Tumia Fursa za Kuwapelekea Watu Magazeti Kuanzisha Mafunzo ya Biblia
1. Kwa nini tengenezo la Yehova limekuwa likiwatia moyo wahubiri waendelee kuwapelekea watu magazeti kwa ukawaida?
1 Watu wengi hawapendi kujifunza Biblia pamoja nasi ingawa wanafurahia kusoma magazeti yetu. Kwa hiyo, tengenezo la Yehova limekuwa likiwatia moyo wahubiri waendelee kuwapelekea watu magazeti kwa ukawaida. Watu wanaposoma magazeti yetu kwa ukawaida, wanakuza tamaa ya Neno la Mungu. (1 Pet. 2:2) Mwishowe, huenda wakavutiwa na mambo fulani wanayosoma ambayo yatawafanya wakubali kujifunza Biblia.
2. Tunaweza kukuzaje upendezi wa watu tunaowapelekea magazeti kwa ukawaida?
2 ‘Tia Maji’ Mbegu za Kweli: Badala ya kumwachia magazeti mwenye nyumba na kuondoka, anzisha mazungumzo na ujaribu kujenga urafiki naye. Jambo hilo litakusaidia kuelewa hali, mapendezi na imani yake, na hivyo kukusaidia uzungumze naye kwa ufahamu. (Met. 16:23) Jitayarishe kwa ajili ya kila ziara. Ikiwezekana, eleza kwa kifupi jambo kuu na uzungumzie andiko kwenye magazeti linalozungumzia jambo hilo, ili kutia maji mbegu yoyote iliyo katika moyo wake. (1 Kor. 3:6) Andika tarehe ya kila ziara, gazeti, mada, na maandiko uliyozungumza naye.
3. Tunapaswa kuwarudia mara ngapi watu tunaowapelekea magazeti kwa ukawaida?
3 Tuwarudie Mara Ngapi? Unapaswa kurudi mara moja kwa mwezi ili kuwapelekea magazeti ya karibuni. Hata hivyo, ikitegemea hali yako na upendezi wa mtu huyo, unaweza kuamua kuwatembelea mara nyingi zaidi. Kwa mfano, juma moja au mawili baada ya kumwachia magazeti, unaweza kumrudia na kusema, “Nimekutembelea kifupi ili kukuonyesha jambo fulani kutoka kwenye magazeti niliyokuachia.” Jambo hilo litampa mtu huyo hamu ya kusoma makala hiyo. Ikiwa tayari ameisoma, unaweza kuuliza maoni yake kuhusu makala hiyo na kuizungumzia kifupi. Au ikiwa mtu huyo anafurahia kusoma machapisho yetu, unaweza kurudi na kumpa trakti, broshua, au kitabu tunachotoa mwezi huo.
4. Mara kwa mara tunaweza kufanya nini ili kutambua ikiwa wale tunaowapelekea magazeti kwa ukawaida wako tayari kujifunza Biblia?
4 Usisubiri mpaka mwenye nyumba aombe kujifunza Biblia. Chukua hatua ya kwanza. Hata ikiwa alikataa kujifunza Biblia wakati uliopita, mara kwa mara unaweza kumwonyesha makala “Majibu ya Maswali ya Biblia” iliyo kwenye Mnara wa Mlinzi ili kuona kama yuko tayari kuizungumzia pamoja nawe. Labda unaweza kuanzisha funzo la Biblia mlangoni. Hata hivyo, ikiwa hautafaulu kuanzisha funzo, unaweza kuendelea kumpelekea magazeti ili kukuza upendezi wake.