Kutangaza Habari Njema-Kwa Kusaidiana Kuanzisha Mafunzo ya Biblia
1 Wote wanaompenda Yehova wanataka kuwa wenye matokeo katika huduma yao. Yesu alitupa utume “mkafanye wanafunzi . . . , kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru.” (Mt. 28:19, 20, NW) Ukiwa na tamaa ya kuanzisha funzo la Biblia, tafuta mwongozo wa Yehova na tumia msaada wenye mafaa na madokezo yanayoandaliwa kupitia kundi.—Mt. 7:7, 8.
2 Kiongozi wa Funzo la Kitabu la Kundi lenu anapendezwa kipekee na kazi ya funzo la Biblia katika kikundi chenu. Mfikie na umweleze tamaa yako ya kutaka kuongoza funzo la Biblia. Huenda akaweza kupanga ili mhubiri mwenye ujuzi afanye kazi pamoja nawe kwa muda fulani. Kusudi linapasa kuwa (1) kukuwezesha uanzishe kisha uongoze funzo la Biblia lenye maendeleo na (2) kuanzisha mafunzo mengine wakati ujao.
JIFUNZE KWA KIELELEZO
3 Katika visa vingi, huenda ikawa hatuna funzo la Biblia kwa sababu haturudii upesi vya kutosha tunapoangusha kichapo au mahali ambapo kupendezwa kunaonyeshwa. Kwa hivyo, hakikisha unarudia upesi iwezekanavyo. Bila shaka, utahitaji kutunza maandishi mazuri kuhusu kupendezwa huko. Labda mhubiri anayekusaidia anaweza kukuonyesha jinsi jambo hilo linavyofanywa. Nyinyi wawili mkiwa pamoja mtataka kujitayarisha kwa ajili ya kufanya ziara hizo za kurudia mkiwa na kusudi la kuanzisha mafunzo ya Biblia. Vipindi vya kufanya mazoezi vitawapa maoni mazuri kuhusu jinsi ya kuamsha tena kupendezwa huko mnaporudia.
4 Angalia yale ambayo mwandamani wako anafanya anapoongoza kwenye ziara fulani. Angalia jinsi anavyomhusisha mwenye nyumba katika mazungumzo. Jiulize jinsi unavyoweza kufanya hivyo. Je! anamfanya mwenye nyumba atoe maoni yake kwa kumwuliza maswali ya kuongoza au kwa kumwuliza atoe elezo kuhusu andiko linalofaa? Baada ya ziara, pitia yale ambayo umejifunza. Kisha jitahidi kutumia haya katika ziara za kurudia za wakati ujao.
5 Mara funzo la Biblia likiisha anzishwa, pangeni njia ambazo nyinyi wawili mnaweza kuzishiriki. Mnaweza kusoma maandiko ya msingi yaliyochaguliwa na kumsaidia mwenye nyumba ayaelewe. Baada ya kuacha funzo, mwombe mwenzako madokezo yenye msaada, kama vile ni wakati gani wa kuuliza maswali ya ziada, jinsi ya kuamsha hamu ya mwanafunzi kwa funzo la wakati ujao, na jinsi ya kuelekeza kupendezwa katika tengenezo.
MAREKEBISHO YA ENEO YANAPOTOKEA
6 Makundi mapya yanapoanzishwa au kunapokuwa marekebisho ya eneo, huenda kukawa na uhitaji wa kumpa mhubiri mwingine funzo la Biblia ambalo umeanzisha. Unaweza kupanga ili mhubiri anayestahili kutoka kundi lingine aende pamoja nawe kwenye funzo hilo. Baada ya majuma machache kupita, mhubiri huyo anaweza kuanza kuliongoza. Kutambua kwamba kupokeza mwingine funzo ni sehemu nyingine tu ya kazi ya kufanya wanafunzi kutakusukuma kufanya lililo bora zaidi kwa mwanafunzi.—Flp. 2:4.
7 Kweli kweli Yehova anatimiza ahadi yake ya ‘kutikisa mataifa yote’ na anajaza nyumba yake na vitu vyenye kutamanika. (Hag. 2:7, NW) Lo, tuna pendeleo la ajabu kama nini la kuwasaidia wengine wajue na kumpenda Yehova! Kwa kusaidiana kupitia mpango wa Funzo la Kitabu la Kundi, huenda ikawa kwamba wengi wetu watakuwa na furaha ya kuongoza funzo la Biblia la nyumbani la ukawaida.