Habari za Kitheokrasi
◆ Kwenye “Haki ya Kimungu” Mikusanyiko ya Wilaya 133 iliyofanywa katika eneo la tawi la United States, kulikuwa na kilele cha wahudhuriaji 1,366,700 na 18,011 wakabatizwa.
◆ Samoa ya Amerika ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 155 katika Juni, ongezeko la asilimia 35.
◆ Antigua ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 238 katika Juni.
◆ Mikusanyiko ya wilaya mitatu katika Bahamas ilihudhuriwa na 2,448, na 48 wakabatizwa.
◆ Saiprasi iliripoti kilele chao cha sita mfululizo, 1,213 wakiripoti katika Juni.
◆ Jamhuri ya Muungano ya Dominika ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 11,605 katika Juni, ongezeko la asilimia 10. Pia walikuwa na kilele kipya cha mafunzo ya Biblia 22,096.
◆ Fiji ilikuwa na kilele chao cha 54 mfululizo, wahubiri 1,454 wakiripoti katika Juni. Mafunzo yao ya Biblia yaliongezeka kufikia 2,403, kilele cha 25 mfululizo.
◆ Tahiti ilikuwa na ongezeko la asilimia 18 katika Juni, ikifikia wahubiri 1,005, kilele chao cha 20 mfululizo.
◆ Vanuatu ilikuwa na kilele cha wahubiri 113 katika Juni, ongezeko la asilimia 35.
◆ Samoa ya Magharibi ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 198 katika Juni, ongezeko la asilimia 24.