Kurudi Tukiwa na Kusudi la Kuanzisha Funzo la Biblia
1 Baada ya kumpata mtu mwenye kupendezwa kwenye ziara ya kwanza, ushahidi kamili unahitajiwa kwa upande wetu ili kuendeleza kupendezwa huko. Kufanya ziara za kurudia kwaweza kuongoza moja kwa moja kwenye mazungumzo ya Biblia na mafunzo ya Biblia yenye kuokoa uhai. Fikiria madokezo haya ya kufanya ziara za kurudia zenye matokeo.
Mwishoni mwa ziara ya kwanza, unaweza kuweka msingi wa ziara ya kurudia kwa kuuliza:
◼ “Je! umepata kujiuliza kwa nini kuna dini nyingi sana?” Baada ya kurudi unaweza kusema: “Mara ya mwisho nilipokuwa hapa, swali lilizuka juu ya kwa nini kuna dini nyingi sana. Kuna sababu kadhaa za hilo. Ningependa kusoma jambo la kupendeza nililopata nilipokuwa nikipitia swali hili.” Fungua ukurasa 67 wa kitabu Kutoa Sababu na usome sehemu iliyo chini ya kichwa kidogo “Kwa nini kuna dini nyingi sana?”
2 Je! Mungu aweza kupatikana katika dini zote? Ili Mungu awe katika dini fulani, ni lazima dini hiyo izae matunda yafaayo.
Ili kuanzisha ziara ya kurudia, ungeweza kuuliza:
◼ “Dini inapaswa iathirije mwenendo wa mtu? Yale ambayo Yesu alisema kwenye Mathayo 7:17-20 hutupa sisi miongozo ambayo dini ya kweli inatazamiwa kufuata.” Soma andiko hilo moja kwa moja kutoka mwisho wa fungu la 19 katika ukurasa wa 12 wa kitabu Mankind’s Search for God. Halafu uliza mwenye nyumba kile anachoona pichani katika ukurasa wa 13. “Ingawa mamilioni wanadai kumwamini Mungu, wengi wanamkana kwa matendo yao.” Halafu, soma sentensi mbili za kwanza za fungu la 20. “Matendo haya ya jeuri yanatambulisha dini ambazo hazifuati mwelekezo uliotolewa na Kristo wa kupendana sisi wenyewe, hata na adui zetu. Kwenye ziara yangu itakayofuata, labda tunaweza kuzungumzia yale ambayo lazima dini iwe inafanya ikiwa inazaa matunda mazuri.”
3 Wakati ujao una nini kwa wale wanaomtafuta Mungu wa kweli? Mazungumzo ya kutoka moja kwa moja kwenye kitabu Mankind’s Search for God juu ya swali hilo yaweza kuongoza kwenye funzo la Biblia.
Ili kuanzisha mazungumzo, huenda ukasema:
◼ “Kukiwa na hali za kiuchumi kama zilivyo sasa, watu wengi wanajiuliza kama wanaweza kuwa na maoni chanya juu ya wakati ujao. Nimeona Biblia kuwa yenye kutia moyo sana inapozungumzia wakati ujao. Acha nishiriki nawe ahadi ya Mungu katika Isaya 65:21, 22, 25. [Soma na ueleze kifupi juu ya andiko hilo.] Kitabu Mankind’s Search for God hujibu baadhi ya maswali ya kupendeza kuhusiana na hilo, kuanzia na fungu la 17 katika ukurasa 372.” Halafu onyesha mpango wa funzo la Biblia, ukitumia mafungu 17-20. “Juma lijalo ningependa tuzungumzie swali hili, Ni nini ulio msingi wa ulimwengu mpya ulioahidiwa katika Biblia?”
4 Tumieni kwa hekima wakati uliobaki ili kushiriki katika kutoa ushahidi kikamili kunakotolewa sasa katika mataifa yote ya dunia. (Linganisha Matendo 20:21.) Kufanya ziara za kurudia tukiwa na kusudi la kuanzisha funzo la Biblia kwaweza kumaanisha uhai wa milele kwa wale tunaohubiria.