Jifunzeni Vitabu Kuishi Milele na Umoja Katika Ibada
1 Trakti, broshua, magazeti, na vitabu—vyote vyaweza kutumiwa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia nyumbani pamoja na watu wenye kupendezwa. Kwa sababu ya ugawanyaji wacho wenye kuenea na wenye kuvutia macho, kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi kimetumiwa kuanzisha mafunzo. Kwa hakika, kila mtu apaswa kutiwa moyo kukisoma na kujifunza, hasa kwa kujitayarisha na kuhudhuria Funzo la Kitabu la Kutaniko kwa ukawaida.
2 Hata hivyo, kuna vitabu viwili mahususi ambavyo vyapaswa kufunzwa watu wapya ili kuwasaidia waelewe mafundisho ya msingi ya Biblia pamoja na viwango vya kuishi vya Kikristo. Hivyo ni vitabu: Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani na Wenye Umoja Katika Ibada ya Mungu wa Pekee wa Kweli. Inapendekezwa kuwa upesi iwezekanavyo, wale wanaoongoza mafunzo ya Biblia katika vichapo vingine wabadili kuingia katika kimojapo vitabu hivyo. Ikiwa funzo lilikuwa linaongozwa katika kitabu Mtu Mkuu Zaidi, mtie moyo mwanafunzi aendelee kukisoma akiwa peke yake. Funzo la Biblia lapaswa kuendelea hadi vitabu Kuishi Milele na Umoja Katika Ibada vimalizwe, hata ingawa mtu aweza kubatizwa kabla kitabu cha pili hakijamalizwa. Utaratibu huu utampa mwanafunzi wa Biblia kiwango fulani cha kina na uthabiti wa kiroho.