Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/98 kur. 3-4
  • Mafunzo Zaidi ya Biblia Yanatakwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mafunzo Zaidi ya Biblia Yanatakwa
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari Zinazolingana
  • Jipe Ujasiri wa Kufanya Ziara za Kurudia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Ziara za Kurudia Huongoza Kwenye Mafunzo ya Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Je! Wewe Unafanya Ziara za Kurudia Zako?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Hakikisha Kwamba Unarudia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 4/98 kur. 3-4

Mafunzo Zaidi ya Biblia Yanatakwa

1 Yehova Mungu analibariki tengenezo lake la kidunia kwa ukuzi wenye kuendelea. Mwaka wa utumishi uliopita, watu 375,923 walibatizwa ulimwenguni pote, ukiwa wastani wa wanafunzi wapya 1,000 kila siku, au kati ya karibu 43 kila saa! Ijapokuwa miongo kadhaa ya magumu ambayo huenda ikawa ndugu zetu waliyakabili katika sehemu mbalimbali za ulimwengu, kazi ya Ufalme inasitawi na maongezeko yenye kutokeza yanaonwa. Inasisimua kusoma juu ya kusonga mbele kunakofanywa katika kueneza habari njema!

2 Katika ofisi yetu ya tawi mwaka wa utumishi uliopita, sisi pia tuliona maongezeko katika jumla ya wastani wa wahubiri na mapainia-wasaidizi, katika saa zilizotumiwa kuhubiri, na katika idadi ya vijitabu, broshua, na magazeti yaliyoangushwa. Kulikuwa na ongezeko katika idadi ya waliobatizwa na kilele cha wakati wote katika hudhurio la Ukumbusho. Je, vipi utendaji wa kufanya ziara za kurudia na mafunzo ya Biblia? Katika nchi nyingi zilizo chini ya ofisi yetu ya tawi, wastani wa ziara za kurudia na mafunzo ya Biblia kwa mhubiri umeshuka. (Linganisha ripoti za Agosti 1996 na Agosti 1997 ili kutoa kielezi, ukitumia wastani ulioonyeshwa katika Huduma ya Ufalme Yetu.) Hizi sehemu za huduma ndizo za muhimu katika kufanya wanafunzi. Kila mmoja wetu aweza kufanya nini ili kurekebisha mwelekeo huu wa kushuka huku katika ziara za kurudia na mafunzo ya Biblia?

3 Imarisha Tamaa ya Kuongoza Funzo: Sisi wenyewe twahitaji kukazia kuwa wenye nguvu kiroho na watendaji. Wafuasi wa kweli wa Kristo ni “wenye bidii kwa kazi zilizo bora.” (Tito 2:14) Tunapopitia huduma yetu, je, twaweza kusema kwamba tuna hamu nyingi sana ya kufuatia maangusho yote ya fasihi zote tulizoangusha shambani? Je, tuna shauku ya kuwatolea mafunzo ya Biblia nyumbani wote wanaoonyesha kupendezwa? (Rom. 12:11) Au twahitaji kusitawisha tamaa nyingi ya kufanya ziara za kurudia na kuanzisha mafunzo ya Biblia nyumbani?

4 Kusoma Biblia kibinafsi, kuhudhuria mikutano kwa ukawaida, na kujifunza vichapo kutatuweka hai kiroho na kuimarishwa na roho ya Mungu. (Efe. 3:16-19) Kufanya hivyo kutaimarisha imani na uhakika wetu katika Yehova na upendo wetu kwa binadamu mwenzetu. Tutachochewa kufundisha mtu mwingine kweli, kwa njia hiyo tukifanya huduma yetu ipendeze, iwe yenye mafanikio, na yenye kusisimua. Naam, twapaswa tutake mafunzo ya Biblia mengi!

