Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/93 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Ajili Ya Agosti

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Ajili Ya Agosti
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Agosti 2
  • Juma Linaloanza Agosti 9
  • Juma Linaloanza Agosti 16
  • Juma Linaloanza Agosti 23
  • Juma Linaloanza Agosti 30
Huduma Yetu ya Ufalme—1993
km 8/93 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Ajili Ya Agosti

Juma Linaloanza Agosti 2

Wimbo 63

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Zungumzia mambo ya kuongea kutoka kwenye magazeti ya karibuni. Tia moyo wote washiriki katika utumishi wa shambani mwisho-juma huu.

Dak. 17: “Jitahidi Kufanya Watu Wasikilize kwa Uangalifu.” Zungumza pamoja na wasikilizaji. Kazia umuhimu wa kumwona mwenye nyumba kuwa mtu, ukiwa na nia ya kuwa na mazungumzo pamoja naye. Uwe na maonyesho mafupi yakitegemea madokezo kwenye mafungu 2 na 3. Kazia utumiaji wa kawaida wa magazeti katika utumishi wa shambani.

Dak. 18: Kuongoza Funzo la Kitabu la Kutaniko katika kitabu Mtu Mkuu Zaidi. Kiongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko atumia kikundi cha wahubiri wanne au watano kuonyesha kutaniko jinsi funzo lapaswa kuongozwa. Wonyesho huu wapaswa kufanywa vizuri na kuongozwa kulingana na maagizo yaliyo kwenye Huduma ya Ufalme Yetu ya Julai. Tumia sura ya 11 ya kitabu Mtu Mkuu Zaidi. Onyesha jinsi maandiko marefu yanavyoweza kugawanywa ili kuruhusu kuwa na wasomaji zaidi ya mmoja au kugusia mambo makuu kama hakuna wakati wa kusoma fungu nzima. Kiongozi anaweza kutoa maelezo mafupi ya mara kwa mara kwa wasikilizaji kuonyesha njia inayotumiwa. Kila mtu katika wasikilizaji anapaswa kufuatana na nakala ya kitabu chake mwenyewe.

Wimbo 193 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 9

Wimbo 70

Dak. 10: Matangazo ya kwenu, kutia ndani ripoti ya hesabu na shukrani za upaji wa hiari. Pongeza kutaniko kwa ajili ya utegemezaji wa kifedha wa kutaniko la kwenu na pia ule wa kazi ya ulimwenguni pote ya Sosaiti.

Dak. 15: “Kutoa Ushahidi kwa Simu—Njia ya Kufikia Wengi.” Ipitiwe kwa maswali na majibu. Katika sehemu ambazo mawasiliano ya simu hayapo, tafadhali pitieni mambo makuu ya programu ya karibuni ya siku ya kusanyiko la pekee au kusanyiko la mzunguko.

Dak. 20: “Rudi Usitawishe Kupendezwa Katika Ujumbe wa Ufalme.” Ipitiwe kwa maswali na majibu. Uwe na wonyesho moja wa ziara ya kurudia ukitegemea utoaji ulioonyeshwa kwenye mafungu 2 na 4

Wimbo 71 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 16

Wimbo 20

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Mazungumzo ya makala “Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee.” Tia moyo wote kufanya mipango ya mapema ya kuhudhuria programu ya siku ya kusanyiko la pekee wakati wa mwaka wa utumishi wa 1994. Tangaza tarehe na mahali ikiwa inajulikana. Pia tia moyo kushiriki katika utendaji wa mwisho-juma.

Dak. 10: Matokeo ya kampeni ya Makedonia. Onyesha yaliyotimizwa na yanayobaki kutimizwa. Tia moyo wote washiriki katika utendaji uliobaki. Panga kuwe na jambo lililoonwa moja au mawili.

Dak. 20: “Matakwa kwa Mhudumu Mpya na Pia Yule Aliye na Ujuzi.” Ipitiwe kwa maswali na majibu na mzee. Malizia na muhtasari wenye uchangamfu lakini ulio mfupi unaotumika kwa mahitaji ya kutaniko la kwenu.

Wimbo 6 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 23

Wimbo 148

Dak. 10: Matangazo ya kwenu.

Dak. 20: “Tafuta Mafunzo ya Biblia kwa Bidii.” Makala ipitiwe kwa maswali na majibu na mwangalizi wa utumishi. Soma na kutumia maandiko yote yaliyowekwa bila manukuu. Pitia maendeleo ya kazi ya mafunzo ya Biblia ya kutaniko tangu miaka mitano iliyopita, na utokeze maelezo ya kumalizia kulingana na mahitaji ya kutaniko.

Dak. 15: Umuhimu wa Tarehe katika Funzo Letu la Biblia. Baada ya hotuba fupi ya habari chini ya “Fasili” kwenye ukurasa 306 wa kitabu Kutoa Sababu, ongoza mazungumzo na wasikilizaji ya habari iliyobaki chini ya “Tarehe.” Shughulikia “Kwa nini Mashahidi wa Yehova husema kwamba Ufalme wa Mungu ulisimamishwa katika 1914?” Onyesha jinsi habari hii husaidia wapya wawe tayari kutetea ujumbe wa Ufalme.

Wimbo 43 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 30

Wimbo 156

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Pia zungumza na wasikilizaji juu ya “Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko.”

Dak. 15 “Uwe Mwenye Nafsi Yote Katika Utumishi Wako.” Hotuba ikitolewa na mzee. Unapozungumzia fungu la 2, toa maelezo yanayofaa ya rejezo la Mnara wa Mlinzi. Soma na utumie Malaki 3:10 kwa kumalizia.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu. Waweza kuzungumzia kitia moyo kilichotolewa na ziara ya mwangalizi wa mzunguko. Kumbusha akina ndugu waangalie kwamba ripoti zote za mwaka wa utumishi wa 1993 zimetolewa.

Wimbo 31 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki