Wachukuaji Nuru Katika Ujirani
1 Baada ya kuhudhuria mkusanyiko wa wilaya wa mwaka huu, tunafahamu vizuri zaidi uhitaji wa kuwa wachukuaji nuru kwa majirani wetu. (Mt. 5:14) Tunapofikiria habari yote iliyotolewa kwenye programu hiyo na kujitahidi kuitumia katika maisha yetu ya kila siku, tunasaidiwa kumkaribia Yehova katika ibada ya kweli na kuwasaidia wengine wajifunze juu ya ahadi za Yehova.
2 Fursa zetu za kuchukua nuru ziliongezeka wakati trakti mpya yenye kichwa Je! Ulimwengu Huu Utaokoka? ilipotolewa mwishoni mwa kipindi cha Ijumaa asubuhi. Maonyesho ya Jumamosi asubuhi yalisaidia sana katika kuonyesha jinsi trakti hiyo inavyoweza kutumiwa. Pamoja na hiyo, kulikuwako tangazo kwamba trakti nyinginezo tatu zingepatikana karibuni. Hizo zina vichwa Faraja kwa Walioshuka Moyo, Furahia Maisha ya Familia, na Ni Nani Hasa Anayeutawala Ulimwengu? Kitia-moyo kilitolewa cha kuchukua vyombo hivyo vifaavyo ili kuvitumia wakati fursa zinapotokea.
3 Mwishoni mwa hotuba “Kukombolewa Wakati wa Kufunuliwa kwa Yesu Kristo” Jumamosi alasiri, broshua mpya yenye kichwa Je! Kweli Mungu Anatujali? ilitolewa. Broshua hiyo yenye rangi kamili na picha zenye kupendeza itajibu maswali mengi ambayo watu huuliza, kama vile: Kwa nini Mungu huruhusu kuteseka? Je! kuteseka kutapata kuisha wakati wowote? Tunajuaje kwamba tumo katika siku za mwisho? Dunia itageuzwaje iwe paradiso? Tunaweza kupataje uhai wa milele katika ulimwengu mpya wa Mungu? Broshua hiyo itakuwa chombo bora kabisa cha kuanzia mafunzo mapya.
4 Tunashukuru kama nini kwa ajili ya wingi wa chakula cha kiroho kilichopokewa kwenye “Wachukuaji Nuru” Mkusanyiko wa Wilaya! Sisi, tukiwa wachukuaji wa nuru ya Mungu ya kiroho, na tuazimie kuonyesha uthamini wetu wa kuhisiwa moyoni kupitia kutumia kwa kudhamiria yale tumejifunza na kutumia kwa bidii-nyendelevu matoleo hayo mazuri mapya katika kuwasaidia watu kila mahali wamjue na kumtumikia Yehova.