Matangazo
◼ Fasihi itakayotumiwa wakati wa Agosti: Yoyote ya broshua zifuatazo zaweza kutumiwa: Je! Kweli Mungu Anatujali?, Furahia Milele Maisha Duniani!, “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya,” Je! Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, au Serikali Itakayoleta Paradiso. Septemba: Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Oktoba: Maandikisho ya Amkeni! au Mnara wa Mlinzi, au nakala moja-moja za magazeti. Kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu chaweza kutolewa ikifaa. Novemba: New World Translation of the Holy Scriptures na kitabu Biblia—Neno la Mungu au Binadamu? TAARIFA: Makutaniko ambayo bado hayajaagiza vifaa vya kampeni vilivyotajwa juu yapaswa yaviagize kwenye Fomu ya Agizo la Vitabu (S-14-SW) la kila mwezi litakalofuata. Tafadhali agizeni magazeti kwa ajili ya ugawanyaji wa Oktoba.
◼ Makutaniko yapaswa kuanza kuagiza kalenda ya 1994 pamoja na ombi la fasihi zao za Septemba. Kalenda zitapatikana katika Kiingereza, Kifaransa.
◼ Kila kutaniko litapokea fomu tatu za Orodha ya Vitabu (S-18-SW). Mwandishi wa kutaniko anapaswa kukutana na mtumishi wa vitabu mapema katika Agosti na kuweka tarehe ya kuhesabu fasihi zote zilizo akibani za kutaniko mwishoni mwa mwezi. Hesabu kamili yapaswa kufanywa ya fasihi zote zilizo akibani, na jumla zapaswa kuingizwa kwenye fomu ya Orodha ya Vitabu. Jumla ya hesabu ya magazeti yaliyopo yaweza kupatikana kutoka kwa mtumishi wa magazeti. Tafadhali pelekeni ile ya kwanza kwa Sosaiti si baada ya Septemba 6. Wekeni nakala ya kaboni kwa ajili ya faili yenu. Nakala ya tatu yaweza kuwa ya kufanyia kazi. Kazi hiyo ya orodha yapaswa kusimamiwa na mwandishi, na fomu iliyokamilika ichunguzwe na kutiwa sahihi na mwangalizi msimamizi.
◼ Ugavi wa kutosha wa fomu za kutumia wakati wa mwaka wa utumishi wa 1994 zinapelekwa kwa kila kutaniko. Fomu hizi hazipaswi kutumiwa vibaya. Zapaswa kutumiwa tu kwa kusudi lazo.
◼ Kila mtu anayeshirikiana na kutaniko apaswa kupeleka maandikisho yote mapya na ya kufanywa upya tena ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, kutia ndani maandikisho yao ya kibinafsi, kupitia kutaniko.
◼ Sosaiti haijazi maombi ya fasihi ambayo yamefanywa na wahubiri mmoja-mmoja. Wale wanaotaka kifaa kilichotolewa wanaweza kumuuliza mtumishi wa fasihi, ambaye atatia ndani ya agizo la fasihi la kutaniko la kila mwezi. Mwangalizi msimamizi anapaswa kupanga kuwe na tangazo kila mwezi kabla ya agizo la fasihi la kila mwezi la kutaniko halijapelekwa kwa Sosaiti ili kwamba wale wote wanaopendezwa kupata vifaa vya fasihi vya kibinafsi waweze kumjulisha ndugu anayeshughulikia fasihi.
◼ Wahubiri ambao wanapanga kuanza utumishi wa upainia wa kawaida Septemba 1, 1993, wanapaswa kujaza maombi bila kuchelewa. Maombi yapaswa kupelekwa kwa Sosaiti kabla ya mwisho wa Agosti. Tafadhali rudieni mafungu 21 hadi 26 ya nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Septemba 1986.
◼ Mwandishi wa kutaniko atakusanya ripoti za utumishi kwa ajili kuingiza kwenye Fomu ya Mchanganuo wa Kundi (S-10-SW). Pia ataagiza kwa uangalifu mzee yeyote au mtumishi wa huduma ambaye anaweza kusaidia kukusanya ripoti. Hilo litahakikisha hesabu sahihi ya habari inayohitajika kutoka kwa kadi za Rekodi za Mhubiri za Kundi (S-21-SW). Fomu ya Mchanganuo wa Kundi (S-10-SW) yapasa kuwekwa kwenye faili kwa usahihi na unadhifu na iangaliwe vizuri na halmashauri ya utumishi.
◼ Vichapo Vipatikanavyo:
Kiingereza: Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli? Kifaransa: Watch Tower Publications Index 1950-1985; Sababu Kwa Nini Wewe Unaweza Kuitumaini Biblia (Trakti Na. 13); Mashahidi wa Yehova Wanaamini Nini? (Trakti Na. 14); Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani (Trakti Na. 15); Kuna Tumaini Gani kwa Wapendwa Waliokufa? (Trakti Na. 16). Kikuyu: Furahia Milele Maisha Duniani! Kiganda: “Habari Njema Hizi za Ufalme”; Furahia Milele Maisha Duniani!