni mbinu gani za kitiba za ki-siku-hizi ambazo huenda kanuni za Biblia zikasemwa kuwa zinatiwa ndani?
17 4 hadi 18 1 Ni tofauti gani isiyofanywa katika Matendo 15:29, na kwa sababu zipi?
18 2 Ni msimamo gani thabiti ambao Mashahidi wa Yehova wanachukua, nao wanasadikishwa juu ya nini?
19 1, 2 Ni nini kilicho hatarini katika suala la damu, nasi tunakubali maneno gani ya mtunga zaburi kwa moyo wote mzima?
19 3, 4
20 1 Ni daraka gani ambalo Mashahidi wa Yehova wanabeba?
20 2, 3 (a) Ni pingamizi gani linalozuka kwa kukataa kutiwa damu mishipani? (b) Kwa nini Mashahidi hawaweza kushtakiwa kuwa ujiuaji, kama inavyoonwa na ushuhuda wa wengine?
21 1 Kwa nini kukataa kutiwa damu mishipani si zoezi la “haki ya kufa”?
21 2 Ni haki zipi ambazo mahakama zimewapa watu mmoja mmoja, na kwa nini ndivyo ilivyo kimantiki?
22 1, 2 (a) Mgonjwa ni mwamuzi wa mwisho juu ya nini? (b) Haki na wajibu wa tabibu unawekewa hadi na uhuru gani wa mwanadamu?
22 3 Watu fulani wana mwelekeo gani kuhusu kuhifadhi uhai, lakini jambo hili linatokeza swali gani?
23 1 Kulingana na N. L. Cantor, ni nini linaloonyesha kwamba utakato wa uhai silo la maana kupita yote, na hili lingetolewaje kielezi?
23 2 Ni msimamo gani wa Mashahidi unaozuia mtu mwingineye yote asijaribu kuwapa kinguvu utibabu fulani unaovunja kanuni zao?
24 1 Katika jarida moja la kitiba, ni taarifa gani iliyotolewa juu ya madaktari wanaojaribu kutumia kinguvu utibabu fulani unaoharibu dhamiri ya mgonjwa?
Juma la Nne
24 2, 3 Kwa nini huenda daktari akaona inataabisha kushughulika na Shahidi anayekataa kutiwa damu mishipani?
25 1, 2 Ni kulingana na kanuni gani za kisheria na kitiba huenda daktari mpasuaji asifuate masadikisho yake mwenyewe ikiwa yanaharibu dhamiri ya mgonjwa?
26 1, 2 Badala ya kuachilia kisa fulani, daktari amepaswa afanye nini anapokabiliwa na katao la mgonjwa kutiwa damu mishipani?
27 1 Ni nini linaloweza kusemwa juu ya wajibu mwingi wa kiadili wa wote wawili mgonjwa na daktari kuhusu utibabu ‘usio wa kikawaida’?
27 2 Ni msimamo gani wanaochukua Mashahidi kwa habari ya utibabu kwa ujumla, lakini isipokuwa nini?
27 3 Ni mambo gani ya uhakika ambayo Mashihidi wanathamini kuhusiana na msimamo wao wa damu?
28 1 Mashahidi wana habari juu ya uhakika gani, nao wana nia ya kukabili nini?
28 2 Ni mkataa gani uliofikiwa katika kisa kimoja chenye kupita kiasi baada ya upasuaji wenye mafinikio bila damu?
29 1 Kwa nini madaktari hawahitaji kuogopa kwamba Mashahidi watawashtaki kwa kutofanya kazi vizuri kwa sababu ya msimamo wao juu ya damu?
29 2 Ni sehemu gani muhimu ya fomu ambayo AMA hupendekeza itiwe sahihi na wagonjwa ambao wanakataa kutiwa damu mishipani?
30 1 Mashahidi wanaonyeshaje kwamba wana nia ya kukubali daraka la kibinafsi kwa kukataa kutiwa damu mishipani?
30 2 Ni nini ambalo limesemwa juu ya uwezekano wa daktari kushtakiwa kwa kutomtia kinguvu mgonjwa damu mishipani?
30 3Ni msimamo gani ulio katika Uingereza mgonjwa anapokufa kwa sababu ya kuwa amekataa kutiwa damu mishipani?
31 1, 2 Daktari ana wajibu gani wa kiadili, lakini ni wajibu gani wa kiadili ambao hana?
31 3 Ni shtaka gani ambalo daktari angestahili ikiwa angemtia kinguvu damu mishipani mgonjwa aliye Shahidi?
32 1, 2 Ni mwendo gani wa daktari ambao ungekuwa “jambo la kuchukiza sana kulingana na maadili” kwa daktari, na kwa nini hivyo?
32 3 mpaka 33 1 (a) Medical Tribune ya Ujeremani Magharibi lililazimika kusema nini juu ya kumtia mgonjwa damu mishipani akiwa hana fahamu? (b) Ni amri gani iliyotolewa na mahakama iliyotilia nguvu msimamo huu, ikiongoza kwenye mkataa gani?
Juma la Tano
33 2, 3 (a) Ni upande gani wa habari hii ambao ni wenye kuwashwa sana hisia za moyoni? (b) Mashahidi wanahisije juu ya jambo hilo, na kwa nini?
34 1, (a) Jambo gani limetokea kwa sababu ya ukosefu wa fundisho la wazazi? (b) Tofauti na hilo, wazazi Mashahidi wanafanya nini?
35 1, 2 Kwa nini daktari hapaswi kuhisi kwamba ni lazima amtie mtoto damu mishipani bila kujali matakwa thabiti ya wazazi kupinga hilo?
35 3 Kwa nini haipatani kimsingi kumtia kinguvu damu mishipani mtoto wa wazazi Mashahidi?
36 1 Taja kutopatana kukubwa kunakopatikana katika hospitali fulani fulani.
36 2 Mhadhiri Msikochi wa koleji alilazimika kusema nini juu ya kuwatia kinguvu damu mishipani watu wazima na watoto?
37 1, 2 Ile kanuni ya kuchagua analotaka mtu katika utibabu inakanushaje kutia kinguvu damu mishipani?
37 3 Ni jambo gani la uhakika juu ya aina ya maarifa ya kitiba hukanusha zaidi kutia kinguvu damu mishipani?
37 4 Ile kanuni ya kutibu mtu mzima ina uhusiano gani na utiwaji kinguvu wa damu mishipani?
38 1, 2 Ni nini linaloweza kusemwa juu ya kuponya mwili huku roho ya mtu ikivunjwa?
38 3 mpaka 39 2 Ni mambo gani ya hakika yanayokanusha kwamba msimamo wa Mashahidi kuhusu kutiwa damu mishipani si jambo lisilo la kiakili?
39 3 4 Kwa nini madaktari fulani wanashindwa kuona utiwaji damu mishipani kwa njia ya kupinga, na kwa sababu gani mahakimu fulani wamependekeza utibabu tofauti?
40 1, 2 Ni jambo gani la uhakika juu ya damu linaloathiri sana ubora wa thamani ya kutia damu mishipani?
40 3 mpaka 41 1 Ni tabia gani za damu zilizo na uhusiano na kihatarishi katika kutia damu mishipani?
41 2-4 Kuna ushuhuda gani wa kuonyesha kwamba kutia damu mishipani kunazo hatari ndani?
42 2-3 Kwa nini madaktari wenye maarifa hawawezi kupuuza hatari za kutiwa damu mishipani kwa kusema zimetiwa chumvi?
43 1 Je! kuna uwezekano wa ondoleo la matatizo ya kutiwa damu mishipani? Ikiwa hakuna, kwa nini?
Juma la Sita
43 2, 3 Ni aina gani mbalimbali za hatari zinazoshirikishwa na kutiwa damu mishipani?
44 1, 2 Ni baadhi gani za matokeo yenye kudhuru ya mara hiyo ya kutiwa damu mishipani?
44 3-5 Ni kwa kadiri gani hatari ya kupitisha ugonjwa inashirikishwa na kutiwa damu mishipani?
45 1, 2 Ni jambo gani linaloweza kusemwa juu ya ugonjwa wa seramu hepataiti?
45 3 Kwa nini uwezekano wa Shahidi kupata seramu hepataiti ni zaidi ya hatari inayoweza kutetewa?
