Matangazo
◼ Toleo la Fasihi kwa Januari: Kitabu chochote cha kurasa 192 kilichochapishwa katika 1980 au mapema zaidi kwa nusu ya mchango wa kawaida. Mapainia waweza kupokea nakala kwa nusu bei ya kawaida kwa mapainia wa kawaida. Makundi yaweza kuomba kupunguziwa bei kwa sababu ya tofauti ya bei ya vitabu hivi vya zamani vilivyochapishwa kabla ya 1980 kwa kutumia fomu ya S-20-SW. Ikiwa kundi halina akiba ya vitabu hivyo, kitabu Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje? kitolewe na chaweza kuagizwa kutoka ofisi ya tawi au depo mbalimbali. Februari: Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Machi: Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Aprili na Mei: Uandikishaji wa Mnara wa Mlinzi. TAARIFA: Makundi yatakayohitaji vifaa vya kampeni vilivyotajwa juu yapaswa yaviagize kwenye Fomu ya Agizo la Vitabu (S-14-SW) ya kila mwezi itakayofuata.
◼ Kuanzia Februari 1, na si baada ya Machi 7, hotuba ya watu wote mpya ya waangalizi wa mzunguko itakuwa “Kuwatazama Vijana Kulingana na Maoni ya Yehova.”
◼ Hotuba ya pekee kwa ajili ya majira ya Ukumbusho ya 1993 itatolewa ulimweguni pote Jumapili, Machi 28. Kichwa cha habari cha hotuba hiyo kitakuwa “‘Vitendo vya Mungu’—Unavionaje?” Muhtasari utaandaliwa. Makundi yale yenye ziara ya mwangalizi wa mzunguko, kusanyiko la mzunguko, au siku ya kusanyiko la pekee mwisho-juma huo yatakuwa na hotuba hiyo ya pekee juma lifuatalo. Hakuna kundi linalopasa kuwa na hotuba hiyo ya pekee kabla ya Machi 28.
◼ Kuanzia Januari 1, 1993, chapa ya mara moja kwa mwezi ya Mnara wa Mlinzi katika lugha ya Kilithuania itapatikana, hivyo ikifikisha idadi ya lugha ambazo gazeti hilo huchapishwa kuwa 112. Pia katika Januari chapa ya Mnara wa Mlinzi katika Kitelugu itakuwa ya mara mbili kwa mwezi.
◼ Tarehe ya Ukumbusho kwa ajili ya mwaka huu ni Jumanne, Aprili 6, 1993, baada ya jua kushuka. Muhtasari mpya wa Ukumbusho utaandaliwa ili kutumiwa. Wazee wanapaswa waanze matayarisho ya kwanza-kwanza kwa ajili ya pindi hiyo ya maana.
◼ Andiko-mwaka la 1993: “Unifunze mimi, Ee Yehova. . . . Ungamanisha moyo wangu kuhofu jina lako.”—Zaburi 86:11, NW.