Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Desemba 30, 2013. Tarehe ya kuzungumzia kila sehemu imeonyeshwa ili wahubiri waweze kufanya utafiti wakati wanapojitayarisha kwa ajili ya shule kila juma.
1. Ni nini kitakachotusaidia kuwa wapole tunaposhughulika na wenye mamlaka serikalini? (Tito 3:2) [Nov. 4, w03 4/1 uku. 25 fu. 18-19]
2. Tunajifunza nini kutokana na maneno ya Paulo kwa Filemoni yanayopatikana katika andiko la Filemoni 4, 5, na 7? [Nov. 4, w08 10/15 uku. 31 fu. 1, 2; w92 4/15 uku. 25 fu. 2]
3. Tunaingiaje katika pumziko la Mungu? (Ebr. 4:9-11) [Nov. 11, w11 7/15 uku. 28 fu. 16, 17]
4. Tunaweza kujifunza nini kutokana na Samweli na waamuzi waaminifu na manabii ambao walitenda “uadilifu”? (Ebr. 11:32, 33) [Nov. 18, w11 1/1 uku. 25 fu. 5-uku. 26 fu. 1]
5. Kwa nini Yakobo aliandika kwamba “hekima inayotoka juu kwanza kabisa ni safi kiadili, kisha yenye kufanya amani”? (Yak. 3:17) [Nov. 25, w11 8/15 uku. 30-31 fu. 15]
6. Ni nani “wafu” ambao ‘walitangaziwa habari njema’? (1 Pet. 4:6) [Des. 2, w08 11/15 uku. 21 fu. 7]
7. Kulingana na andiko la 1 Yohana 2:7, 8, ni amri gani ambayo Yohana anasema ni ya “zamani” na pia ni “mpya”? [Des. 9,w08 12/15 uku. 27 fu. 6
8. Majina ya cheo “Alfa na Omega” na “wa Kwanza na wa Mwisho” yanamhusu nani? (Ufu. 1:8, 17) [Des. 16, w09 1/15 uku. 30 fu. 6]
9. Wakristo watiwa-mafuta ‘wanatiwa muhuri’ katika njia zipi mbili? (Ufu. 7:3) [Des. 23, w07 1/1 uku. 31 fu. 1]
10. Kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kabisa kwamba baraka zilizoahidiwa na Ufalme wa Mungu zitatimia, na kujua jambo hilo kunapaswa kutuathirije? (Ufu. 21:5, 6) [Des. 30, re uku. 304 fu. 9]