Matangazo
◼ Fasihi ya kutumiwa wakati wa Septemba: Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Oktoba: Uandikishaji wa Amkeni! au Mnara wa Mlinzi au nakala moja-moja za magazeti hayo. Kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kumtafuta Mungu chaweza kutolewa inapofaa. Novemba: New World Translation of the Holy Scriptures na kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. TAARIFA: Makutaniko ambayo yatahitaji vifaa vya kampeni vilivyotajwa juu yapaswa yaviagize kwenye Fomu ya Agizo la Vitabu (S-14-SW) ya kila mwezi itakayofuata. Tafadhali agizeni magazeti ya ziada yenye kuhitajiwa kwa ajili ya ugawanyaji wa Oktoba.
◼ Mwangalizi msimamizi au mtu yeyote aliyewekwa naye apaswa kukagua hesabu ya kutaniko katika Septemba 1 au upesi iwezekanavyo baada ya hapo. Tangazieni kutaniko jambo hili lifanywapo.
◼ Wahubiri wanaopanga kufanya upainia msaidizi katika Oktoba wanapaswa kutoa maombi yao mapema. Hilo litaruhusu wazee kufanya mipango ya lazima kwa ajili ya fasihi na eneo.
◼ Wazee wanakumbushwa kufuatia maagizo yaliyotolewa kwenye kurasa 21-3 za Mnara wa Mlinzi la Aprili 15, 1991, kuhusu watu wowote waliotengwa na ushirika au waliojitenga na ushirika ambao huenda wana mwelekeo wa kurudi.
◼ Orodha ya Bei mpya imetayarishwa na nakala nne zinapelekwa kwenye kila kutaniko katika maeneo ambako bei zimerekebishwa. Zapaswa kugawanywa kwa mwandishi na ndugu wanaoshughulikia fasihi, magazeti, na hesabu.
◼ Sosaiti sasa inatokeza mabuku yaliyojalidiwa ya Kiingereza ya Mnara wa Mlinzi ya miaka ya 1970 hadi 1979 yakiwa ni vifaa vya daima. Yeyote anayependezwa kupata mabuku hayo yaliyojalidiwa anapaswa kuyaagiza kupitia kutaniko. Tafadhali kumbukeni kwamba mabuku yaliyojalidiwa ni bidhaa za kuagizwa kipekee.
◼ Akina ndugu watokao kwenye mizunguko inayohudhuria mikusanyiko ya wilaya katika Mombasa, Kisumu na Eldoret ambao wangependa kuhudhuria mkusanyiko wa pekee katika Nairobi wanakaribishwa kufanya hivyo. Hata hivyo, twapendekeza kwamba wale ambao huenda wakaja kutoka maeneo ya pwani na South Nyanza wahudhurie mkusanyiko wa pekee uliopangwa kwa ajili ya Desemba 23-26, 1993. Wale wanaotoka Magharibi mwa Kenya kutia Kisumu na Eldoret wanaweza kuhudhuria mkusanyiko wa pekee uliopangwa kwa ajili ya Januari 6-9, 1994. Nchi za nje zaweza kuhudhuria wowote watakaochagua kati ya mikusanyiko miwili ya pekee katika Nairobi.
◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:
Kiingereza kwa ajili ya Viziwi: Sababu Kwa Nini Wewe Unaweza Kuitumaini Biblia (Trakti Na. 13); Faraja kwa Walioshuka Moyo (Trakti Na. 20); Furahia Maisha ya Familia (Trakti Na. 21); Ni Nani Hasa Anayeutawala Ulimwengu? (Trakti Na. 22). Kirusi: Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani (Ndogo).
◼ Kaseti Mpya Zinazopatikana:
Kifaransa: Isaiah (seti ya kaseti nne).
◼ Kaseti Mpya za Video Zinazopatikana:
Kiarabu: Jehovah’s Witnesses—The Organization Behind the Name.