Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 1/15 kur. 14-19
  • Baraka Nyingi Kwenye “Wachukuaji Nuru” Mikusanyiko ya Wilaya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Baraka Nyingi Kwenye “Wachukuaji Nuru” Mikusanyiko ya Wilaya
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “Karibuni, Enyi Nyote Wachukuaji Nuru!”
  • Wachukuaji Nuru Wachanga
  • Acha Nuru Iangaze
  • Kuwapo na Kufunuliwa kwa Kristo
  • Nyumba za Kikristo
  • Jumapili Alasiri
  • Njooni Kwenye “Wachukuaji Nuru” Mkusanyiko wa Wilaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • “Wachukuaji Nuru” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1992
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Wachukuaji Nuru Katika Ujirani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Mikusanyiko Uthibitisho wa Udugu Wetu
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 1/15 kur. 14-19

Baraka Nyingi Kwenye “Wachukuaji Nuru” Mikusanyiko ya Wilaya

MIAKA 2,700 hivi iliyopita, nabii Isaya aliandika hivi: “Tazama, giza litafunika dunia, na giza kuu litazifunika kabila za watu.” (Isaya 60:2) Maneno hayo ni ya kweli kama nini! Hata hivyo, kuna tumaini, kwani Yehova amesababisha nuru iangaze. Mwaka jana, wale wapendao nuru ya Mungu walikaribishwa kwa uchangamfu kuhudhuria “Wachukuaji Nuru” Mkusanyiko wa Wilaya.

Programu ya mkusanyiko huo ulitolewa kwanza mwezi wa Juni katika Amerika Kaskazini. Katika miezi iliyofuata, ilitolewa katika Ulaya ya Mashariki na ya Magharibi, Amerika ya Kati na ya Kusini, Afrika, Esia, na visiwa vya bahari. Wale waliohudhuria walijumulika kuwa mamilioni. Nao wamefurahia karamu kubwa ya kiroho iliyoje!

“Karibuni, Enyi Nyote Wachukuaji Nuru!”

Katika sehemu nyingi mkusanyiko ulianza Ijumaa na ukamalizika Jumapili alasiri. Wakusanyikaji walipokalia viti vyao Ijumaa asubuhi, walifurahia kusikia pitio fupi la njia ambayo nuru ya Yehova imeangaza hata zaidi katika siku hizi za mwisho. Kisha mwenyekiti wa mkusanyiko akaenda jukwaani. Alikazia kwamba Wakristo wa kweli wanapaswa wawe wachukuaji wa nuru akasema kwa uchangamfu: “Karibuni, enyi nyote wachukuaji nuru!” Programu ya mkusanyiko ingewasaidia wahudhuriaji waendelee kuangaza nuru ya Yehova.

Hotuba ya msingi iliwekea msingi mkusanyiko mzima. Msemaji huyo aliwakumbusha wakusanyikaji kwamba taa za wanadamu zilizimwa huko nyuma katika bustani ya Edeni. Tangu wakati huo, Shetani amewapofusha wanadamu wasione nuru ya kweli. (2 Wakorintho 4:4) Hata hivyo, Yesu alikuja akiwa “nuru ya mataifa.” (Isaya 42:1-6) Alifunua uwongo wa kidini, alitambulisha matendo mabaya ya giza, alitegemeza enzi kuu ya Yehova, na kuhubiri habari njema za Ufalme. Wafuasi wa Yesu walifanya vivyo hivyo—na wangali wanafanya hivyo! (Mathayo 28:19, 20) Msemaji alisema hivi kwa kuchochea: “Sisi, kama vile Yesu, twaweza kuwa wachukuaji nuru. Hakuna kazi nyingine yoyote iliyo ya maana zaidi katika siku yetu. Na hakuna pendeleo jingine kubwa zaidi.”

Kipindi cha kwanza kilipokuwa kikimalizika tu, kulikuwako jambo la kushangaza. Mwenyekiti wa mkusanyiko alirudi jukwaani na kutangaza toleo la mfululizo wa trakti nne mpya. Makofi yenye uchangamfu yalikaribisha jambo hilo, na kila mhudhuriaji alipewa nakala moja ya kila trakti.

