Habari Za Kitheokrasi
Mikusanyiko ya Wilaya: Tulimalizia mikusanyiko ya wilaya kwa mahudhurio mazuri yafuatayo:
Hesabu ya Hudhurio Waliobatizwa
Kenya: 22,115 630
Rwanda: 5,660 259
Tanzania: 11,733 337
Uganda: 3,196 125
Vikumbusha vizuri vilivyotolewa katika “Imani Katika Neno la Mungu” Mkusanyiko wa Wilaya vitatusaidia tudumu imara katika kweli.
Benin: Wahubiri 5,331 walitoa ripoti katika Novemba, na hicho kilikuwa kilele cha wahubiri cha 59 mfululizo.
India: Maendeleo bora katika kazi ya kuhubiri yalionekana katika Novemba wahubiri 18,077 walipotoa ripoti ya utumishi wa shambani. Hicho kilikuwa kilele cha 39 mfululizo.
Liberia: Kulikuwa na kilele kilichopita wakati wote cha wahubiri 2,120 walioripoti utumishi wa shambani katika Novemba.
Saiprasi: Ongezeko la asilimia 2 katika Novemba lilileta kilele kipya cha wahubiri 1,758. Pia kulikuwa na kilele kipya cha mapainia wa kawaida, 136 waliotoa ripoti.
Taiwan: Hesabu ya wastani ya wahubiri kufikia sasa, mwaka huu wa utumishi ni 3,516, na hiyo yaonyesha ongezeko la asilimia 6 kuliko mwaka jana.
Visiwa vya Solomon: Kilele kipya cha wahubiri kilifikiwa, wahubiri 1,393 wakiripoti katika Novemba.