Watafute Wenye Kufundishika
1 “Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka.” (Yn. 6:44) Yehova achunguzaye moyo, atathawabisha wale wenye kufundishika nao watatenda kulingana na wanayofundishwa. (Yer. 17:10; Yn. 6:45) Tuna pendeleo la kuwa wafanyakazi wenzi katika kutafuta wapole wanaotamani ulimwengu mpya.—Zab. 37:11; 1 Kor. 3:9.
2 Yesu alifafanua wanafunzi wake kuwa “wavuvi wa watu.” (Mt. 4:19) Ijapokuwa aina hiyo ya kazi wakati mwingine yaweza kuchosha, kuna uradhi mwingi katika kupata matokeo mazuri. Badala ya kufanyia faida yetu wenyewe, kwa kweli tunaokoa “samaki” kutokana na uharibifu fulani. Mvuvi mwenye mafanikio apaswa kujua la kufanya ili kuvutia samaki. Vivyo hivyo, lazima tutoe ujumbe wa Ufalme kwa njia ivutiayo itakayoamsha kupendezwa kwa wasikilizaji. Jambo hili ni kweli hasa tunapofanya ziara za kurudia. Twaweza kusema nini?
3 Ikiwa kupendezwa kulionyeshwa katika makala za “Mnara wa Mlinzi” zinazoshughulikia sala, unaweza kusema:
◼ “Wakati uliopita tuliongea juu ya sala zinazosikiwa na Mungu. Kwa kuwa sisi sote twataka Mungu asikie sala zetu basi swali la asili lingekuwa, Ni mambo gani yanayofaa ya kutolea sala? Nina hakika wakubali kwamba kuna maoni mengi kuhusu swali hilo.” Ruhusu itikio. Kisha fungua ukurasa 278 katika kitabu Kutoa Sababu na ushiriki mawazo machache chini ya kichwa “Ni mambo gani yanayofaa ya kutolea sala?”
4 Ikiwa katika ziara iliyopita ulishughulikia habari kuhusu kuteseka kutoka kurasa 131-133 katika kitabu Kutoa Sababu waweza sasa kutumia habari iliyo chini ya ukurasa 133. Katika maelezo yako ya utangulizi mbona usitokeze swali linalofanyiza kichwa kidogo chini ya ukurasa huo? Ruhusu itikio. Kisha uendelee na mawazo ya kimaandiko chini ya kichwa hicho kidogo.
5 Ikiwa mwenye nyumba alionekana kuhangaikia hali za ulimwengu, unaweza kutaka kujaribu huu:
◼ “Kwa wazi wahisi kuhangaika kuhusu hali mbaya zinazotubidi kukabiliana nazo katika kuishi na katika kutunza familia zetu. Biblia hufunua ahadi nzuri ajabu atakayotimiza Mungu wakati ujao karibuni.” Soma Mithali 2:21, 22, na ueleze jinsi Yehova ameahidi ulimwengu wa amani ya kudumu.
6 Unapofanya ziara za kurudia baada ya kampeni ya pekee ya trakti Habari za Ufalme kuanza, tafadhali hakikisha umeacha nakala ya trakti Habari za Ufalme kwa wenye nyumba ambao hawana. Huenda utakayosema kwenye ziara za kurudia unapofuatia maangusho ya trakti Habari za Ufalme yatazungumziwa katika toleo la Huduma ya Ufalme Yetu ya Mei.
7 Kwa kuwa Neno la Mungu “lina nguvu,” twapaswa kujaribu kulitumia katika utoaji wetu. (Ebr. 4:12) Hakikisha unatia mwenye nyumba moyo ajisomee Biblia. (Linganisha Matendo 17:11.) Tukifanya sehemu yetu kwa bidii, Yehova atabariki jitihada zetu.