Ijumaa alasiri, programu ya mkusanyiko ilielekeza fikira kwenye shauri la msingi kwa Wakristo wenye kuchukua nuru. Hotuba mbili za kwanza ziliandaa shauri zuri juu ya namna ya kuepuka kuchafuliwa na giza la ulimwengu. Kwa kuwa Shetani aweza kutokea akiwa malaika wa nuru, ni muhimu kudumisha maoni ya kiroho ili mambo machafu ya ulimwengu yasitupotoshe. (2 Wakorintho 11:14) Paulo alishauri hivi: “Msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.” (Warumi 12:2) Wahudhuriaji wa mkusanyiko walisikia kwamba kugeuzwa kwa Mkristo ni utaratibu wenye kuendelea. Akili zetu zinaendelea kusafishwa na kufinyangwa tunapojifunza Neno la Mungu na kutumia yale tunayojifunza. Hivyo, tunazidi kuwa kama Yesu, ‘aliyejaa fadhili isiyostahiliwa na kweli.’—Yohana 1:14, NW.

Wachukuaji Nuru Wachanga

Sehemu ya pili ya Ijumaa alasiri ilielekezwa kwa vijana. Hotuba ya kwanza (“Vijana—Mnafuatia Nini?”) iliwapongeza Wakristo wachanga walio vielelezo vizuri sana vya uaminifu. Lakini iliwakumbusha kwamba wao ni shabaha maalumu ya Shetani. Hata mwanariadha mwenye kuzoezwa vizuri huhitaji kocha. Kwa njia iyo hiyo, vijana wanahitaji msaada wa wazazi wao na wa kundi ili waendelee kutembea katika nuru.

Hilo lilikaziwa na ile drama bora sana Kufanya Yaliyo Sawa Machoni pa Yehova, iliyofunga programu ya Ijumaa. Kielelezo cha Mfalme Yosia kilikaziwa. Hata wakati alipokuwa mvulana, aliazimia kumtumikia Yehova. Uvutano mbaya ulimzunguka, lakini kwa mwongozo wa kuhani mkuu Hilkia na kwa sababu ya upendo wake mwenyewe kwa Sheria ya Mungu, Yosia alifanya yaliyo sawa machoni pa Yehova. Wakristo wachanga leo na watende kwa njia iyo hiyo.

Acha Nuru Iangaze

Baada ya pumziko la usiku, wahudhuriaji walikuja kwenye mkusanyiko Jumamosi asubuhi wakiwa tayari kujengwa zaidi na shauri la Kimaandiko. Hawakukatishwa tamaa. Baada ya mazungumzo ya andiko la siku, programu iliendelea na mfululizo yenye kuorodhesha njia tofauti-tofauti ambazo kwazo Mkristo aweza kuacha nuru yake iangaze. (Mathayo 5:14-16) Kuhubiri ni njia moja ya muhimu, na mwenendo mzuri pia hufanyiza sehemu ya maana. Kama vile msemaji alivyosema, “kuhubiri kunawaambia wengine yale tunayoamini, lakini kuzoea upendo kunayaonyesha.”

Halafu fikira za wakusanyikaji zikaelekezwa kwenye msaada muhimu wa kuhubiri: trakti. Tangazo la siku iliyopita likiwa bado akilini, wahudhuriaji walisikia maono yenye kuthibitisha jinsi vifaa hivyo vidogo vilivyo vyenye nguvu. Wahudhuriaji walitiwa moyo wawe na ugavi wa trakti nyakati zote, wakiwa tayari kwa kila pindi.

Kisha fikira zikaelekezwa kwa mapainia, wale wapiga mbiu ya Ufalme wa wakati wote wanaojitahidi katika kuchukua nuru. Jinsi tunavyowathamini mapainia wetu wenye bidii! Na idadi yao inaongezeka. Hata katika nchi ambako uhuru wa ibada umetolewa hivi karibuni tu, idadi za mapainia zinaongezeka. Mapainia walitiwa moyo wathamini kama hazina pendeleo lao. Wale ambao bado si mapainia walihimizwa wafikirie hali yao. Labda wao pia wangeweza kupanga mambo yao ili waache nuru yao iangaze hata zaidi katika utumishi wa wakati wote.