5 Jifunze na Familia Kwanza: Wazazi Wakristo walio na watoto wanaoishi nyumbani wapaswa kuhangaikia programu ya funzo la Biblia la familia lenye kufanywa kwa ukawaida. (Kum. 31:12; Zab. 148:12, 13; Mit. 22:6) Ingefaa zaidi wazazi wajifunze broshua Anataka, kisha kitabu Ujuzi pamoja na watoto wao ili kuwatayarisha wastahili kuwa wahubiri wasiobatizwa na kujiweka wakfu na kubatizwa. Bila shaka, habari ya ziada yaweza kuchunguzwa, ikitegemea uhitaji na umri wa mtoto. Mzazi ajifunzaye na mtoto asiyebatizwa anaweza kuhesabu hilo funzo, saa, na ziara za kurudia, kama ilivyoonyeshwa katika Sanduku la Swali la Huduma ya Ufalme Yetu ya Aprili 1987.

6 Boresha Mpango Mzuri wa Kibinafsi: Kwa kufikiria idadi ya magazeti, broshua, na vitabu vilivyoangushwa, hapana shaka kwamba kiwango kikubwa cha mbegu kimetawanywa. Mbegu hizi za kweli ambazo zimepandwa zina uwezekano mkubwa wa kutokeza wanafunzi wapya. Lakini je, mkulima au mtunza-bustani angetosheka ikiwa angeendelea kupanda, na baada ya jitihada zake zote, akose wakati wa kuvuna? Sivyo hata kidogo. Vivyo hivyo, kufuatia kupendezwa katika huduma ni kwa lazima.

7 Je, wewe hupanga ratiba ya wakati ili kufanya ziara za kurudia? Warudie bila kukawia watu wote waliopendezwa. Fanya ziara za kurudia ukiwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia. Je, wewe huweka maandishi ya wakati ufaao na yaliyopangwa vizuri, ya ziara zako za kurudia? Hakikisha unaandika tarehe ya ziara ya kwanza, pamoja na jina na anwani ya mwenye nyumba, maangusho yoyote, ufafanuzi mfupi wa kile mlichozungumzia, na jambo liwezalo kuzungumzwa kwenye ziara inayofuata. Katika maandishi yako, acha nafasi ya habari ya ziada itakayoongezwa baada ya kila ziara ya kurudia.

8 Changanua Jinsi ya Kufanya Ziara ya Kurudia: Ni baadhi ya mambo gani ya kukumbukwa unapofanya ziara ya kurudia kwa mtu anayependezwa? (1) Uwe mchangamfu, mwenye urafiki, mwenye shauku, na wa hali ya kawaida. (2) Zungumzia mambo au maswali yanayompendeza. (3) Fanya mazungumzo yawe sahili na ya Kimaandiko. (4) Katika kila moja ya ziara za kurudia, jitahidi kufundisha mwenye nyumba jambo ambalo atalitambua kuwa lenye thamani ya kibinafsi kwake. (5) Jenga hamu ya kutazamia habari itakayozungumziwa katika ziara ya kurudia itakayofuata. (6) Usikae kwa muda mrefu. (7) Usiulize maswali yanayomwaibisha mwenye nyumba au yanayomtatanisha. (8) Tumia ufahamu ili usihukumu maoni mabaya au mazoea mabaya ya mwenye nyumba kabla hajasitawisha uthamini wa kiroho.—Ona nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Machi 1997 ili kupata msaada zaidi wa jinsi ya kufanikiwa katika kufanya ziara za kurudia na kuanzisha mafunzo ya Biblia.

9 Vumbua Uwezekano Wote: Katika kutaniko moja, iliwezekana kupata majina na namba za vyumba vya wapangaji katika jengo la nyumba lenye ulinzi mkali. Kila mkazi aliandikiwa barua ya kibinafsi, na trakti mbili zikawekwa ndani yake. Mwishoni mwa barua, funzo la Biblia nyumbani lilitajwa na namba ya simu ilitiwa ndani ili mwenye kuipokea aijibu. Baada ya siku chache, mwanamume asiye na umri mkubwa alipiga simu akiomba funzo. Ziara ya kurudia ilifanywa siku iliyofuata, na funzo likaanzishwa katika kitabu Ujuzi. Usiku huohuo alihudhuria Funzo la Kitabu la Kutaniko, akaendelea kuhudhuria mikutano. Mara, akaanza kusoma Biblia kila siku kwa ukawaida na kufanya maendeleo imara kuelekea ubatizo.

