Habari za Kitheokrasi
Majumba ya Ufalme yafuatayo yaliwekwa wakfu hivi majuzi: Katika Kenya, North Kinangop, 247 wakiwepo katika programu. Katika Tanzania, Ilonga kukiwa na hudhurio la 146 na Tengeru kulikuwa na 157. Katika Uganda, Jumba la Ufalme la Tororo 349 wakiwepo.
Jamhuri ya Afrika ya Kati: Utendaji wa utumishi wakati wa mwezi wa Oktoba ulikuwa wenye kutokeza, kukiwa na kilele kipya cha wahubiri 1,846. Programu za siku ya kusanyiko la pekee zilifanywa katika sehemu 19, kukiwa na hudhurio la 5,577 na 32 waliobatizwa.
Mexico: Katika Novemba, wahubiri 411,292 waliripoti. Hiki kilikuwa kilele kipya kingine.
Sri Lanka: Kulikuwa na wahubiri 1,873 walioripoti katika Novemba, ongezeko lenye kupendeza la asilimia 9.
Taiwan: Mbali na kilele cha wahubiri 2,523, ripoti ya Novemba ilionyesha kilele kipya cha ziara za kurudia 44,514 na mafunzo ya Biblia 4,234.
Visiwa vya Virgin (Marekani): Kilele kipya cha wahubiri 647 pamoja na jumla ya mafunzo ya Biblia 778 yalileta shangwe katika Novemba.