Sanduku la Swali
● Kwa nini ni jambo la maana kumaliza kujifunza vitabu viwili kikamili pamoja na wanafunzi wapya hata ikiwa wanabatizwa kabla ya kitabu cha pili kumalizika?
Yehova anabariki tengenezo lake kwa mmiminiko wa wapya ambao wanamiminika katika makundi. Sisi twashangilia kuona mkusanyo huu mkubwa kuingia katika tengenezo. Hata hivyo, sisi twathamini kwamba watu hawa wenye mfano wa kondoo wahitaji usaidizi na mwelekezo wenye kuendelea katika kujifunza kumtumikia Yehova.
Wapya wahitaji msaada ili wapate maarifa sahihi ya kweli. (Kol. 1:9, 10) Sisi tuna pendeleo la kuwasaidia wapate uelewevu mzuri wa mafundisho ya msingi ya Biblia na ufahamu wa yale yanayofundishwa na Biblia kuhusu viwango vya maadili, maisha ya Kikristo, na mambo yanayohusiana na hayo. Hiyo itawasaidia wasimame imara katika kweli ili washinde mitihani yoyote inayoweza kuwa huko mbele.
Pia wanafunzi wahitaji kuwa na ukuzi kamili katika uwezo wao wa kufahamu. (1 Kor. 14:20) Maono yameonyesha kwamba ili kufikia kimo cha mtu aliyekomaa kabisa kiroho, funzo la kibinafsi likiongozwa na mwalimu ni lenye msaada. Hivyo, hata ingawa mtu huenda akabatizwa kabla ya kumaliza kujifunza vitabu viwili, hekima huonyesha kwamba funzo lake la Biblia la nyumbani lapasa kuendelea mpaka awe amemaliza kujifunza vitabu vyote viwili.
BAADA YA UBATIZO
Yesu alisema kwamba twapaswa kufanya wanafunzi—kuwabatiza na kuwafundisha. (Mt. 28:19, 20) Wanafunzi wanafundishwa mengi zaidi baada ya ubatizo. Maarifa ambayo mtu anaweza kupata kutoka kitabu kimoja kwa kawaida hayatoshi kukamilisha mazoezi yake ya kiroho. Mafundisho zaidi yahitajiwa ili afae kwa kazi ya huduma na kumtayarisha akinze mikazo ambayo huwajia wale wanaotumikia Yehova katika hizi siku za mwisho. Kushindwa kuandaa mazoezi ya kutosha huenda kukamwacha mwanafunzi akiwa hajatayarishwa kiroho ajisimamie mwenyewe. Baada ya mpya huyo kubatizwa, twaendelea kumsaidia afanye maendeleo zaidi awe amemaliza kujifunza vitabu viwili au la. Kichapo cha kwanza anachojifunza huandaa uelewevu juu ya mambo ya msingi. Kichapo cha pili huzungumzia sifa za Kikristo. Vichapo hivyo huenda vikawa kitabu Kuishi Milele kisha ama kitabu Wenye Umoja Katika Ibada au kitabu Amani ya Kweli. Ikiwa vitabu hivi havipatikani, vingine vilivyo na habari inayofanana na hiyo vyaweza kutumiwa. Kuendeleza funzo mpaka kitabu cha pili kiwe kimemalizwa huandaa elimu kamili katika makusudi ya Yehova pamoja na viwango vyake vya juu na matakwa ya Kikristo. Hiyo humsaidia huyo mpya aelewe maana ya kanuni za Kikristo na awe ameimarika katika imani. (Kol. 2:7) Ili kupata mambo zaidi na habari kuhusu kuripoti mafunzo kama hayo, ona Sanduku la Swali katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Novemba 1987.
Bila shaka, baada ya ubatizo wapya hao wapaswa kutarajiwa wafanye maendeleo ya kiroho. (Ebr. 6:1-3) Katika visa vilivyo vingi haichukui muda mrefu kumaliza kitabu cha pili. Mtu huyo mpya anaandaliwa hivyo msingi imara.