10 Wahubiri katika kikundi kimoja cha gari walipanga kufanya ziara za kurudia pamoja. Dada mmoja alipofanya mojawapo ya ziara zake, mtu aliyekuwa akimtafuta hakuwako nyumbani, lakini mwanamke mwingine asiye na umri mkubwa alijibu mlangoni, akisema: “Nimekuwa nikiwangoja.” Huyo mwenye nyumba alikuwa amepokea kitabu Ujuzi mapema kutoka kwa mtu anayejuana naye. Kufikia wakati huo dada alipokuwa anafika mlangoni pake, alikuwa amekisoma kitabu chote mara mbili naye alipendezwa sana na habari iliyokuwamo. Alisema hakuwa ameshangaa kuona Mashahidi wakimrudia siku hiyo kwa sababu alikuwa amesali waje kujifunza Biblia naye. Funzo lilianzishwa, alianza kuhudhuria mikutano ya kutaniko, na alifanya maendeleo ya haraka.

11 Dada aliyebatizwa kwa miaka karibu 25, hivi majuzi alimpa mama yake kitabu Ujuzi. Mama yake, akiwa mshiriki wa kanisa, alianza kusoma hicho kitabu. Baada ya kumaliza sura mbili, alimpigia binti yake simu, ambaye alishangaa mama yake aliposema: “Nataka kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova!” Huyo mama alianza kujifunza na sasa amebatizwa.

12 Jaribu Madokezo Haya: Je, umepata kutumia mfikio wa moja kwa moja kuanzisha mafunzo? Waweza tu kusema hivi: “Ikiwa ungependa kuwa na funzo la Biblia nyumbani bila malipo, naweza kukuonyesha kwa dakika chache tu jinsi linavyofanywa. Ukilifurahia, waweza kuendelea.” Watu wengi hawasiti kukubali toleo hilo, nao kwa utayari huchunguza wonyesho wa funzo la Biblia.

13 Mapema mwa funzo, mwonyeshe mwanafunzi jinsi ya kutayarisha kimbele kwa kusoma maandiko yaliyotajwa na kutia alama maneno makuu yanayojibu maswali yaliyochapishwa. Kazia mambo makuu pekee. Ijapokuwa huenda tukahitaji kuwa wenye kubadilikana katika vipindi vichache vya kwanza, ni jambo la maana funzo la Biblia liongozwe kwa ukawaida. Fikiria jinsi utakavyoanzisha sala ikiwa sehemu muhimu ya funzo na jinsi utakavyomtayarisha mwanafunzi Kimaandiko kwa ajili ya upinzani. Kwa vyovyote, fanya funzo lako liwe lenye kupendeza!

14 Bila shaka, wanafunzi wote wa Biblia hawafanyi maendeleo kwa kiwango kilekile. Baadhi yao si wenye mwelekeo wa kiroho kama wengine wala hawaelewi mambo haraka wanapofundishwa. Wengine huwa na maisha yenye shughuli nyingi sana nao huenda wasiweze kutoa wakati unaohitajiwa ili kumaliza sura nzima kila juma. Hivyo, katika visa fulani huenda ikawa lazima kuchukua zaidi ya kipindi kimoja cha funzo kukimaliza sura kadhaa na miezi ya ziada kumaliza kitabu. Katika visa fulani huenda tukajifunza broshua Anataka kwanza kisha tuendelee na kitabu Ujuzi. Hilo, pamoja na kuongezea kuhudhuria mikutano ya kutaniko, kutamsaidia kila mwanafunzi apate msingi imara katika kweli.

15 Zaidi ya yote, sali upate funzo la Biblia! (1 Yoh. 3:22) Mojawapo ya mambo yaliyoonwa yenye kuthawabisha kwa Mkristo ni kutumiwa na Yehova kusaidia mtu awe mwanafunzi wa Yesu Kristo. (Mdo. 20:35; 1 Kor. 3:6-9; 1 The. 2:8) Sasa ndio wakati wa kuonyesha bidii nyingi katika kazi ya kuongoza funzo la Biblia, tukiwa na uhakika wa kupata baraka nyingi za Yehova katika jitihada zetu za kuanzisha mafunzo zaidi!

[Blabu katika ukurasa wa 3]

Je, wewe unasali ili uanzishe funzo jipya la Biblia?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki