Je, Wewe Huona Uhitaji?
1 Yehova aelezwa kuwa Msaidiaji na Kimbilio. Twajua twaweza kumwendea wakati wa uhitaji naye atatusaidia. (Zab. 18:2; 46:1) Twaweza kuiga sifa hii ya ufikirio kwa kujitolea kusaidia wengine tunapoona uhitaji.
2 Ni nini humhamasisha mtu afanye jitihada za pekee ili kusaidia mtu mwingine? Watu wengi hutambua hili kuwa jambo lenye upendo, jema kufanya. Kwa hakika Neno la Mungu hulitia moyo. (Rum. 15:1) Paulo alitusihi ‘tuangalie, si mambo yetu wenyewe, bali yale ya wengine.’—Flp. 2:4.
3 Hili ni jambo ambalo sote twaweza kupata shangwe katika kulifanya. (Mdo. 20:35) Paulo alimtaja kijana Timotheo kuwa kielelezo cha yule ‘atakayeiangalia kwelikweli hali’ ya ndugu zake. (Flp. 2:20) Ni vizuri kwamba tuna vijana wengi katika makutaniko leo walio na nia kama hiyo. Lakini iwe sisi ni vijana au wazee, kuna mambo tuwezayo kufanya tunapoona uhitaji.
4 Je, umepata kuhisi kwamba wengine wana mahitaji ambayo yangehitaji kupewa uangalifu bora zaidi? Labda ndugu au dada alikuwa hospitalini, na wachache walimtembelea; au mtu akawa katika hali ya kutoweza, lakini hakukuwa na mtu wa kutumwa au kusaidia na shughuli za nyumbani. Yesu huona wanaomtumikia Yehova kuwa washirika wa familia ambao walijali mmoja na mwenzake kikweli. (Mk. 3:33-35) Katika kielezi cha kondoo na mbuzi, alionyesha kwamba wale wanaofurahia kuwa katika mkono wa kuume wa upendeleo wa Mfalme wafanya hivyo kwa sababu ya usaidizi wao kwa ndugu za Mfalme.—Mt. 25:40.
5 Naweza Kusaidiaje? Ni jambo gani linaloweza kufanywa ili kuandaa msaada palipo na uhitaji ulio wazi? Je, tungeweza kuchukua hatua ya kusaidia katika njia fulani? Labda kuna wazee-wazee wanaohitaji kitia-moyo, lakini hawana washirika wa karibu wa kuwasaidia. Huenda kukawa na vijana wanaohitaji msaada. Familia mpya inayopendezwa iliyo na watoto kadhaa yaweza kuwepo kwenye Jumba la Ufalme wakati mhubiri anayejifunza nayo hayupo. Wanaweza kuthamini mtu akijitolea kusaidia watoto.
6 Tunapokua katika kupenda kweli na tengenezo la Yehova, pia twakua katika uthamini na hangaikio kwa wengine katika kutaniko. Paulo alitutia moyo tupanuke kwa upande huu. (2 Kor. 6:11-13) Yesu alikazia kwamba kuonyesha upendo sisi kwa sisi ni njia kuu ya kuonyesha kwamba sisi kwa kweli ni wafuasi wake.—Yn. 13:35.
7 Kwa hiyo tuonapo uhitaji, upendo wa kweli kwa ndugu zetu na kwa kutaniko wapaswa utuhamasishe tuchukue hatua ya kusaidia katika njia yoyote tuwezayo. (Gal. 6:9, 10) Hangaikio hili kwa wengine hutuvuta pamoja katika vifungo vya ukaribu vya upendo na umoja. (1 Kor. 10:24) Kwa njia hii, twafanya sehemu yetu ya kusaidia kujaza uhitaji katika kutaniko.