Sanduku La Swali
◼ Tunapaswa kujifunza kwa muda gani na mwanafunzi wa Biblia anayefanya maendeleo?
Inafaa kuendelea kujifunza pamoja na mwanafunzi wa Biblia anayefanya maendeleo mpaka atakapokuwa amemaliza kujifunza vitabu viwili, yaani, Biblia Inafundisha Nini Hasa? na “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu.” Tunapaswa kufanya hivyo, hata akibatizwa kabla ya kumaliza kujifunza vitabu vyote viwili. Baada ya mwanafunzi kubatizwa, tunaweza kuendelea kuripoti muda tunaotumia kujifunza naye, ziara za kurudia, na funzo. Iwapo mhubiri mwingine anaandamana nasi na kushiriki katika funzo, yeye pia anaweza kuripoti muda anaotumia.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme, Machi 2009, ukurasa wa 2.
Ni muhimu kwa Wakristo wapya kuwa na msingi imara katika kweli kabla hatujaacha kujifunza nao. Ili wasimame imara watakapokabili majaribu, Wakristo wapya wanahitaji ‘kutia mizizi’ katika Kristo na “kuimarishwa katika imani.” (Kol. 2:6, 7; 2 Tim. 3:12; 1 Pet. 5:8, 9) Zaidi ya hayo, ili kuwafundisha wengine ifaavyo, ni lazima wao wenyewe wawe na “ujuzi sahihi wa kweli.” (1 Tim. 2:4) Kwa kujifunza vitabu viwili pamoja na wanafunzi, tunawasaidia kuwa imara wanapotembea kwenye “barabara inayoongoza kwenye uzima.”—Mt. 7:14.
Kabla ya kumkubali mhubiri kubatizwa, wazee wanapaswa kuhakikisha kwamba anaelewa kabisa mafundisho ya msingi ya Biblia na anaishi kupatana nayo. Wazee wanapaswa kuwa waangalifu hasa wakati mwanafunzi ambaye hajamaliza kitabu cha kwanza anapotaka kubatizwa. Iwapo wazee wataona kwamba mhubiri hastahili kubatizwa, watahakikisha kwamba atapata msaada anaohitaji ili astahili kubatizwa baadaye.—Ona kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova, ukurasa wa 217-218.
[Blabu katika ukurasa wa 2]
Ni muhimu kwa Wakristo wapya kuwa na msingi imara katika kweli