Wasaidie “Waimarishwe Katika Imani”
Inapendeza kuona jinsi Yehova anavyobariki kazi ya kukusanywa kwa watu wake hivi kwamba zaidi ya watu robo milioni hubatizwa kila mwaka. (Kum. 28:2) Punde tu mhubiri anapomsaidia mwanafunzi kufikia ubatizo, huenda mwelekeo ukawa ni kuacha kujifunza naye na kukazia fikira kuwasaidia wengine. Mwanafunzi pia anaweza kuwa na mwelekeo wa kuacha kujifunza ili atumie muda wake mwingi katika utumishi. Hata hivyo, ni muhimu wanafunzi wa Biblia wawe na msingi mzuri katika kweli. Wanapaswa ‘kutia mizizi’ katika Kristo na “kuimarishwa katika imani.” (Kol. 2:6, 7; 2 Tim. 3:12) Kwa hiyo, baada ya mwanafunzi kubatizwa, anapaswa kuendelea na funzo lake la Biblia mpaka amalize vitabu vyote viwili yaani Biblia Inafundisha na “Upendo wa Mungu”.—Ona Huduma ya Ufalme ya Aprili 2011 ukurasa wa 2.