Fanya Ziara za Kurudia Zenye Matokeo
1 Kufanya ziara za kurudia ni sehemu muhimu ya utumishi wetu tukiwa “wafanya kazi pamoja na Mungu.” (1 Kor. 3:6-9) Hakuna haja ya kukisia juu ya itikio la mwenye nyumba, kwa sababu tunarudia mtu ambaye tayari ameonyesha kupendezwa na kweli. Matayarisho mazuri kwa upande wetu yataonyesha kupendezwa kibinafsi kwa moyo mweupe kuelekea yule anayezuriwa tunapozungumzia kichwa fulani cha Biblia chenye kuvutia.
2 Sema mambo kihususa; uliza maswali yenye busara.
Kutokana na maandishi yako ya ziara ya kwanza, unaweza kuuliza:
◼ “Je! umefikiria zaidi kuhusu ahadi za Mungu za kutawala dunia kwa haki?”
Swali jingine laweza kuwa:
◼ “Je! unahisi kuwa sala yako kwamba Ufalme wa Mungu uje ina maana zaidi tangu mazungumzo yetu ya Biblia juma lililopita?”
Uso na namna ya sauti yenye urafiki husaidia sana katika kuonyesha kupendezwa kwetu kwa moyo mweupe tunapouliza maswali kama hayo.
3 Usiwe Mwenye Haraka; Sikiliza Yale Ambayo Mwenye Nyumba Anasema. Ikiwa tunasikiliza yale ambayo mwenye nyumba anasema na kufikiri kwa uzito kabla ya kujibu, kupendezwa kwetu naye kwa moyo mweupe akiwa mtu kutakuwa wazi. Ikitegemea yale anayosema, unaweza kutoa jambo la Kimaandiko linalohusiana na ziara yako ya kwanza. Uwe tayari kumfundisha mwenye nyumba jambo fulani kila mara unaporudi. Iwapo habari isiyotazamiwa inazuka, tumia fursa hiyo kutoa kitabu chako Kutoa Sababu ili kupata habari inayohitajika.
4 Ikiwa uliangusha “Mnara wa Mlinzi” la Aprili 1, 1992, unaweza kusema:
◼ “Wakati uliopita, tulizungumzia baraka ambazo uhuru katika ulimwengu mpya wa Mungu utaleta. Miongoni mwa baraka hizo ni uhakika wa kwamba kila mtu atakuwa na makao mazuri, chakula kingi, na kazi inayothawabisha, yenye amani. Hata hivyo, swali ambalo lapasa kutuhusu sisi sote ni, ‘Tunaweza kufanya nini ili tuwepo tuweze kufurahia baraka hizo?’ Ona yale ambayo Yesu alisema kwenye Yohana 17:3.” Baada ya kusoma na kuonyesha utumizi wa andiko hilo unaweza kutoa kitabu Kuishi Milele na uonyeshe jinsi kinavyoweza kumsaidia mtu aelewe mafundisho ya msingi ya Biblia.
5 Ikiwa uliangusha “Mnara wa Mlinzi” la Aprili 15, 1992, unaweza kusema:
◼ “Nilipokutembelea wakati uliopita, tulizungumza kuhusu uhakika wa kwamba Mungu husikia na pia hujibu sala. Hata hivyo, kusikizwa na Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu wote mzima ni pendeleo lenye thamani. Kwa sababu hiyo ni lazima tusikilize kwa uangalifu wakati Mungu, kupitia Neno lake, anapozungumza nasi kuhusu matakwa yake. Ona jinsi jambo hilo linavyotiliwa mkazo kwenye 1 Yohana 3:22.” Halafu unaweza kusoma na kutumia andiko hilo kama vile inavyoonyeshwa katika kitabu Kutoa Sababu kwenye ukurasa 277. Hata andiko kwenye Isaya 55:6, 7 laweza kutumiwa katika utoaji huu. Halafu unaweza kufungua sura ya 27 katika kitabu Kuishi Milele na usome au ufanye muhtasari wa mafungu ya kwanza, ukiuliza maswali ya mafungu hayo.
6 Acheni tuendelee kuonyesha kupendezwa kibinafsi na kuweka akilini vichwa vya Biblia vyenye kuvutia tunavyoweza kuzungumzia ili kwamba ziara zetu za kurudia ziwe na mafanikio.