Mara nyingi kuwa mchukuaji nuru kunatia ndani dhabihu, na hilo lilikaziwa katika hotuba iliyofuata, “Kutumikia Yehova kwa Roho ya Kujidhabihu.” Paulo alisihi sana hivi: “Itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu.” (Warumi 12:1) Roho ya kujidhabihu inaonyeshwa na wale wanaovumilia mnyanyaso. Mapainia hutoa dhabihu kila siku ili kubaki katika utumishi wa wakati wote. Kwa kweli, Wakristo wote wa kweli hutoa dhabihu, wakijihusisha katika utumishi wa Yehova badala ya ufuatiaji mbalimbali wenye ubinafsi wa vitu vya kimwili wa ulimwengu huu. Mwendo huo hutokeza baraka nyingi kutoka kwa Yehova.

Hotuba hiyo ilitumika kama utangulizi ufaao kwa ile iliyofuata—hotuba ya ubatizo. Wale waliobatizwa kwenye “Wachukuaji Nuru” Mkusanyiko wa Wilaya kwa hakika hawataisahau hotuba hiyo. Ubatizo wao utakuwa jambo kuu la maisha yao sikuzote. Walikumbushwa kwamba walikuwa wakifuata kielelezo cha Yesu Kristo, aliyebatizwa akiwa na umri wa miaka 30. Isitoshe, wale waliotaka kubatizwa walifurahi kukumbuka kwamba walikuwa ‘wameyavua matendo ya giza” na walikuwa wamefanya uamuzi wa ‘kumtumikia Yehova.’ (Warumi 12:11; 13:12) Kwa shangwe, walisimama mbele ya umati wa mkusanyiko na kutoa julisho la waziwazi lenye kusikika kabla ya kwenda kwenye ubatizo. (Warumi 10:10) Twaomba baraka ya Yehova juu ya wale wote waliofananisha wakfu wao wa kibinafsi kwake kwa kubatizwa kwa maji wakati wa “Wachukuaji Nuru” Mikusanyiko ya Wilaya.

Jumamosi alasiri ulikuwa wakati wa maonyo ya waziwazi. Hayo yalikuja kwa namna ya hotuba zenye vichwa “Epuka Mitego ya Pupa,” “Je! Mtu Fulani Anaharibu Mazoea Yako Yenye Mafaa?” na “Jilinde na Ibada ya Sanamu ya Kila Aina.” Hotuba hizo tatu zilitambulisha baadhi ya mbinu zinazotumiwa na Shetani ili kudhoofisha Mkristo. Yuda Iskariote alikuwa mtume, lakini alimsaliti Yesu ili kupata pesa. Samweli mchanga alikua katika kitovu chenyewe cha kitaifa cha ibada ya Yehova, lakini aliwekwa wazi kwenye ushirika mbaya sana bila kuweza kuuepuka. (1 Samweli 2:12, 18-20) Ibada ya Sanamu yaweza kutia ndani mambo kama vile ukosefu wa maadili katika ngono na kutamani. (Waefeso 5:5; Wakolosai 3:5) Naam, pupa, mashirika mabaya, na ibada ya sanamu ni mambo ya hatari na ni lazima yaepukwe.

Kisha habari ya programu ya mkusanyiko ikabadilika. Hotuba iliyofuata ilitokeza maswali ya Biblia kadhaa yenye kupendeza na kuyajibu. Kwa mfano, je, unaweza kueleza kama watu ambao hawakubali kweli na wanaokufa kabla ya dhiki kubwa watafufuliwa? Je! inafaa kutumia usemi “kutetewa kwa jina la Yehova”? Ili waongeze maarifa yao ya Biblia, wahudhuriaji walitiwa moyo watumie kikamili Watch Tower Publications Index, hasa chini ya kichwa “Maswali Kutoka kwa Wasomaji.”

