Pendeleo Zuri la Utumishi
1 Msomaji mmoja alisema kwamba alikuwa amejifunza mengi zaidi yenye thamani halisi kwa kusoma Mnara wa Mlinzi na Amkeni! kuliko yale aliyojifunza katika miaka sita ya elimu ya chuo kikuu. Ni jambo la kawaida kwa wasomaji kusema maneno hayo ya uthamini yenye kuchangamsha moyo baada ya kuyasoma magazeti hayo kwa muda mfupi tu. Tumependelewa kama nini kushiriki magazeti yetu kwa ukawaidi na wale wanaoyathamini kwelikweli!
2 Watu wengi, ingawa wanapendezwa na kweli kadiri fulani, hawajafanya maendeleo hadi hatua ya kukubali funzo la Biblia nyumbani. Lakini kupendezwa kwao kwaweza kukuzwa ikiwa mtu fulani afanya ziara za kuwarudia kikawaida akiwa na kila toleo jipya la Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Naam, kupeleka magazeti kwa uaminifu katika njia ya kupelekea watu magazeti kwa ukawaida kumesaidia kuwasukuma watu wakubali hatimaye kuwa na funzo la Biblia la kawaida.
3 Tunanufaika kibinafsi kwa kuwa na njia ya kupelekea watu magazeti kwa ukawaida tukiyasoma magazeti kwanza na kutia alama mambo hususa yatakayokuwa yenye kupendeza hasa kwa kila mtu aliye kwenye orodha yetu.
4 Kumbuka kwamba ni kadiri ya kupendezwa kwa mwenye nyumba inayoamua kama unapaswa kutia ndani jina lake kwenye orodha yako ya wale waliomo katika njia yako ya kupelekea watu magazeti kwa ukawaida. Mtu huyo akionyesha kupendezwa kikweli anapoyakubali magazeti, waweza kueleza kwamba makala zenye kutokeza huonekana katika magazeti yetu kila majuma mawili na kwamba utafurahia kuwapelekea. Hakikisha kufuatia jambo hilo kwa ukawaida, ukitumia kwa kujifaidi fursa za kuzungumza pamoja na mwenye nyumba habari za Biblia. Twajua utafurahia pendeleo hilo zuri la utumishi.