Habari Za Kitheokrasi
Argentina: Katika Mei, Argentina ilikuwa nchi ya 13 kupitisha kiwango cha wahubiri 100,000. Kilele chayo cha 29 mfululizo kilikuwa 100,024.
Kolombia: Kukiwa na 58,589 walioripoti katika Mei, Kolombia ilifikia kilele chayo cha tano mfululizo katika wahubiri.
Madagaska: Kiwango cha 5,000 kilipitwa katika Mei kukiwa na wahubiri 5,013 walioripoti.
Rwanda: Katika mwezi wa Juni, Rwanda ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 2,057 kukiwa na wastani wa saa zaidi ya 30 na mafunzo ya Biblia 2.7 kwa kila mhubiri!