Kuwapo na Kufunuliwa kwa Kristo

Sehemu ya kumalizia ya programu ya Jumamosi ilizungumzia unabii kwa mfululizo wenye kichwa “Kuangaza Nuru Juu ya Kuwapo kwa Kristo na Kufunuliwa Kwake.” Sehemu za “ishara” yenye kuthibitisha kuwapo kwa Yesu Kristo zilipitiwa. (Mathayo 24:3, NW) Katika sehemu ya pili, utendaji mbalimbali wa ki-siku-hizi wa “mtumwa mwaminifu mwenye akili” zilizungumziwa. (Mathayo 24:45-47) Ilionyeshwa kwamba tangu 1919 jamii ya mtumwa imeongoza kwa uaminifu kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme. Halafu mkutano mkubwa ukakusanywa kutoka mataifa yote ili kushiriki pamoja na Wakristo wapakwa-mafuta katika kuangaza nuru ya Yehova. Msemaji alimalizia hivi: “Acheni wote waendelee kwa bidii kumwunga mkono mtumwa mwaminifu mwenye akili. Ni kwa kufanya hivyo tu ndipo siku moja hivi karibuni wote wenye mfano wa kondoo wataweza kusikia maneno haya ya furaha: ‘Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa kwa ulimwengu.’”—Mathayo 25:34.

Msemaji wa mwisho alizungumzia maana na yale yanayohusishwa na kufunuliwa kwa Yesu Kristo. (1 Wakorintho 1:7) Kufunuliwa huko kutakuwa ono lililoje! Babuloni Mkubwa ataharibiwa. Vita kuu kati ya ulimwengu wa Shetani na Yesu na malaika zake itamalizika katika uharibifu wa mfumo huu. Mwishowe, Shetani mwenyewe atatiwa katika abiso na kufanywa asiweze kutenda. Lakini kutakuwako kitulizo kwa watu wa Mungu, kwa ndoa ya Mwana-Kondoo mbinguni na kutokezwa kwa dunia mpya. Msemaji aliwafurahisha wasikilizaji wake kwa kutoa broshua mpya Je! Kweli Mungu Anatujali? hiyo itakuwa yenye msaada kama nini kwa watu mmoja mmoja wanyenyekevu wanaohitaji kujua juu ya Muumba wetu mwenye kujali na makusudi yake kwetu!

Nyumba za Kikristo

Jumapili, siku ya mwisho ya mkusanyiko, ilikuwa imefika sasa. Hata hivyo, mengi yalikuwa bado yatolewe. Baada ya mazungumzo ya andiko la siku fikira zilielekezwa kwenye familia za Kikristo kwa mfululizo “Kujali Mmoja na Mwenzake Katika Nyumba ya Kikristo.” Sehemu ya kwanza iliwasaidia wakusanyikaji watambue ufunguo wa familia ya Kikristo yenye mafanikio: kutanguliza mambo ya kiroho. Sehemu ya pili ilitia moyo familia zifanye mambo pamoja, hata kama hilo linahusisha kuhudhuria mikutano, utumishi wa shambani, funzo la familia, au tafrija. Na sehemu ya tatu ya mfululizo huo uliwakumbusha wahudhuriaji kuhusu pendeleo lao na daraka la kuwajali walio wazee-wazee. “Ndugu na dada zetu wenye umri mkubwa zaidi ni faida kwa kundi,” akasema msemaji. Acheni tuthamini kama hazina ujuzi wao na kuiga uaminifu-maadili wao.

Maana na yale yanayohusishwa na usemi “timamu katika akili” yalizungumziwa baada ya hapo. (1 Petro 4:7) Mtu aliye timamu katika akili ni mwenye usawaziko, mwenye akili, mwenye kiasi, mnyenyekevu, na mwenye kusababu. Anaweza kutambua kati ya yaliyo sawa na yasiyo sawa, kweli na uwongo. Isitoshe, anajitahidi kudumisha afya nzuri ya kiroho.

Hotuba ya mwisho Jumapili asubuhi ilizungumzia ujitiisho wetu kwa Mungu na kwa Kristo. “Umaana wa kuwa na ujitiisho wenye uaminifu-mshikamanifu kwa Yehova Mungu na kwa Mwana wake, Yesu Kristo, wapasa kukaziwa sana,” akasema msemaji. Aliendelea kuonyesha jinsi hilo linavyoathiri kila sehemu ya maisha zetu. Ni nini kitakachotusaidia tubaki wenye kujitiisha? Sifa nne: upendo, hofu ya kimungu, imani, na unyenyekevu.

