Habari za Kitheokrasi
◆ Jamhuri ya Dominika iliripoti kilele kipya cha wahubiri 11,205 katika Desemba. Mafunzo ya Biblia yaliongezeka asilimia 18 kutoka Desemba uliopita kufika 20,067, na ziara za kurudia ziliongezeka asilimia 25.
◆ Guyana ilipata ongezeko la asilimia 8 zaidi ya wastani wa mwaka uliopita, ikiwa na kilele cha wahubiri 1,468 katika Desemba.
◆ Ailandi ilifikia kilele cha tisa mfululizo cha wahubiri katika Desemba 2,930 wakiripoti. Kilele cha mapainia wa kawaida 298 kiliripotiwa pia.
◆ Kilele kipya cha wahubiri 163,692 kilifikiwa katika Italia wakati wa Desemba, ongezeko la asilimia 5 zaidi ya wastani wa mwaka uliopita. Wahubiri wa kundi walifikia wastani wa saa 13.1 katika utumishi.
◆ Martiniki ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 2,649 katika Desemba kwa ongezeko la asilimia 9, kilele chao cha nne mfululizo cha wahubiri. Siku ya mkusanyiko wao wa pekee ilihudhuriwa na 4,941 na 77 wakabatizwa.
◆ Peru iliendelea kuona ukuzi mzuri kwa kuwa waliripoti kilele kipya cha wahubiri 29,187 kwa Desemba, ongezeko la asilimia 11 zaidi ya mwezi ule ule mwaka mmoja uliopita. Wahubiri wa kundi walifikia wastani wa saa 14.8 shambani.