Jitahidi Kufanya Watu Wasikilize kwa Uangalifu
1 Watu wengi tunaokuta katika huduma yetu ya nyumba kwa nyumba hawafikirii mambo ya kiroho. Huenda wakawa wamejawa na shughuli za washiriki wa familia, magumu ya kiuchumi, au matatizo ya kibinafsi. Ili kuanzisha mazungumzo, ni vema kwa kawaida kuzungumzia juu ya mambo yenye kupendeza yanayowapata wengi katika ujirani. Maswali yanaweza kutumiwa ili kuchochea kupendezwa, kwa kuwa hilo latia mwenye nyumba kwenye mazungumzo. Maswali ya maoni yasiyoaibisha watu ni yenye matokeo zaidi.
2 Wengi walikuwa na mafanikio mazuri mwezi uliopita kwa kufanya watu wasikilize kwa uangalifu kwa utoaji wa matoleo ya broshua. Tutarudia mifikio hiyo mwezi huu tena ili tuitumie katika kampeni yetu ya maeneo ya mbali na yasiyohubiriwa kwa ukawaida. Unaweza kusema:
◼ “Je! umetaka kujua: ‘Je! kweli Mungu anajali udhalimu na kuteseka kwa wanadamu?’” Ruhusu itikio. Soma Zaburi 72:12-14. Kisha fungua ukurasa 22 wa broshua Je! Kweli Mungu Anatujali? na uzungumzie vichwa vyenye herufi nzito katika sehemu ya 10, pamoja na maana ya kielezi kwenye ukurasa 23. Ikiwa broshua haikubaliwi, kwa nini usitoe trakti kama vile Faraja kwa Walioshuka Moyo au Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani?
3 Unapotoa broshua “Tazama!,” unaweza kutumia mfikio huu:
◼ “Tumekuwa tukizungumza na jirani zetu juu ya jambo linaloweza kufanywa ili kuhakikisha kwamba kutakuwako kazi na nyumba kwa kila mtu. Unasadiki kwamba ni jambo la akili kutazamia kwamba wanadamu watatimiza hili? [Ruhusu itikio la mwenye nyumba.] Kuna mtu anayejua jinsi ya kutatua matatizo hayo; angalia ahadi yake yenye uhakikisho kwenye Isaya 65:21-23. [Soma.] Muumba wetu alifanya ahadi hiyo iandikwe kwa ajili ya kitia moyo chetu, na sisi sote twahitaji hicho katika hizi nyakati ngumu, sivyo?”—rs-SW, uku. 11. Katika kutoa broshua “Tazama!”, kwa nini usionyeshe wazo la makao na kazi kwa wote limetolewa kielelezo kwenye jalada la mbele na nyuma la broshua hiyo? Unaweza kuifungua ili mwenye nyumba aone kielezi chote pamoja.
4 Mahali palipo na woga wa uhalifu katika ujirani unaweza kurudi kwenye utoaji huu:
◼ “Watu wengi wanajiuliza, ‘Ikiwa Mungu ni upendo, kwa nini anaruhusu uovu?’ Je! umewahi kujiuliza juu ya hilo pia?” Ruhusu elezo, kisha useme: “Ona kwamba Mithali 19:3 hutahadharisha dhidi ya kumlaumu Mungu kwa mambo mabaya ambayo watu hufanya.” Baada ya kusoma andiko hilo, elekeza uangalifu kwenye ukurasa 15 wa ile broshua “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya” na usome fungu la 27. Hilo laweza kuongoza kwenye mazungumzo ya mafungu yanayofuata.
5 Kumbuka kwamba kusudi letu ni kuamsha kupendezwa katika ujumbe wa Ufalme. Ili kufanya watu wasikilize kwa uangalifu, tunapaswa kuvuta uangalifu wa mwenye nyumba na kuchochea kufikiri kwake. Hilo litafanya watu walio mfano wa kondoo watake ‘kusikia atakayosema Mungu BWANA’ kuhusu kusudi lake kwa ainabinadamu.—Zab. 85:8.