Jumapili Alasiri

Kwa ghafula, ilikuwa Jumapili alasiri na wakati wa kipindi cha mwisho cha mkusanyiko. Kwa wengi, ilionekana kwamba mkusanyiko ulikuwa umeanza tu, na tayari ulikuwa ukikaribia umalizio wao.

Hotuba ya watu wote ilikuwa na kichwa “Fuata Nuru ya Ulimwengu.” Wale waliokuwako walifurahishwa na elezo lenye kusisimua la fungu la nuru halisi katika kudumisha uhai. Kisha msemaji akaonyesha umaana mkubwa zaidi wa nuru ya kiroho. Nuru halisi hutuendeleza tukiwa hai kwa miongo michache, lakini nuru ya kiroho yaweza kutuendeleza tukiwa hai kwa umilele wote. Jambo kuu la hotuba hiyo lilikuwa mazungumzo ya mstari kwa mstari ya Yohana 1:1-16, ambamo Yesu atambulishwa kuwa nuru ya ulimwengu. Leo, katika miaka ya mwisho-mwisho ya mfumo huu mbovu, ni jambo la uharaka kuliko wakati mwingine wowote kufuata Yesu katika daraka hilo.

Baada ya muhtasari wa habari ya funzo la Mnara wa Mlinzi iliyogawiwa juma hilo, ulikuwa wakati wa hotuba ya kumalizia. Kwa furaha, msemaji alionyesha kwamba kuna mambo mengi ya kutazamia. Kwa kielelezo, alitangaza kaseti mpya ya drama Kufanya Mapenzi ya Mungu kwa Bidii. Na si hiyo tu. Kungekuwa mfululizo mpya wa vidio wenye kichwa The Bible—A Book of Fact and Prophecy, ya kwanza ikiwa na habari The Bible—Accurate History, Reliable Prophecy.

Mwishowe, msemaji alitangaza kwamba katika 1993 kungekuwako mkusanyiko wa wilaya wa siku nne, kutia na mikusanyiko ya pekee ya kimataifa katika Afrika, Esia, Ulaya, na Amerika Kusini. Hata ingawa “Wachukuaji Nuru” Mkusanyiko wa Wilaya ulikuwa ukiisha, wahudhuriaji wangeweza kuanza kufanya mipango kwa ajili ya mwaka ujao.

Ndipo ukawa wakati wa wahudhuriaji wa mkusanyiko kwenda nyumbani. Kwa hakika, walikuwa wameazimia zaidi ya wakati mwingine wowote kuendelea kuangaza nuru katika ulimwengu huu wenye giza. Baada ya siku tatu zenye kujaa mambo mazuri ya kiroho, maneno ya andiko la mwisho lililonukuliwa katika hotuba ya mwisho yalikuwa yamepata umaana mkubwa: “BWANA [Yehova, NW] ndiye aliye Mungu, naye ndiye aliyetupa nuru. . . . Mshukuruni BWANA [Yehova, NW] kwa kuwa ni mwema, kwa maana fadhili zake ni za milele.”—Zaburi 118:27, 29.

[Picha katika ukurasa wa 15]

Programu ya mkusanyiko katika Kirusi

[Picha katika ukurasa wa 16, 17]

Washiriki wa Baraza Linaloongoza walitoa hotuba kwenye mikusanyiko mingi

Wahudhuriaji Wajapani walikuwa miongoni mwa wale waliokusanyika katika St. Petersburg, Urusi

Drama ya Biblia yenye kuchochea ilikazia uhitaji wa kufanya yaliyo sawa machoni pa Yehova

Wachukuaji nuru wapya walifananisha wakfu wao kwa Yehova kwa kubatizwa

Wakusanyikaji wakisikiliza programu kwa makini katika St. Petersburg

[Picha katika ukurasa wa 18]

Wahudhuriaji walisisimuka kupokea broshua mpya “Je! Kweli Mungu Anatujali?”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki