Chagua Mambo Yafaayo ya Kuzungumzia
1 Tunaweza kufanya nini ili tuwatie watu moyo wasome Mnara wa Mlinzi na Amkeni! kwa ukawaida? Tunahitaji kuwa na mambo ya kupendeza ya kuzungumzia tunapopendekeza magazeti hayo kwa wengine. Ikiwa tumefahamiana vema na watu katika eneo letu na tunawaweka akilini tunaposoma magazeti hayo, tunaweza kuwa tukitafuta mambo ya kuzungumzia yanayoweza kunasa kupendezwa kwao.
2 Katika maeneo mengine, huenda watu wakawa na malezi yaleyale, jambo linalofanya iwe rahisi kuona lile linaloweza kuwa la kupendeza wote kwa ujumla. Lakini katika maeneo mengine, huenda tukapata watu wa malezi mbalimbali. Ikiwa tuna mambo kadha akilini ya kuzungumzia, tunaweza kuchagua mojawapo linalofaa zaidi kila mtu tunayekutana naye.
3 Usiwe mwenye haraka kuweka kando matoleo ya magazeti ya zamani unapopokea yale mapya zaidi. Baada ya kukazia jambo moja, makala moja, na gazeti moja, huenda ukaona kuwa inasaidia kumkabidhi mwenye nyumba matoleo matatu au manne ya magazeti hayo na umruhusu mwenye nyumba achague yale anayotaka kusoma. Tafadhali usijaribu kupitia mambo ya kuzungumzia katika kila gazeti. Badala ya hivyo, kazia gazeti moja kisha uonyeshe unamna-namna wa habari zinazopatikana ili mwenye nyumba achague. Ikiwa twapata kwamba tunapokea magazeti mengi zaidi ya yale tunayoweza kugawanya, tunapaswa tufikirie kurekebisha agizo letu.
4 Kwa kutumia nyakati zote mambo yafaayo ya kuzungumzia, huenda tukachochea wengine kusoma magazeti yetu na labda tuwasaidie waanze kutembea kwenye njia iendayo kwenye uhai. (Mt. 7:14) Tukitoa ufikirio wa uangalifu kwa jambo hilo la maana, tunaweza kuwa na uhakika wa kupata baraka za Yehova.