46 1, 2 Ni mambo gani ya uhakika yanayokanusha mgonjwa kuhakikishiwa vya kufaa kwamba ataokoka shambulio la seramu hepataiti?
46 3, 4 Ni kwa kadiri gani mbinu za ki-siku-hizi zimeondolea mbali hatari za kupata seramu hepataiti kutokana na kutiwa damu mishipani?
47 1 Ni tatizo gani la pande mbili linalotokezwa na damu iliyoambukizwa kaswende?
47 2 hadi 48 1 Ni maambukizo gani mengine ambayo yamkini kupitishwa kwa kutiwa damu mishipani?
48 2 Ni hatari gani nyingine inayoshirikishwa na kutiwa damu mishipani, na ni kubwa jinsi gani?
48 3 Kwa sababu ya hatari zinazoshirikishwa na kutiwa damu mishipani, hospitali fulani zinawataka wagonjwa wafanye nini?
48 4 Ni sababu gani ya msingi inayofanya Mashahidi wasikubali kutiwa damu mishipani?
49 1-3 Katika upasuaji wa hiari, kuna njia gani nyinginezo zinazoweza kutumiwa badala ya damu?
50 1, 2 Ni upi ulio uhitaji mkubwa hasa wakati damu nyingi sana imepotezwa?
51 1 Ni upi ulio umajimaji wa kuchagua wakati damu nyingi sana imepotezwa?
51 2, 3 Ni kwa kadiri gani mmoja anaweza kuongeza upotevu wa damu, na kwa nini viyeyuko vinavyotumiwa kuwa njia nyingine si vibadala vya damu?
Juma la Saba
52 1, 2 Mambo ya hakika yameonyesha nini kuhusu kipimo kilicho salama cha damu au hemoglobini iliyomo kwa ajili ya upasuaji?
53 1, 2 Ni jambo gani ambalo limepata kujulikana kwa kujifunza habari ya kutia damu mishipani kuongezea mara hiyo uwezo wa damu kubeba oksijeni?
53 3 Ni baadhi ya umajimaji gani ambao umetumiwa badala ya kutiwa damu mishipani?
54 1 Ni vipi vingine viongeza-kiasi-cha umajimaji-damu ambavyo vimetumiwa kwa matokeo mazuri?
54 2 Ni jambo gani linaloweza kusemwa juu ya matumizi ya viongeza umajimaji-damu mbalimbali katika hatua hatari ya upungufu wa damu?
54 3 hadi 55 1 Ni uthibati gani inaoyonyesha kwamba damu si njia pekee yenye matokeo badala ya damu iliyopotea?
55 2, 3 Taja baadhi ya faida viongeza-kiasi-cha umajimaji wa damu kuliko damu yenyewe.
55 4 Ni mambo gani ya uhakika yenye kupendeza ambayo ujuzi wa Dakt. Denton Cooley umefunua
56 1 Yamekuwa matokeo gani ya muda mrefu ya upasuaji wa moyo bila kutumia damu kwa watu wazima na watoto Mashahidi?
57 1, 2 Yamekuwa matokeo gani mahali ambako Mashahidi wamelazimika kuhitaji upasuaji bila kutumia damu na ambako kwa kawaida damu ni muhimu sana?
57 3 Ni mambo gani Dakt. Philip Roen ambayo ameona?
58 1, 2 Ni mambo gani ya hakika yanayoonyesha kwamba msimamo wa Mashahidi kuhusu kutiwa damu mishipani unaweza kukubaliwa kitiba?
59 1, 2 (a) Kwa sababu ya mambo yote ya hakika yaliyotangulia, daktari amepaswa kuthamini nini juu ya Mashahidi wa Yehova? (b) Hii inamaanisha nini katika kutenda kwake hasa?
60 1, 2 Ni shauri gani wanalopewa Mashahidi wanapokabiliwa na suala la kutiwa damu mishipani?
60 3 Kwa msimamo wao juu ya damu, Mashahidi wanadhihirisha nini, kupatana na kielelzo gani cha Wakristo wa mapema?
Juma la Kwanza
Juma la Pili
3 HUDUMA YA UFALME YETU, APRILI 1988
Juma la Tatu
Juma la Nne
4
Juma la Tano
5
Juma la Sita
Juma la Saba
6